Teuzi za raisi Trump, Marekani ina mpango gani dhidi ya dunia?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,784
Trump amteua Bolton kuwa mshauri wake mpya wa usalama

> Rais wa Marekani Donald Trump amemuondoa mshauri wake wa usalama wa taifa H.R McMaster na kumteua katika nafasi hiyo John Bolton, mtu mwenye msimamo mkali na aliyewahi kuwa balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa.


=====

Hizi teuzi za Donald Trump zinanifanya nifikiri sana,
Maana watu ambao anawaweka kwenye nafasi nyeti ni wale ambao wanaiangalia dunia katika mtizamo wa tofauti kabisa. Kwanza ni wale Wazalendo sugu yaani wao wanaamini dunia nzima ni Marekani tu. Wapenda vita na vurugu na hata chembe chembe za diplomasia hazipo kwenye kauli zao kabisa...

Haya Waziri wa mambo ya nje Mike Pompeo alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kijasusi CIA na amesikika wazi kabisa akisema yeye atawashughulikia maadui wa Marekani kama Iran, Korea na ambao wanajitegemea kama Wiki-Leaks. Haya kamchagua mama mwingine Gina Haspel kuwa Mkurugenzi wa CIA, huyu mwanamama ni mtata sana na historia yake inafahaika vizuri sana.

Sasa ya leo kali sana,
Bwana John Bolton kuwa Mshauri Mkuu wa mambo ya Usalama.
Hili linjemba lipo tangia enzi za Ronald Reagan, Bush Mkubwa na Bush Mdogo.
Yaani ni libalozi lakini halina hata chembe ya lugha ya staha..Kama alivyofanya Collin Powel kumsingizia Saddam Hussein kuwa na silaha za maangamizi, basi hili linjemba nalo lilikuwepo kwenye hiyo orodha ya watu walioshabikia sana Uvamizi wa Iraq.

NB 1: Kitu kimoja ambacho hawa wateule wa Trump wanacho ni chuki dhidi ya Uchina na Urusi.
Mataifa ambayo Marekani amesema dhahiri kwenye Mkakati wake wa Ulinzi (The National Security Strategy) kwamba wanafanya kazi kuharibu maslahi yake ya kiulinzi na Kibiashara.

Balozi Bolton aliwahi kusema kwenye Fox News kwamba Raisi wa Urusi Vladmir Putin ana akili sana na hilo ndilo linamwogopesha. Upande wa pili huyu jamaa naye anafahamika kwa kushutumu sana Uchina kama ambavyo Steve Bannon anasema kwamba Uchina imeshiriki kuharibu Uchumi wa Marekani. Yeye Bolton anasema Uchina anaiba teknolojia ya Marekani na hivyo ashughulikiwe tu. Kuhusu Korea Kaskazini Balozi huyu anasema jeshi litumike tu.

NB 2: Marekani ni taifa kubwa sana hapa duniani ambalo maamuzi yake yanaweza kuwa na madhara makubwa sana Usalama wa dunia pamoja na hali yake ya kiuchumi. Kipindi hiki chote mambo ambayo yanazungumzwa kuhatarisha usalama wa dunia ni:
  1. Mkakati wa nyuklia wa Korea Kaskazini,
  2. Mkataba wa nyuklia wa Iran,
  3. Hali ya amani nchini Ukraine,
  4. Hali ya amani kwenye Bahari ya Uchina na Taiwan,
  5. Hali ya Uchumi na Usalama Barani Ulaya,
  6. Hali ya Usalam nchini Syria,
  7. Hali ya Usalama nchini Israel na Palestina (kuhusu Yerusalemu)
Hawa washauri wateule wa Rais Trump, Mike Pompeo, Gina Haspel, John Bolton na James Mattis wako kinyume kabisa na mkakati wa mazungumzo ya amani kwenye sehemu yoyote ile niliyotaja hapo juu. Wamenukuliwa wazi kabisa kutaka nguvu ya kijeshi au vikwazo zitumiek dhidi ya maadui wa Marekeni. Mbaya ziaidi ikafika hadi kipindi Trump alitishia kabisa kujitoa kwenye mikataba muhimu ya kiuchumi kwa kudai Marekani analaliwa kiuchumi...

