Papaa Gx
JF-Expert Member
- Oct 10, 2016
- 10,085
- 15,664
Michuano mikubwa ya Tennis kwa upande wa Gland Slam imeanza kutimua vumbi hii leo huko Australia katika jiji la Melbourne. Michuano hiyo mikubwa inatarajiwa kufika ukomo hapo tarehe 2 ya mwezi wa pili 2020.
Wakongwe katika mchezo huo Roger Federer, Novak Djokovic pamoja na Rafael Nadal wanatarajia kushiriki katika michuano hiyo. Bigwa mtetezi Novak Djokovic anatarajia kutetea ubingwa wake.
Kwa upande wa wanawake bigwa mtetezi Naomi Osaka itampasa apambane ili kutetea ubingwa wake huku akisaka Gland Slam ya tatu.
Kwa upande wa mgao wa fedha kwa mwaka huu ni asilimia 13.6 zilizo ongezeka katika jumla ya fedha ya mgao. Mshindi ataibuka na kiasi cha dola 2,853,079 sawa na Tsh 6,562,081,700 huku mshindi wa pili akiibuka na kiasi cha dola 1,431,002 sawa na Tsh 3,291,304,600.
Wadau wa mchezo huu pedwa kina Victoire niah Mgagaa na Upwa Penison Ole BAK na wengineo wote karibuni hapa tujadili yanayo endelea huko Australia.
Wakongwe katika mchezo huo Roger Federer, Novak Djokovic pamoja na Rafael Nadal wanatarajia kushiriki katika michuano hiyo. Bigwa mtetezi Novak Djokovic anatarajia kutetea ubingwa wake.
Kwa upande wa wanawake bigwa mtetezi Naomi Osaka itampasa apambane ili kutetea ubingwa wake huku akisaka Gland Slam ya tatu.
Kwa upande wa mgao wa fedha kwa mwaka huu ni asilimia 13.6 zilizo ongezeka katika jumla ya fedha ya mgao. Mshindi ataibuka na kiasi cha dola 2,853,079 sawa na Tsh 6,562,081,700 huku mshindi wa pili akiibuka na kiasi cha dola 1,431,002 sawa na Tsh 3,291,304,600.
Wadau wa mchezo huu pedwa kina Victoire niah Mgagaa na Upwa Penison Ole BAK na wengineo wote karibuni hapa tujadili yanayo endelea huko Australia.