TCRA mmekubali Continental kuendelea kutuumiza?

TCRA mmekubali Continental kuendelea kutuumiza?

mkalimani4

Member
Joined
Nov 30, 2016
Posts
26
Reaction score
29
Napenda kwanza niwape hongera kwa kazi nzuri mnayoifanya hasa ya kuwapa habari wananchi kuhusu haki zao za kupata habari. Nakumbuka mwaka juzi mlitangaza kuwa Channel za ITV, EATV,TBC, CLOUDS n.k zinatakiwa kuonyeshwa bure na King'amuzi cha Continental hata kama mteja hajajiunga na kifurushi chao.
Hivi sasa agizo lenu limewekwa kapuni na sasa wameachia channel tatu tu;- Star tv, Tbc na Tanzania Safari.
Mkuu wa Tcra wachunguze vijana wako inawezekana wamepewa mlungula na kampuni hilo ili wavae miwani ya mbao kwa kutoona jinsi wananchi wanavyonyimwa haki ya kupata habari.
Kama leseni yao walibadilisha ni vyema jamii ikafahamishwa kuliko kuwa na ukimya wa namna hii.
Pia nimebaini hata King'amuzi cha Zuku kinalipisha hata channel ya Tbc kama kifurushi kikiisha na yenyewe inasitishwa.
Natumaini mtafanyia kazi suala hili.
 
Ngoja turudishe hela tulizotolea matangazo ya bure wakati wa kampeni kwanza tukimaliza Tutakusikiliza
 
Hujakosea kabisa, hawa na Ting hawafai kabisa. Hawaoni shida wakati wowote kuwa offline.
 
...
Jukumu la zile TV tano za mwanzo kurushwa bila pingamizi alipewa startimes, hizi nyingine zilijileta baadae. Ting na kingamuzi kingine cha wazawa havijashuritshwa na kadhia hii. Digitek na Continental ni matokeo ya mgawanyiko. Azam nae anaingia kwa kutumia udhaifu huu.
...
 
Kiburi wanakipata kwa Mwakyembe.

Kama maelekezo alikwishayatoa na kuutangazia umma kuwa channels zote za ndani ni bure, bado wanaziuza na hachukui hatua yoyote. Wao hao mumiani wafanye nini?

Magufuli anapowala vichwa mawaziri wazembe kama hawa, tuacheni kupiga kelele za kuwakingia kifua!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom