Tecno ni halisi, ni orijino na kamwe haziwezi kuwa bandia

Eric Mkomoya

Member
Oct 10, 2014
55
56
Katika kampuni za simu, Tecno ni kampuni bomba inayojali wateja wake na ndio maana tunawaelekeza wateja na watumiaji wote wa bidhaa za Tecno, kumekuwa na maneno ya upatu kuhusu simu za Tecno kuwa bandia, lakini upatu hauwezi kubadilisha uhalisia wa Tecno usiogope, jiamini, amini Tecno, usiandikie mate na wino ungalipo, Kamwe Tecno hazitafungwa kupitia TCRA. Hapa kuna hatua za kufahamu kama simu yako ni orijino au la, simu iliyotumika hapa ni Tecno C8.
  • Andika *#06# kisha bonyeza kitufe cha kupiga
  • Baada ya hapo simu yako itakuletea IMEI namba, ambapo kama simu yako ina laini mbili basi zitakuja IMEI namba zikiwa mbili, lakini unapaswa kutumia mojawapo kati ya hizo mbili. Kama zinavyoonekana hapo chini.

  • Namba hii pia unaweza kuipata nyuma ya simu ukitoa betri na utaijua kwani huwa na tarakimu 15, kwa simu zisizohamishika betri namba hizo utazipata mwanzoni ukishatoa mfuniko wa simu yako.
  • Nakili namba hizo pembeni.
  • Iandike ile namba kwenye sehemu ya kuandikia ujumbe(message)
  • Utume ujumbe huo kwenda namba 15090, kama inavyoonekana kwenye picha.
  • Baada ya kutuma jumbe, utaangaliziwa aina ya simu na mtengenezaji, mfano Tecno Telecom Limited na aina ya simu ni C5.
  • Subiri majibu kwa ujumbe mfupi haitachukua muda.
  • Ujumbe huo ukija unakuwa na Kampuni iliyotengeneza simu hiyo pamoja na aina ya simu basi ujue simu yako ni orijino kama inavyoonekana hapo chini.

Hapo tayari, simu inaonekana kuwa ni orijino kwani ina jina la mtengenezaji ambaye ni kampuni ya Tecno yaani Tecno Telecom Limited na aina ya simu ni Tecno C5. Furahia bidhaa za Tecno kwani zimeenea karibu nchi zote Afrika, Ulaya na Asia.
 
Ni nchi gani ya Ulaya inayotumia Tecno? Hata nchi za Asia nna mashaka labda huko China. Kampuni ya Tecno imelenga soko la Afrika tu. Inawezekana zisifungiwe lakini hata kama zitaendelea kutumika bado ukweli uko palepale kwamba simu za Tecno hazina kiwango na ni hitari kwa afya yako.
 
Ni nchi gani ya Ulaya inayotumia Tecno? Hata nchi za Asia nna mashaka labda huko China. Kampuni ya Tecno imelenga soko la Afrika tu. Inawezekana zisifungiwe lakini hata kama zitaendelea kutumia bado ukweli uko palepale kwamba simu za Tecno hazina kiwango na ni hitari kwa afya yako.
Nyasiro TBS wanalifahamu hilo?
 
Tusikubali kuwa kasuku kwa kila kitu, umemsikia rafiki ako mtaani anasema kuwa ni hatari na wewe linakukaa kichwani, bila kutafuta angalau vigenzo ambavyo ukiulizwa kuthibitisha juu ya unachokihubiri unashindwa kutoa proved data/scientific reports, unakuja na maneno yako mengi ya kuungaunga.
 
Sikatai kuwa zaweza kuwa hatari, lakin nitakubaliana na wewe kama ukinipa ushahidi toshelevu kuonesha hatari yenyewe na ni kwa kiasi gani (usitumie maneno bila data), na ni vizuri ukatupa ripoti/ studies zinazoonesha uhatari wa tecno.
Kikawaida nchi zote kubwa duniani kunakuwa na chombo kinachopima simu zinazoingia nchini mwao. mifano ya hivyo vyombo ni kama TENAA (china), FCC (marekani) na nchi ambazo hazina vyombo vyake hutumia standard za vyombo vyengine, mfano India nae anatumia FCC.

huku kwetu hatuna kabisa hivi vyombo ndio maana kila mtu analeta simu huku. utakuta simu haiuzwi ulaya na china kwenyewe ila inaletea Africa wenyewe watakudanganya tuna target soko la Africa kumbe uhalisia ni kwamba wanaogopa kupimwa simu zao hazina viwango hivyo wanaleta huku kwetu ambapo hatupimi.

na ubaya wa hii mionzi haina madhara ya papo kwa hapo useme utaungua ueke ubandike plasta yaishe, bali madhar yanaweza kuwa madogo madogo na kudhuru hadi vizazi vijavyo.

na sidhani kama hili suala ni gumu kwetu kama nchi sababu standard tayari zipo ni suala tu la kuamua sisi tunatumia ipi na kuanza kuchukua sample za kila aina ya simu inayoingia nchini,
 
