eh wana jf wakali,jamaa ameuliza tu..
jamani nimesikia tetesi kuwa vengu yule msanii wa ze komedy kuwa hatunaye. Nimezipata habari hizi kwa mtu aliyenithibitishia. Lakini kupata uthibitisho zaidi nimelileta kwenu jamvini kwa mwenye taarifa za ndani zaidi atueleze.
Kama uliiona ulichukua hatua gani? yaani mpaka uone ninihii ndo u......Ata mimi nimeiona hii habari kwa facebook
Hata mie mkuu najiuliza hapa nilipo hawa wananchi wa Jf wakoje? Mbona jamaa wanataka kumtoa macho wakati jamaa anaulizia kwa yule aliye na taarifa! Kwani kuna ubaya gani kuuliza eti nimesikia fulani kafariki mwenzangu una taarifa zozote? Jamani hebu tuwe na kiasi! Kama huna taarifa si unakaa kimya! Eboo!
Ajisikieje wakati kauliza jamani,kwani taarifa ya msiba mtu anaposikia si huwa anauliza kupata uhakika??
Hata mimi nimesikia leo LAKINI SIO KUTHIBITISHA na kwa bahati mbaya aliyeniambia namuamini kwa nae yupo India amesindikiza Mgonjwa wake lakini nikawasiliana na mwenzao mmoja katika kundi lao amesema hawajapata hiyo taarifa, nikaona ninyamaze kwanza maana sijui niulize wapi tena japo mtoa habari wangu anadai ni kweli.
Sina nia ya kupotosha.
Utajisikiaje akija jamaa hapa kwenye forum na kusema kunatetesi bibikuku amafariki utajisikiaje? Tena labda ulikuwa unaumwa, utajisikiaje ww?
Na mimi nilipata habari hizi, halafu nikaonana naye live, akanithibitishia habari hiyo!Jamani mpaka sasa hakuna mwenye uhakika na taarifa hizi?