Mwaka 2003 Waziri wa Ulinzi wa Marekani Jemedari James Mattis aliwaambia hivi wanajeshi wa Sadam Hussein: I come in peace," didn't bring artillery. But I'm pleading with you, with tears in my eyes: If you https://jamii.app/JFUserGuide with me, I'll kill you all.".......(Sasa mtu kama huyu leo ndiye waziri wa Ulinzi unategemea nini ???)

Dr. Henry Kissinger, Zbigniew Brzezinski na George F Kennan na ubabe wao wote wa kushabikia vita walifika kipindi wakawa na uelewa kwamba wakicheza vibaya siasa za kimataifa basi Marekani inaweza ikashindwa Vita Baridi japo ina Uchumi mkubwa na nguvu kubwa sana kijeshi, wakaka mezani kufanya mazungumzo ndiyo dunia ikapata matokeo kama Detente, SALT na AMB Treaty: Diplomasia ndiyo ilipelekea hadi Raisi Ronald Reagan kumaliza vita baridi kwa amani mwaka 1989.Zamani kucheza siasa za kimataifa zilikuwa Rahisi sana kwasababu Mataifa mawili ndiyo yalikuwa na sauti (Urusi na Marekani). Lakini siku hizi mataifa yenye silaha na nguvu kijeshi yamekuwa mengi tupilia mbali makundi binafsi ya magaidi au makundi binafsi yanayofanya mashambulizi ya mtandaoni......

Ukweli mchungu ni kwamba,
Mahasimu wa Marekani kama Uchina, Urusi, Iran na Korea Kaskazini wana nguvu kipindi hiki kuliko kipindi chochote kuwahi kutokea huko nyuma. Nilikuwa naangalia The Munk Debate wanazuoni wa Marekani kama Prof. Stephen Cohen, Dr Henry Kissinger walikubali kwamba Marekani ina changamoto kubwa sana kiusalama kuliko wakati wowote ule kwenye historia yake.

Gideon Rachman wa chuo cha Cambridge ameandika kitabu "Easternisation: War and Peace in Asina Century", Prof. Graham Allison wa Harvard University amendika kitabu "Destined for War: Can America and China escape the thucydides Trap (Kilizungumziwa hadi kwenye Bunge la Marekani) ?" wamezungumzia hizi changamoto za Kiuslama za Marekani na kwamba akicheza vibaya imekula kwake. Wengine kama Prof John Mearshimer na Prof. Noam Chomsky waliongea kwenye Council for Foreign Relation na Vyuo mbali mbali vikubwa duniani kwamba Kipindi hiki mambo yamekaa vibaya sana kwa Marekani.

Je, unadhani hawa wateule wa Raisi Trump wanaweza kuitoa Marekani hapa ilipo kwa mabavu kama ambavyo tumeona Marekani ikifanya kwa miaka ishirini iliyopita. AU ndiyo wanaweza wakawa ndiyo chanzo cha uvunjivu wa amani hapa duniani na kuanguka kwa Marekani ?????

Updates:
Haya ni baadhi ya maneno ya wanasiasa wa Marekani baada ya huu uteuzi


Bernie Sanders mgombea Uraisi kwa kupitia Democratic Party anasema hivi:


Senator Jeff Merkley naye ameshangazwa na uteuzi huu akasema hivi:


Senator Ed Merkley naye alisema haya:


NB: Nimesoma hizi tweets kupitia mtandao wa RT News nikagundua kwamba siyo mimi peke yangu ninayeogopa, tupo wengi mno. Nahisi kama kuna vita kubwa sana inakuja huko mbeleni maana huu mwendo siyo mzuri kabisa na haujakaa kirafiki kwenye amani ya dunia:‘Trump lining up war cabinet’? Bolton’s elevation to NSC adviser fuels alarm

