Tembo toka Kenya wanafilisi wananchi Wilayani ROMBO

sirluta

JF-Expert Member
Nov 28, 2012
6,325
2,491
Tembo toka katika mbuga ya TSAVO nchini Kenya wamevamia makazi na kuharibu mazao katika baadhi ya maeneo yanayopakana na Kenya Wilayani Rombo.

Vijiji vilivyoathirika ni kama Kirongo Chini, Letto, Tangwa, Maweteta, Lotiro, Msaranga, n.k

Aidha mazao yaliyoharibiwa ni kama Mihogo, Mbaazi, Migomba, Alizeti, Mtama, n.k

Kwa miaka mingi sasa, tembo kutoka Kenya wamekuwa wakiharibu makazi, mazao na hata kuua watu katika maeneo hayo Wilayani huko, na hivyo wananchi hao wakipata hasa pamoja na kukumbwa na baa la njaa kutokana na uharibifu huo unaofanywa na tembo hao huku wakiwa hawana wa kuwasemea shida hiyo.

Rai kwa Serikali: Ni vema tembo hao wadhibitiwe kwani wanasababisha madhara makubwa kila mwaka na hayafiki sehemu husika. Kwa siku huingia hadi tembo 20 kwa msimu huu wa chakula hivyo huharibu kila kitu. Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii idhibiti hali hiyo na pia tembo hao hawana tofauti na wahamiaji haramu .

Nina imani suala hili litapata msukumo wa kukabiliana nalo mapema.
 
Si sawa kusema ni tembo wa Kenya. Ni mali ya nchi wanapokuwa wakati husika.
 
Kweli mkuu wiki iliyopita pia vifaru 3 walionekana maaeneo ya mwika makerere wanadaiwa kutokea kenya ilibidi wanaakijiji waache shughuli zao wajifungie hadi askari wanyama pori walipofanikiwa wakamata
 
Kweli mkuu wiki iliyopita pia vifaru 3 walionekana maaeneo ya mwika makerere wanadaiwa kutokea kenya ilibidi wanaakijiji waache shughuli zao wajifungie hadi askari wanyama pori walipofanikiwa wakamata
Kweli mkuu wiki iliyopita pia vifaru 3 walionekana maaeneo ya mwika makerere wanadaiwa kutokea kenya ilibidi wanaakijiji waache shughuli zao wajifungie hadi askari wanyama pori walipofanikiwa wakamata
ni hatari sana kwa wanyama kama hao kujichanganya kwenye makazi ya wananchi
 
Mkuu wanyama hawana geographical boundaries, issue ya hao tembo ni ndogo sana , inahitaji mamlaka ya uhifadhi hapo iwasaidie ku manage wasilete hasara zaidi, hata hivyo hilo si suala la serikali sana, ni ishu ya mazingira..........
 
Mkuu wanyama hawana geographical boundaries, issue ya hao tembo ni ndogo sana , inahitaji mamlaka ya uhifadhi hapo iwasaidie ku manage wasilete hasara zaidi, hata hivyo hilo si suala la serikali sana, ni ishu ya mazingira..........
mazingira kvp? Na ni mamlaka ipi ina jukumu hilo? Ya Kenya ama Tanzania?
 
mazingira kvp? Na ni mamlaka ipi ina jukumu hilo? Ya Kenya ama Tanzania?
Mamlaka za uhifadhi za nchi mbili lazima zishirikiane ku wa control hai tembo, na Si issue ya kiserikali Sana Kama wengi wanavyotaka kuamini...ni suala la kiutendaji zaidi.....
 
Back
Top Bottom