KESSY FRANCIS
Member
- Nov 9, 2011
- 42
- 11
TENGA AKUBALIANA NA MAAMUZI YA SERIKALI
Watanzania sasa wanafahamu na Ulimwengu kuwa soka la Tanzania liko rehani kwa ajili ya uamuzi wa kiongozi wake TENGA kwa kuamua makusudi kuandika historia mpya ya kupambana na mabadiliko ambayo Watanzania na wapenda michezo wote, wangependa kuona soka la nchi hii linapiga hatua kubwa na kuwa kichocheo kikubwa cha vijana kujiajiri na kuongeza kipato, lakini yote hayo yamegonga mwamba chini ya uongozi wa KIFEDHULI wa TENGA.
Tenga alianza vizuri kidogo lakini anaondoka Madarakani huku akiwa amekandamiza demokrasia kwa kiwango cha juu sana kwani ametawala kiimla.
Mabadiliko ya katiba aliyofanya kwa kutumia waraka kubadilisha sehemu muhimu ya katiba haikuwa sawa, kwani alipaswa kikatiba kuitisha mkutano mkuu ili theluthi mbili ya wajumbe HALALI wapitishe mabadiliko, cha ajabu matakwa ya katiba hayakufuatwa na ushahidi upo.
Wapo WAJUMBE waliokata mchakato na kususia na wakaonekana wasaliti. Vitimbi vya kukaba roba demokrasia havikuishia hapo bali alienda mbali zaidi katika mchakato Mzima wa kuwapata viongozi wapya baada ya kudiriki kuwatupa nje wapinzani wake 2008 ( MALINZI) kwa vigezo vya kuwa hana uzoefu ( huku akiwa amesahau walivyochuana nyuma) n.k.
Hizi hoja zimekuja wakati ambapo Malinzi amekuwa tishio kwake na wagombea anaotaka kuwaweka, hatimaye Malinzi akakatwa jina vigezo vya kihayawani. Lakini mpaka sasa kikatiba kulipaswa kuwa na safu ya UONGOZI mpya maana kikatiba TENGA si kiongozi tena.
Ameweka kiongozi mmoja mmoja kugombea! Hiyo ndio demokrasia ya Tenga tunayemfahamu.
Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo walieleza kuwa habari yao na TFF inaeleweka na halipotoshwi.
Kimsingi yapo mambo 4 Wizara ilisisitiza.
1. TFF wafuate kifungu cha katiba yao cha kufanya mabadiliko, maana hakikufuatwa
2. TFF wafuate sheria na taratibu za Baraza la Michezo kusajili katiba iliyorekebishwa kihalali, ambazo hawakufuata
3. Serikali haijaiingilia TFF wala FIFA, Bali inawasaidia wao kufuata utaratibu uliokubaliwa na wote.
4. Kuepuka migogoro isiyo ya lazima na kuheshimu sheria za nchi na zao.
Hii tabia ya Tenga kuvurunda kwa kutumia mwavuli wa FIFA kamwe haitampeleka mbali zaidi ya kuonekana anasaliti nchi yake kwa maslahi yake binafsi.
CHA kufanya ni TENGA kuitisha mkutano Mkuu ili moja wapitishe mabadiliko ya katiba na pili wafanye UCHAGUZI wao wa kikatiba.
Serikali isifumbie macho maovu ya Tenga kwani kukaidi maagizo ya serikali ni dalili ya kutaka taifa kufungiwa na FIFA na akumbule TFF aliikuta na ataiacha na ameandika historia CHAFU ambayo kizazi na kizazi watamlalamikia kwa uamuzi wake wa KIBINAFSI.
Watanzania sasa wanafahamu na Ulimwengu kuwa soka la Tanzania liko rehani kwa ajili ya uamuzi wa kiongozi wake TENGA kwa kuamua makusudi kuandika historia mpya ya kupambana na mabadiliko ambayo Watanzania na wapenda michezo wote, wangependa kuona soka la nchi hii linapiga hatua kubwa na kuwa kichocheo kikubwa cha vijana kujiajiri na kuongeza kipato, lakini yote hayo yamegonga mwamba chini ya uongozi wa KIFEDHULI wa TENGA.
Tenga alianza vizuri kidogo lakini anaondoka Madarakani huku akiwa amekandamiza demokrasia kwa kiwango cha juu sana kwani ametawala kiimla.
Mabadiliko ya katiba aliyofanya kwa kutumia waraka kubadilisha sehemu muhimu ya katiba haikuwa sawa, kwani alipaswa kikatiba kuitisha mkutano mkuu ili theluthi mbili ya wajumbe HALALI wapitishe mabadiliko, cha ajabu matakwa ya katiba hayakufuatwa na ushahidi upo.
Wapo WAJUMBE waliokata mchakato na kususia na wakaonekana wasaliti. Vitimbi vya kukaba roba demokrasia havikuishia hapo bali alienda mbali zaidi katika mchakato Mzima wa kuwapata viongozi wapya baada ya kudiriki kuwatupa nje wapinzani wake 2008 ( MALINZI) kwa vigezo vya kuwa hana uzoefu ( huku akiwa amesahau walivyochuana nyuma) n.k.
Hizi hoja zimekuja wakati ambapo Malinzi amekuwa tishio kwake na wagombea anaotaka kuwaweka, hatimaye Malinzi akakatwa jina vigezo vya kihayawani. Lakini mpaka sasa kikatiba kulipaswa kuwa na safu ya UONGOZI mpya maana kikatiba TENGA si kiongozi tena.
Ameweka kiongozi mmoja mmoja kugombea! Hiyo ndio demokrasia ya Tenga tunayemfahamu.
Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo walieleza kuwa habari yao na TFF inaeleweka na halipotoshwi.
Kimsingi yapo mambo 4 Wizara ilisisitiza.
1. TFF wafuate kifungu cha katiba yao cha kufanya mabadiliko, maana hakikufuatwa
2. TFF wafuate sheria na taratibu za Baraza la Michezo kusajili katiba iliyorekebishwa kihalali, ambazo hawakufuata
3. Serikali haijaiingilia TFF wala FIFA, Bali inawasaidia wao kufuata utaratibu uliokubaliwa na wote.
4. Kuepuka migogoro isiyo ya lazima na kuheshimu sheria za nchi na zao.
Hii tabia ya Tenga kuvurunda kwa kutumia mwavuli wa FIFA kamwe haitampeleka mbali zaidi ya kuonekana anasaliti nchi yake kwa maslahi yake binafsi.
CHA kufanya ni TENGA kuitisha mkutano Mkuu ili moja wapitishe mabadiliko ya katiba na pili wafanye UCHAGUZI wao wa kikatiba.
Serikali isifumbie macho maovu ya Tenga kwani kukaidi maagizo ya serikali ni dalili ya kutaka taifa kufungiwa na FIFA na akumbule TFF aliikuta na ataiacha na ameandika historia CHAFU ambayo kizazi na kizazi watamlalamikia kwa uamuzi wake wa KIBINAFSI.