mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 11,867
- 8,271
Jamani kwa kweli hili sakata limetufumbua wengi,mimi asilani nilikuwa sijui aina ya wabunge na viongozi tulionao,na juzi ndio kwa mara ya kwanza nimesikia baadhi yao wakichangia ripoti ya tume,kusema ukweli kwa sampuli hii ya wabunge tulionao sidhani na siamini kabisa kama tunawezakulitegemea hili bunge hasa kwa wabunge wa chama tawala ambao ndio wengi.
Na nimeshtushwa na uzalendo walionao hao wabunge wa CCM kwa chama chao kuliko maslahi ya nchi ambayo yanawagusa wapiga kura zao.Pia ukiacha ushabiki hata uwezo wa kujenga hoja au kujua na kupima wanachoongea upo chini sana,nimeshangaa wabunge wa upinzani wameonyesha uwezo mkubwa wa kujenga hoja kuliko mipasho ya hawa wabunge wa CCM.Pia imenishangaza sana hata wabunge wasomi wa CCM wamegeuka mbumbumbu sijui dhamira zao haziwasuti.
Kwa mwelekeo huu tunapiga hatua mia nyuma na kwenda nusu hatua mbele,ni muda hao wabunge wangeanzia kupitia hansard kusikia yale wabunge wa zamani walivyokuwa wanawateteawananchi,akina mzee Tuntemeke Sanga,Kasaka,Kabuye,Nandonde,Ngalai.
Na katika maisha yangu sijawahi kusikia matusi bunge lilipokuwa na maspeaker kama Chifu Adam Sapi na Pius Msekwa,hata Mzee wa Viwango (wakati ule sio sasa)walikuwa kweli ma speaker,huyu wa sasa anavuna alichopanda kwa kifupi hana haiba wala uwezo wa kuwa speaker hata Zungu amemzidi kwa kiasi kikubwa,I wish Azzan Zungu angekuwa speaker kuliko huyu madame speaker,speaker gani anababaika kiasi hicho anashindwa kutumia kiti kutoa maamuzi yake?
Speaker gani anashindwa eti kujua jinsiya kuandika vizuri(kumpaka mafuta ya mgongo raisi)ili eti raisi asijue kama anamwingilia?je wakati wabunge wanapika kelele za wasurubiwe wasurubiwe akina Kagasheki,Nchimbi,Nahodha ,Ngereja je walikuwa hawaingilia mamlaka ya raisi?je huu si undumila kuwili wa bunge letu?kwanini wengine walazimishwe kujiuzuru na wengine waachiwe mpaka wapende wenyewe.
Na nimeshtushwa na uzalendo walionao hao wabunge wa CCM kwa chama chao kuliko maslahi ya nchi ambayo yanawagusa wapiga kura zao.Pia ukiacha ushabiki hata uwezo wa kujenga hoja au kujua na kupima wanachoongea upo chini sana,nimeshangaa wabunge wa upinzani wameonyesha uwezo mkubwa wa kujenga hoja kuliko mipasho ya hawa wabunge wa CCM.Pia imenishangaza sana hata wabunge wasomi wa CCM wamegeuka mbumbumbu sijui dhamira zao haziwasuti.
Kwa mwelekeo huu tunapiga hatua mia nyuma na kwenda nusu hatua mbele,ni muda hao wabunge wangeanzia kupitia hansard kusikia yale wabunge wa zamani walivyokuwa wanawateteawananchi,akina mzee Tuntemeke Sanga,Kasaka,Kabuye,Nandonde,Ngalai.
Na katika maisha yangu sijawahi kusikia matusi bunge lilipokuwa na maspeaker kama Chifu Adam Sapi na Pius Msekwa,hata Mzee wa Viwango (wakati ule sio sasa)walikuwa kweli ma speaker,huyu wa sasa anavuna alichopanda kwa kifupi hana haiba wala uwezo wa kuwa speaker hata Zungu amemzidi kwa kiasi kikubwa,I wish Azzan Zungu angekuwa speaker kuliko huyu madame speaker,speaker gani anababaika kiasi hicho anashindwa kutumia kiti kutoa maamuzi yake?
Speaker gani anashindwa eti kujua jinsiya kuandika vizuri(kumpaka mafuta ya mgongo raisi)ili eti raisi asijue kama anamwingilia?je wakati wabunge wanapika kelele za wasurubiwe wasurubiwe akina Kagasheki,Nchimbi,Nahodha ,Ngereja je walikuwa hawaingilia mamlaka ya raisi?je huu si undumila kuwili wa bunge letu?kwanini wengine walazimishwe kujiuzuru na wengine waachiwe mpaka wapende wenyewe.