Ni kweli Mwl. Nyerere alijitahidi sana lakini bado nikikumbuka haya machache yafuatayo kati ya mengi nasikia machungu sana.
§ Tulitembea kilomita nyingi kufuata zahanati na ukifika huko uongee faragha na daktari umpe chochote ndiyo upate matibabu.
§ Hatukuweza kumudu kunywa chai, sukari ilikuwa haipatikani hali ya kuwa pesa tunazo.
§ Tulifulia nguo kwa kutumia majani ya mpapai au mrenda, sabuni ilikuwa shida kufipatikani. Nakumbuka sabuni za mbuni, gardenia, Ilula nk. Ilikuwa ni issue kuzipata.
§ Maduka ya kaya na RTC walikuwa ni miungu watu kwa vile bidhaa muhimu zilikuwa adimu
§ Nakumbuka wazanzibari walivyokuwa wanatuchukulia dada zetu kilahisi shauri ya kupe kitu kidogo kama collogate tu
§ Kumiliki redio cassete tu ilikuwa issue lakini hivi sasa hata msukuma mkokoteni anamiliki TV
§ Mmiliki wa pikipiki wakati huo alihesabika kuwa ni tajiri lakini hivi sasa hata muuza genge anaweza kumiliki bodaboda.
§ Nakumbuka tulivyokuwa tunavaa nguo sare za kiwanda cha Urafiki na viatu sare vya kampuni za Bora shoes na Moro shoes kama watoto wa shule, lakini navyo kupata ilikuwa ni issue mpaka ulanguliwe.
§ Ukitaka kusafiri kwenda bara wakati huo usafiri ni mabasi ya kampuni ya Kamata au Treni uweke booking miezi miwili au mitatu kabla.
§ Usafiri wa mjini kwa kutumia UDA ni balaa watu wanagombea kuingia ndani ya bus kwa kupitia madirishani.
§ Timu za michezo zilikosa sare za michezo, ilkuwa ni kawaida timu kubwa kama Simba na Yanga kuiona sare ya aina moja kwa miaka miwili bila ya kubadilisha.
§ Ukitaka mawasiliano ya simu ni issue, ni jambo la kawaida pale Dar maeneo ya usahilini kama Temeke, Tandika, Ilala, Buguruni na Magomeni, mtaa mzima ukakosa mtu mwenye simu kuweza kuwasiliana pindi itokeapo dharura ya msiba nk.
§ Rushwa ilienea kila sehemu hata kwa mambo madogo madogo na ilitambulika kwa majina mengi kama vile mrungula, propoza, mlango wa nyuma, zunguka mbuyu, shati la mikono mirefu, chai, mchicha, hongo nk.
§ Bidhaa muhimu kama mchele, unga wa sembe, unga wa ngano, sabuni, mafuta ya kupikia, dawa ya meno, mabati, saruji, viatu, nguo, nk. Havipatikani isipokuwa kwa kutoa hongo.