PostGE2025 TEC: Maandamano yaliyotokea nchini chanzo ni ukosefu wa demokrasia ya kweli na usalama, wasiojulikana, utekaji pamoja na kupotea na kuumizwa kwa watu

PostGE2025 TEC: Maandamano yaliyotokea nchini chanzo ni ukosefu wa demokrasia ya kweli na usalama, wasiojulikana, utekaji pamoja na kupotea na kuumizwa kwa watu

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Heparin

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2021
Posts
440
Reaction score
3,211
Baraza la Maaskofu la Kanisa Katoliki Tanzania (TEC) limesema Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 imeliingiza Taifa katika hali ya maandamano yaliyozaa vifo, watu kujeruhiwa, kupotea na uharibifu wa mali, hali ambayo imepelekea Taifa kuwa kwenye masononeko, na maumivu kwani wapo walioawa na kuumizwa wakiwa nyumbani kwao bila kuhusika kwenye maandamano hayo

Rais wa TEC Askofu Wolfgang Pisa ameeleza hayo wakati akisoma tafakuri ya pamoja ya Maaskofu wa Kanisa hilo, kufuatia tafakari na sala walizofanya kwa takribani siku nne (4) kuanzia Novemba 11 hadi 14 mwaka huu, ambapo Maaskofu hao wametumia siku hizo kuiombea nchi amani kufuatia mapito magumu inayopitia nchi kwa sasa, kutokana na kile walochokitaja kuwa 'maumivu' waliyonayo Watanzania

Sambamba na kulaani matukio hayo, TEC imesema Taifa limejeruhiwa na kupoteza heshima yake kimataifa ambapo mataifa, hivyo kutumia nafasi hiyo kutoa rai kwa mamlaka husika hususani Vyombo vya Ulinzi na Usalama na Serikali kwa ujumla kuchukua hatua za haraka za kuliponya Taifa

Wametaka kufanyika uchunguzi utakaoshirikisha wadau wa ndani na nje ya nchi, na kwamba wachunguzi wawe kutoka kwenye vyombo visivyofungamana na upande wowote ikiwemo Taasisi za Dini, Taasisi za Kimataifa huru nk, huku wakitoa wito kwa viongozi wa umma kuishi maisha ya uadilifu na uwajibikaji kwa viongozi

TEC pia imetaka wote waliokamatwa kwa hila kabla, wakati na baada ya uchaguzi waachiwe huru bila masharti yoyote

Aidha, katika maelezo yake, Askofu Pisa amesema tathmini inaonesha kuwa maandamano yaliyotokea nchini yametokana ukosefu wa usalama nchini hasa uwepo wa matukio ya utakaji, kupotea na kuumizwa kwa watu, uwepo wa watu wasiojulikana ambao wamedai kuwa wanaonekana kuwa na nguvu kuliko vyombo vya Dola nk,

Sababu nyingine ni kukosekana kwa demokrasia ya kweli, hasa kilio cha muda mrefu tangu mwaka 2016, kilio ambacho hakijapatikana suluhisho la kweli

Pia, imeelezwa kuwa wananchi wamekosa eneo la kufikisha malalamiko yao pale haki zao zinapokiukwa nk.

Kwa muktadha huo, TEC imeshauri mamlaka husika kuhakikisha inaliponya Taifa na kuhakikisha mchakato wa Katiba Mpya unaanza haraka iwezekanavyo, huku Watanzania kwa ujumla wake wakipewa wito wa kuendelea kusali na kuliweka Taifa kwenye hali ya uponyaji.

1000508734.jpg
 
Kuna ukosefu wa usalama nchi hii,na Somalia kuna nini?..wao mbona hawakutekwa?
Unalipwa Tsh ngapi, mbona wajitafutia laana tu, unatukana viongozi wako wa Kiroho kwa tsh 5000 au ndo raisi wenu na ccm yako inawaelekeza hivo, chama kimekosa nidhamu kabisa, vijana wa chama wamekua machawa na makatili kuliko Hilter, ujui kwamba rais wako kateka moaka mapadre.
 
Unalipwa Tsh ngapi, mbona wajitafutia laana tu, unatukana viongozi wako wa Kiroho kwa tsh 5000 au ndo raisi wenu na ccm yako inawaelekeza hivo, chama kimekosa nidhamu kabisa, vijana wa chama wamekua machawa na makatili kuliko Hilter, ujui kwamba rais wako kateka moaka mapadre.
Sina kiongozi wa kiroho mimi,na silipwi,napinga unafiki tu wa hao watu,bandari kupewa mwarabu wameumia sana wakati bandari ilikua mikononi mwa ticts kwa miaka 25 hawakusema kitu
 
Safi sanaaaaa

 
Unauliza au unapigia jibu mstari? Mapadri wangapi wametekwa, achia mbali aliyeshambuliwa kwenye makazi ya baraza la maaskofu? Kuingia barabarani pekee ndio kutaleta majibu stahiki.
Padre gani alitekwa!?..wa nyanda za juu kusini alibet mitandaoni madeni yakamzidia akajiteka,wa songea alihonga hawara 39m akaachwa akaenda jificha shambani akila karanga na maji
Hapo TEC waliposhambuliwa hakuna CCTV camera watuoneshe mshambuliaji?
 
Hawa nao ni wanafiki tu hakuna lolote hapa..

-Wakati walikuwa wanachochea upumbavu wao walitegemea matokeo gani?

-hz kamati zitokanazo na makundi ya dini mara taasisi za nje, malengo yake ni nin? Ni wapi waliwahi kuona uchunguzi kama huu? Hzo kamati zitokanazo na taasisi za nje ni kwa mjibu wa katiba ipi au sheria ipi?

msituletee udini hapa, mara uislamu (hii nchi si ya kiislam), mara TEC wamesema (hii si vatican)..mara wakristo (hii nchi si ya ukristo), kwa ujumla nchi hii haina dini,

mm ni mkiristo, lakn nachukia sana matamko ya bakwata. tec, cct, mara ukristo, maana wote wanafiki tu..

iacheni tanzania na mambo yake msipanue mikundu na kamati zenu za bakwata mara tec mara kutoka nje,

SERIKALI INAJUA WAJIBU WAKE, SI LAZIMA IKUMBUSHWE NA HAWA WEZI WA SWADAKA NA SADAKA!
 
Padre gani alitekwa!?..wa nyanda za juu kusini alibet mitandaoni madeni yakamzidia akajiteka,wa songea alihonga hawara 39m akaachwa akaenda jificha shambani akila karanga na maji
Hapo TEC waliposhambuliwa hakuna CCTV camera watuoneshe mshambuliaji?
unadhani sisi ni wa kuokotwa na hizo porojo za polisi wauawaji? Ngoja turudi barabarani kama hamtatajana.
 
Back
Top Bottom