CC: Palantir , Iceman 3D , SirChief , Dotworld , Chief , Bukyanagandi , chige, JokaKuu , Nguruvi3 , zitto junior , Da'Vinci , ze kokuyo, Prof, izzo, TUJITEGEMEE , MASAMILA, Consigliere , haa mym , Red Giant, Bavaria, neo1, Bilionea Asigwa , jay-millions, Hussein Melkiory
 
Hi mada nzito sana, ila vyovyote itakavyo kuwa marekan amisha chelewa sana sana kuzuia mataifa kama china, Iran na North Korea kukuwa kijesh na kiuchum. Maamuzi yeyote atakayo chukua lazima yatamgharimu sana
Na ikitokea mataifa hasa wabaya wake wakajua udhaifu wake amekwisha.

Mfano hili la vikwazo vya kiuchum wa biashara alilolianzisha na Uchina wamejibu kwakuongeza kodi kwenye bidhaa zaid ya mia kutoka US, mnyonge hapo ataumia zaid
 
Any miscalculation itawacost wamarekani and the rest

Kuna Professor nguli wa Historia kutoka Chuo cha Oxford ni mzee sanaa.
Anasema kinachoendelea kipindi hiki hakina tofauti na kilichokuwa kinaendelea kabla ya Vita ya kwanza ya dunia.
Anasema kuanzia mwaka 1880's hadi 1914 mambo yalikuwa yanalingana na mambo ya sasa ya dunia yetu:
  1. Kukua sana kwa Utaifa na Uzalendo sugu (Ultra-Nationalism)
  2. Mataifa yalikuwa ni mengi sana na yana mifumo ya kujihami ya Siri (Alliance System) Kama: Entente Cardiale, Tripple Entente, Tripple Alliance, Dreikaiserbund A.K.A The League of three emperors (Kama leo NATO, SEATO, SENTO,ANZUS, European Continental Alliance, Russia & Iran & China)
  3. Propaganda za kisiasa kwenye magazeti zilikuwa zimepamba sana moto kama: The Protocols of the learned elders of Zion (Angalia leo CNN, FOX NEWS, RT NEWS, SPUTNIK, Wiki-Leaks)
  4. Silaha za kisasa zilikuwa zinaonyeshwa ili kutishana kama : Machine Gun Rifle, Nerve Gas, Tanks, Air fighters ( Angalia leo Urusi, Uchina na Marekani wanchokifanya)
  5. Mataifa madogo yakawa na nguvu ghafla kiasi cha kutishia mataifa makubwa kama: Urusi kupigwa vibaya sana na Japan kwenye Russo-Japanese War (Kama ambavyo Korea Kaskazini, Syria na Iran wanavyomtunishia misuli Marekani)
  6. Makundi binafsi ya kigaidi au ya harakati kama: The Union or Death A.K.A The Black Hand walio muua Archduke Ferdinand na Zionists waliopelekea Uturuki kuvunjwa (Angali ISIS, Backwaters, Hamas, Hezbollah na Wiki-Leaks)
  7. Vita za mbali nje ya mipaka yao kugombea makoloni au Ushawishi kama: The Morrocan Crisis 1911 na The Fashoda Crisis 1898 (Angalia kinachoendelea nchini Syria, Ukraine, Korea, Libya, Iraq na Afghanistan)
  8. Kukua kijeshi na kiuchumi kwa mataifa ambayo hayakutegemewa kama: Falme za Ujerumani na Austria-Hungary (Angalia leo Urusi, Uchina, Iran, India na Brazil)
NB: Kinachoendelea hapo hakina tofauti kabisa na kilichotokea kabla ya vita ya Kwanza ya dunia.
Kukosea kidogo kwa mahesabu (Miscalculation) kilisababisha Ulaya nzima ijikute kwenye matatizo ambayo hawakuweza kutoka kabisa.
 
Ili kurudisha USA kama taifa lenye uchumi mkubwa duniani ni lazima Marekani ianzishe vita vya 3 vya dunia dhidi ya China na Urusi. Hao wateule wote wa Rais Donald Trump si watu wa busara na ni War Mongers.
 
NB 2: Marekani ni taifa kubwa sana hapa duniani ambalo maamuzi yake yanaweza kuwa na madhara makubwa sana Usalama wa dunia pamoja na hali yake ya kiuchumi. Kipindi hiki chote mambo ambayo yanazungumzwa kuhatarisha usalama wa dunia ni:
  1. Mkakati wa nyuklia wa Korea Kaskazini,
  2. Mkataba wa nyuklia wa Iran,
  3. Hali ya amani nchini Ukraine,
  4. Hali ya amani kwenye Bahari ya Uchina na Taiwan,
  5. Hali ya Uchumi na Usalama Barani Ulaya,
  6. Hali ya Usalam nchini Syria,
  7. Hali ya Usalama nchini Israel na Palestina (kuhusu Yerusalemu)
Hawa washauri wateule wa Rais Trump, Mike Pompeo, Gina Haspel, John Bolton na James Mattis wako kinyume kabisa na mkakati wa mazungumzo ya amani kwenye sehemu yoyote ile niliyotaja hapo juu. Wamenukuliwa wazi kabisa kutaka nguvu ya kijeshi au vikwazo zitumiek dhidi ya maadui wa Marekeni. Mbaya ziaidi ikafika hadi kipindi Trump alitishia kabisa kujitoa kwenye mikataba muhimu ya kiuchumi kwa kudai Marekani analaliwa kiuchumi...

Je, unadhani hawa wateule wa Raisi Trump wanaweza kuitoa Marekani hapa ilipo kwa mabavu kama ambavyo tumeona Marekani ikifanya kwa miaka ishirini iliyopita. AU ndiyo wanaweza wakawa ndiyo chanzo cha uvunjivu wa amani hapa duniani na ukawa ndiyo mwanzo wa kuanguka Marekani ?????
Big NO!!
Mwanzo wa kuporomoka kwa USA upo chini ya Trump, me nilitarajia siasa zake za "Marekani kwanza" zitaangazia masuala ya kiuchumi kumbe ana base hadi kwenye kuleta vurugu ili apate yeye kwaza!. Ingawa Hillary Clinton tulimuona kama mpenda vita kumbe kuna kichaa mwingine asiyejua marafiki wa kuwaweka karibu yake kapewa madaraka!!.
China ameweza kututeka Africa sio kwa njia ya misaada ya kijeshi yeye Politics zetu hajaamua kujishughulisha nazo kaamua yupo tayari awe dikteta awe nani yeye kwake biashara za maendeleo atafanya naye tu!. Na kwa hili African Nations hatutaweza kaa kimya shuhudia China akipigwa lazima tutaingilia vita ile!.
Kipindi vita itakapoanza wasitarajie Bara lao litakuwa salama hiyo wasahau mataifa sasa hivi yameadvance kwa kiwango kikubwa sana. Njia pekee itakuwa kutumia kila silaha inayopatikana duniani hapa!.
Katika dunia yenye Technological flows kubwa kama ya sasa, Marekani inabidi ijiangalie sana siasa inazoleta!. watu sio wajinga wa kukaa kutawalika.. Tumeshaona matokeo ya Afghanistan, Libya, Iraq, Syria, Yemen na pande zote ambazo alienda!. Matokeo ya Siasa zake ni kuliachia eneo mtifuano hana msaada wowote!.
Kitu kimoja ambacho wanajisahau Marekani ni kuzani Nguvu ya jeshi inaweza waokoa na kuwarudisha kuwa 'world police'. Sijui hawajifunzi dola ya Muingereza, Mrumi, Turks, Spain zilishindwa vipi!?.

Too much power corrupt absolutely
 
Ili kurudisha USA kama taifa lenye uchumi mkubwa duniani ni lazima Marekani ianzishe vita vya 3 vya dunia dhidi ya China na Urusi. Hao wateule wote wa Rais Donald Trump si watu wa busara na ni War Mongers.

Vita ya tatu ya dunia ikianza unadhani Marekani atashinda au atabaki kama alivyo leo hii ???
 
Big NO!!
Mwanzo wa kuporomoka kwa USA upo chini ya Trump, me nilitarajia siasa zake za "Marekani kwanza" zitaangazia masuala ya kiuchumi kumbe ana base hadi kwenye kuleta vurugu ili apate yeye kwaza!. Ingawa Hillary Clinton tulimuona kama mpenda vita kumbe kuna kichaa mwingine asiyejua marafiki wa kuwaweka karibu yake kapewa madaraka!!.
China ameweza kututeka Africa sio kwa njia ya misaada ya kijeshi yeye Politics zetu hajaamua kujishughulisha nazo kaamua yupo tayari awe dikteta awe nani yeye kwake biashara za maendeleo atafanya naye tu!. Na kwa hili African Nations hatutaweza kaa kimya shuhudia China akipigwa lazima tutaingilia vita ile!.
Kipindi vita itakapoanza wasitarajie Bara lao litakuwa salama hiyo wasahau mataifa sasa hivi yameadvance kwa kiwango kikubwa sana. Njia pekee itakuwa kutumia kila silaha inayopatikana duniani hapa!.
Katika dunia yenye Technological flows kubwa kama ya sasa, Marekani inabidi ijiangalie sana siasa inazoleta!. watu sio wajinga wa kukaa kutawalika.. Tumeshaona matokeo ya Afghanistan, Libya, Iraq, Syria, Yemen na pande zote ambazo alienda!. Matokeo ya Siasa zake ni kuliachia eneo mtifuano hana msaada wowote!.
Kitu kimoja ambacho wanajisahau Marekani ni kuzani Nguvu ya jeshi inaweza waokoa na kuwarudisha kuwa 'world police'. Sijui hawajifunzi dola ya Muingereza, Mrumi, Turks, Spain zilishindwa vipi!?.

Too much power corrupt absolutely
China amekutwa ameweka wire za kijasusi kwenye jengo la African Union.

Kwa Africa mataifa yanayomuunga mkono China kabla ya Sakata la African Union kugundua ujasusi linaofanywa kwa kivuli cha misaada kutoka China.

South Africa,
Zimbabwe.
Na South africa wako more or less neutral. Manake wana roho ya kimagharibi lakini wana urafiki na wachina katika Umoja wa BRICS.

Mataifa yanayomuunga mkono USA.
Egypt, Kenya, Libya, Rwanda,
Liberia Morroco, Ghana, Cameroon

Mataifa ambayo ni non allign movement
Tanzania.

Duniani mataifa yanayomuunga mkono na kua na imani na UsA ni mengi kuliko China.
China ana safari ndefu sana mpaka kuja kuvunja ushawishi wa USA duniani.
 
China amekutwa ameweka wire za kijasusi kwenye jengo la African Union.

Kwa Africa mataifa yanayomuunga mkono China kabla ya Sakata la African Union kugundua ujasusi linaofanywa kwa kivuli cha misaada kutoka China.

South Africa,
Zimbabwe.
Na South africa wako more or less neutral. Manake wana roho ya kimagharibi lakini wana urafiki na wachina katika Umoja wa BRICS.

Mataifa yanayomuunga mkono USA.
Egypt, Kenya, Libya, Rwanda,
Liberia Morroco, Ghana, Cameroon

Mataifa ambayo ni non allign movement
Tanzania.

Duniani mataifa yanayomuunga mkono na kua na imani na UsA ni mengi kuliko China.
China ana safari ndefu sana mpaka kuja kuvunja ushawishi wa USA duniani.
Ujasusi wa wire tapping USA na UK wameufanya sana!!.. Mambo yanayoendelea Congo ni matokeo ya USA, UK na France!. Nitajie taifa moja ambalo limekuwa distabillized kwa mgongo wa China Africa or anywhere then nikutajie mataifa yalokuwa distabillized na Hao unaoita waungwa mkono!.
Kusema China ni rafiki mbaya kwa Africa zaidi ya European countries then you are still immature on these stuffs!.
Hivi unaijua ONE BELT ROAD/SILK ROAD!?..
South Africa itoe katika nchi zenye kuhitaji misaada kama Other African Nations, wenzio miaka hiyo walitengeneza hadi Bomu la Nyuklia!. (small london in Africa).
Yani non allign nation umeiona Tanzania pekee!?.
Naona unapingana na ripoti za USA kuhusu China Vs Africa. hongera mkuu!!.
 
Na jana Trump kaanza rasmi vita ya kiuchumi na Uchina,kwa kuanza kutoza kodi kubwa kwa bidhaa zitokazo Uchina,Uchina nao kwa hasira kuu wamesema kuwa watalipiza kisasi,Tatizo kubwa la Marekani,mimi hapa sioni kama ni Trump,tatizo lao ni wivu na hofu tu,kwa mataifa mengine,wanataka wabaki wao tu juu,hawapendi Mataifa mengine yaibuke kiuchumi,kijeshi na mambo mengine.Juu ya huo utata wa wateule wa Trump hiyo ndio tabia halisi ya Wamarekani ,ukorofi,uchokozi,ubabe wa kijinga,dhuluma,na kila aina ya vitimbi.Na hii ni tabia yao ya asili unakumbuka walivyovamia Bara la america ni kuwadhulumu wahindi wekundu haki zao ,wao wenyewe kudhulumiana na kuuana,hawa ndo Ma cow boy. Hata hivyo hawajui kuwa wanatengeneza tatizo jingine,Kauli kama kuzishughulikia NK,Iran,China, ni kuzifanya nazo ziangalie nji mbadala za kujihami.Haya yote anayoyafanya kiduku na urusi kutengeza silaha kalikali ni kutokana na kauli kama za huyo Mshauri wa Usalama wa Trump.Kauli hizi za vitisho ndo baadhi ya nchi wanaziona na kuzichukulia ni kauli rasmi na wanazifanyia kazi,ndi matokeo yake watu wanagundua makombora ya kuingia hadi vyumbani kwa maadui.
Wamarekani huwa wanajiongezea na maadui na kuzalisha wengine siku hadi siku kwa maneno namatendo yao kwa nchi nyingine.
 
China amekutwa ameweka wire za kijasusi kwenye jengo la African Union.

Kwa Africa mataifa yanayomuunga mkono China kabla ya Sakata la African Union kugundua ujasusi linaofanywa kwa kivuli cha misaada kutoka China.

South Africa,
Zimbabwe.
Na South africa wako more or less neutral. Manake wana roho ya kimagharibi lakini wana urafiki na wachina katika Umoja wa BRICS.

Mataifa yanayomuunga mkono USA.
Egypt, Kenya, Libya, Rwanda,
Liberia Morroco, Ghana, Cameroon

Mataifa ambayo ni non allign movement
Tanzania.

Duniani mataifa yanayomuunga mkono na kua na imani na UsA ni mengi kuliko China.
China ana safari ndefu sana mpaka kuja kuvunja ushawishi wa USA duniani.

Duniani mataifa yanayomuunga mkono na kua na imani na UsA ni mengi kuliko China.
China ana safari ndefu sana mpaka kuja kuvunja ushawishi wa USA duniani
Mkuu natofautiana kwa 100% na wewe juu ya Marekani kuwa anaungwa mkono na mataifa mengi , na pia kua Marekani na anaaminika na wengi.
Ukweli ni kwamba Marekani anungwa mkono na kuaminika na nchi chache sana hapa Duniani, isipokua nchi nyingi zinamwogopa kwa sababu ya mabavu yake.Tunaposema nchi, huwa tunamaanisha viongozi,viongozi wa nchi nyingi wanatii matakwa ya marekani kwa kuogopa fitina na hatimae kupinduliwa,mifano ipo mingi sana.Na kila kiongozi anayeitii Marekani huwa anataka ulinzi wa madaraka yake tuu,Mfano wa ambao walikataa kuitii marekani ni pamoja na Hugo Chavez,nini kilimpata,Fidel Castro,Gadafi,Sadam,Al Asad wa Syria,.Huko Ulaya hawamtaki Marekani lakini basi tu wafanyeje,kila siku wanahangaika na kuunda jeshi lao nje ya NATO, EU Army.Marekani hana ushawishi wowowte kama watu wanavyopendaga kusema ni vitisho na fitina tu, chunguza.Misaada ya masharti,na ukikataa, vikwazo vinakuhusu.
 