TECNO inawezekana zikakidhi vigezo kwa maana, hapa kagera kuna site moja tupo na wachina wana simu ka za kwetu hizi tecno na itel, je zingelikuwa na madhara wangetumia? japo kwa upande wa smartphone wanatumia simu zimeandikwa 4G CHINA MOBILE PHONE
 
donbeny nisaidie jinsi ya ku reset simu tecno h6 maana inanisumbua nimejaribu njia ya kawaida lakin waap? msaada bandugu..
Nenda kwenye setting,then check backup & reset click it utaona factory data reset baada ya hapo ukibonyeza itakuuliza unataka kureset na memory yote kwenye phone will be deleted ,say yes and it will reset
 
Hakuna tofauti kubwa kati ya techno na simu nyingine kwa matumizi ya watu wengi, matumizi muhimu kwa simu yote techno zinaweza, watu wengi utamkuta na simu ta ghali muulize anafaidi nini zaidi ya mwenye techno, hana jibu zaidi ya kukwambia aah techno sio simu.
 
Tecno sio feki ila hili jina lake ndo inaiweka njia panda. Awali walivyoanza ilianza km cm feki toka China, wakati ule Nokia alikuwa kwenye kilo bado. Pale smartphone ilipoanza kuvuma, tecno walitakiwa kuweka logo na jina jipya. Kulingana ujio wa smartphones, ili kuondoa dhana mbaya juu yake.
 
Kikawaida nchi zote kubwa duniani kunakuwa na chombo kinachopima simu zinazoingia nchini mwao. mifano ya hivyo vyombo ni kama TENAA (china), FCC (marekani) na nchi ambazo hazina vyombo vyake hutumia standard za vyombo vyengine, mfano India nae anatumia FCC.

huku kwetu hatuna kabisa hivi vyombo ndio maana kila mtu analeta simu huku. utakuta simu haiuzwi ulaya na china kwenyewe ila inaletea Africa wenyewe watakudanganya tuna target soko la Africa kumbe uhalisia ni kwamba wanaogopa kupimwa simu zao hazina viwango hivyo wanaleta huku kwetu ambapo hatupimi.

na ubaya wa hii mionzi haina madhara ya papo kwa hapo useme utaungua ueke ubandike plasta yaishe, bali madhar yanaweza kuwa madogo madogo na kudhuru hadi vizazi vijavyo.

na sidhani kama hili suala ni gumu kwetu kama nchi sababu standard tayari zipo ni suala tu la kuamua sisi tunatumia ipi na kuanza kuchukua sample za kila aina ya simu inayoingia nchini,
tecno inapatikan India, kampuni mama ya tecno ni TRANSSION HOLDINGS AMBAYO MAKAO MAKUU YAKE YAKO CHINA, LAKIN PIA INAFANYA KAZI FRANCE NA KOREA KUZALISHA SIMU ZAO....KJE INDIA WANAYO HIYO ULIYOITAJA MBONA TECNO ZIPO PIA
 
Tecno wanaweza kuwa orijino uku africa ila material duni wanayotengenezea simu zao na specs za uwongo, hawawezi kupeleka ivyo vituko kwenye soko la ulaya.
 
tecno inapatikan India, kampuni mama ya tecno ni TRANSSION HOLDINGS AMBAYO MAKAO MAKUU YAKE YAKO CHINA, LAKIN PIA INAFANYA KAZI FRANCE NA KOREA KUZALISHA SIMU ZAO....KJE INDIA WANAYO HIYO ULIYOITAJA MBONA TECNO ZIPO PIA
mkuu tusidanganyane hao ma giant hawana uwezo wa kuzalisha ufaransa na korea sembuse Tecno? unajua mishahara hizo nchi mbili wanavyolipa? unajua square metre moja ya ardhi ni shilingi ngapi? samsung mwenyewe ambaye korea ni kwao hakumtoshelezi gharama ni kubwa sana amehamishia mitambo china na vietnam. unaweza tupa link ya location za hivyo viwanda?

pia sijawahi sikia Tecno zikiuzwa india unaweza nipa source?
 
Ni nchi gani ya Ulaya inayotumia Tecno? Hata nchi za Asia nna mashaka labda huko China. Kampuni ya Tecno imelenga soko la Afrika tu. Inawezekana zisifungiwe lakini hata kama zitaendelea kutumika bado ukweli uko palepale kwamba simu za Tecno hazina kiwango na ni hitari kwa afya yako.
Tecno hata wakenya wanatengeneza,Nigeria ndio usiseme kabisa
 
Nenda kwenye setting,then check backup & reset click it utaona factory data reset baada ya hapo ukibonyeza itakuuliza unataka kureset na memory yote kwenye phone will be deleted ,say yes and it will reset
mzee tatizo lilopo ni privacy password ambayo imesahaulika...so nataka design kama kuiflash
 
Back
Top Bottom