Tekinolojia inayotumiwa na whatsapp ya ENCRYPTION

Tekinolojia inayotumiwa na whatsapp ya ENCRYPTION

Ingia kwenye link hapo chini ufanye vyote vinavyotakiwa alafu ulete feedback
Here
Tatizo huelewi kuwa sheria ina mipaka, wakati teknolojia 'haina' mipaka. Mtu aliyeomba ushauri ameomba kwa kutegemea mchango wa kisheria na kiteknolojia. Kiteknolojia, encryption ni kitu kidogo sana maana keys zinaweza kuwa broken, hivyo encryption sio 100% safe. Kisheria, kuna utaratibu wa kukusanya ushahidi unaokubalika mahakamani.
 
Duh! kumbe encryption hamna kitu!! hehe sikujuaga! au unaongelea caesar cipher sio AES
Unaleta ujuaji tu. Kwa mujibu wa theory ya encryption, kila cipher yaweza kuwa broken-it is just a matter of time and computing power. Tofauti kubwa kati ya Caesar na AES ni number of possible keys tu.
 
Ingia kwenye link hapo chini ufanye vyote vinavyotakiwa alafu ulete feedback
Here
Feedback ya kitu gani? Hiyo ni app unayoinstall kwenye simu sasa TCRA wameinstall app zao kwenye simu za watanzania wote?
End to end encryption maana yake ujumbe unasomeka kwa mtumaji na mpokeaji so obviously ukiinstall App inaweza ikasoma message zako hasa kama upo rooted.
TCRA na mtu yoyote mwingine hana uwezo wa kusoma msg za WhatsApp zikiwa hewani.
 
hiyo whatsapp encryption imetajwa na Wikileaks kwenye Vault7/Year 0 kwamba ni moja ya vitu ambavyo CIA wanaweza compromise!
Ila nafikiri hii ni moja ya body kubwa sana hivo kwao ku hack kitu kama hiki sio ajabu sana na hii ni kinyume na kwetu huku kwa hao jamaa unaowaita TCRA!

Hii sio kweli, actually leak ya Vault 7 inaonyesha kuwa encryption za WhatsApp na Signal zinafanya kazi, CIA wanafanya compromise zao kwa kuinstall software/malware kwenye simu za watumiaji so wanaipata message kabla haujaituma na haiko encrypted, hawana uwezo wa kuisoma hewani.

Hii maana yake ni kwamba inabidi uinstall malware katika simu ya kila unayetaka kumfuatilia kitu ambacho ni kigumu sana, hauwezi kufanya mass surveillance ya wananchi wote kwa style hii.
 
Mawasiliano yana sehemu tatu: 1) sender 2)medium 3)receiver:
Ukitaka kudukua mawasiliano unaweza ukafanya katika sehemu hizo tatu. End-to-end encryption ina maana hakuna mtu katikati anaweza kufuatilia mawasiliano yenu kwa sababu kabla ujumbe haujatumwa unafungwa(encrypted) na haufunguliwi mpaka ufike kwa receiver(decryption).

Hii whatsup mpya ni tofauti na huduma ya ujumbe wa simu (SMS) ambako kati ya sender na receiver kuna makampuni ya simu. Ujumbe unatumwa kama ulivyo bila kufungwa, unapokelewa na server za makampuni ya simu na baadae kutumwa na server hizo kwa mhusika(receiver). Hivyo ukifuta ujumbe kwenye simu yako au ya anayetumiwa, makampuni ya simu bado yanakuwa na messeji mlizotumiana katika server zao na wanawapatia polisi na vyombo vingine vya dola wakitaka kwa sababu wao wako katikati ya mawasiliano yenu. Hivyo whatsapp ni bora kuliko sms ya kawaida kwa sababu hakuna namna polisi watapata mawasiliano yenu kama sender au receiver hakuwapatia.

So TCRA bado wanakamata kwa sababu receiver anawapatia taarifa zako. Kumbuka kwenye sms za kawaida, hata usipowapatia, bado wataenda Voda,Tigo,Zantel,nk na kuyapata hayo mawasiliano.

Ushauri kisheria:
Ukihisi ujumbe wa whatsup umepelekwa kwa 'wasiohusika':
  • Kwanza ufute huo ujumbe/chat nzima baina yako na huyo aliyekutumia
  • Ondoa whatsapp katika simu yako
  • factory reset
  • usimpe email address yako mtu yeyote. Au ukitakiwa kutoa email address-toa tofauti naile uliyojiungia whatapp au uliyotengenezea account ya simu zako. Unique ID ktk smartphone ni email address-sio namba ya simu
Hizi hatua hazimaanishi huwezi kupatikana na hatia-zinafanya wahusika washindwe kuthibitisha 'pasipo shaka' kwamba ulitenda kosa. Kumbuka, number za simu zinaweza kufekiwa (phone number spoofing), pia hata email address zaweza kughushiwa. Naweza kabisa kufungua akaunti yangu ya email kwa jina la Donald Trump na kuitumia bila shida(dtrump@gmail.com). Hivi vitu vinafanya kuthibitisha pasipo shaka kwamba ulitenda kosa kuwa ngumu.

Wanaokukamata wanatakiwa wa'clone' simu yako na ya huyo aliyesnitch-hawatakiwi kufanyia uchunguzi wao na kuandaa ushahidi kwa kutumia simu halisi kwa sababu kuna uwezekano wa kuharibu ushahidi.
Nimekuelewa mkali wangu
 
Back
Top Bottom