Vita ya tatu ya dunia ikianza unadhani Marekani atashinda au atabaki kama alivyo leo hii ???
Haya masuala yapo very complicated, always am believing that these things are not happening accidentally; mimi kwa mtizamo wangu kushinda au kushindwa kwa marekani kutategemeana Russia yupo na washirika gani wakati wa vita, let say Russia yupo na China, India, Noth Korea, Iran, Pakistan, Iran na nchi nyingine za Amerika kusini hapa vita itabalance, lakini pamoja na hilo kila nchi itakayo shiriki katika vita hii hasa Russia, nchi za ulaya na Marekani yenyewe zitaharibiwa vibaya sana, again pamoja na uharibifu huo Marekani na washirika wake hasa Israel narudia hasa Israel wataibuka washindi. The war of all war, jamani hii dunia inaelekea kwenye uharibifu kama vita ya kwanza ilichukua miaka minne, ya pili miaka sita hii ya tatu itakuwa nane na kuendelea (sequence and series )
 
Haya masuala yapo very complicated, always am believing that these things are not happening accidentally; mimi kwa mtizamo wangu kushinda au kushindwa kwa marekani kutategemeana Russia yupo na washirika gani wakati wa vita, let say Russia yupo na China, India, Noth Korea, Iran, Pakistan, Iran na nchi nyingine za Amerika kusini hapa vita itabalance, lakini pamoja na hilo kila nchi itakayo shiriki katika vita hii hasa Russia, nchi za ulaya na Marekani yenyewe zitaharibiwa vibaya sana, again pamoja na uharibifu huo Marekani na washirika wake hasa Israel narudia hasa Israel wataibuka washindi. The war of all war, jamani hii dunia inaelekea kwenye uharibifu kama vita ya kwanza ilichukua miaka minne, ya pili miaka sita hii ya tatu itakuwa nane na kuendelea (sequence and series )

Vita ya kwanza ya Dunia mataifa manne tu (Ujerumani, Austria, Bulgaria na Ottoman Empire)yaliweza kupigana na mataifa zaidi ya 14 (akiwemo Muingereza, Mfarasansa, Marekani, Urusi, Ubelgiji, Romania, Ugiriki, Japan) kwa miaka 4 mfululizo. Vita ya pili kulikuwa na Ujerumani, Italia na Japani lakini walifanywa nini Waingereza, Warusi, Wamarekani, na wengineo kwa miaka kama saba hivi ???

NB: Idadi inaweza isiwe sababu pekee ya kushinda vita,
Hasahasa unapopigana na taifa lenye nguvu kubwa ya kijeshi kama Urusi na Uchina.
Jiulize kwanini mataifa ziaidi ya 28 ya NATO yanahangaika na nchi moja tu huko Ulaya kama hana nguvu kubwa ???

Kama vita ya tatu itatokea sidhani kama Barani Ulaya kuna taifa lenye nguvu ya kuweza kumzuia Mrusi kirahisi rahisi bila kutumia Nyuklia, vivyo hivyo Barani Asia sidhani kama Japan, Vietnam, India , Taiwan na Korea kusini wanaweza kumzuia Uchina kirahisi.

Kule Barani Marekani sidhani kama kuna taifa linauwezo wa Kushinda nguvu ya Kijeshi ya Marekani na Canada kwasababu Brazil, Arjenitina, Venezuela na Cuba wakiwekwa kwa pamoja kuyashinda haya mataifa mawili ni ngumu sana.

Tusiombe hii vita itokee kwasababu ikiisha hakutakuwa na taifa ambalo litakuwa Super Power. Watu watakufa sana sanaaa na kutakuwa na njaa na umasikini mkubwa haujawahi tokea...!
 
Back
Top Bottom