TCRA mko wapi mpaka hiki kinatokea ?

TCRA mko wapi mpaka hiki kinatokea ?

Mkuu MUUZA NGADA fahamu kwamba hayo makampuni ya simu yanafanya biashara ya kutangaza matangazo ya hayo makampuni ya kamali. Hiyo ni biashara ya matangazo na hizo sms zimeshalipiwa tayari ndiyo maana VODACOM au kampuni yoyote ile ya simu hawawezi kuzizuia. Hii biashara inawaingizia pesa mingi sana ndiyo maana wewe ulipoenda kuwauliza wamekuzungusha tu, lakini wanajua ukweli wote kuwa wao ndiyo waliotoa hizo namba za wateja kwa makubaliano maalumu ya kulipwa.

Kiutaratibu ninavyo fahamu mimi namba ya simu unayoimiliki siyo mali yako, bali ni mali ya SERVICE PROVIDER uliyejiunga naye kama ni VODACOM, AIRTELL, HALLOTELL n.k. hawa ndiyo wamiliki halali wa hizo namba za simu. Literally tunaweza kusema namba za simu ni mali yetu, but technically zinamilikiwa na makampuni ya simu.
Sawa,ila wajaribu siku moja kumpa mtu mwengine namba yangu ya simu ndio tutajua namba ni ya kwao au yangu. Kesi za hivi uwa nazipenda sana.
 
9ad27421b6d51d6d40b75b373565c28e.jpg



ONLY IN TANZANIA
 
Ur very smart broo! Sio wewe tu,nami nakwazika na jumbe km hizo na Nina line3 almost napokea kwenye namba zote! Ni kero kweli!
 
Nachukia sana hii mitangazo..wakati mwingine usiku unasikia mlio wa SMS unaamka kucheki ni matangazo ya kipuuzi.!
Najiuliza ingekuwaje kila mfanyabiashara atangaze bidhaa yake kwa style hii sijui ingekuwaje.!
Maana hata mimi muuza majeneza ningetangaza biashara yangu kama hivyo,
Mtu anakuta SMS kwa simu yake yenye ujumbe
"Jipatie ofa ya majeneza ya kisasa, nunua mawili ujishindie moja la mtoto mdogo."
 
Sportpesa
Tatu Mzuka
MOJA SPESHO
INSTAMOJA

hizi meseji lazima zikatize kwangu kila siku
 
USILAUMU TCRA HAWA WANATUMA TUMA randomly ILI MRADI DIGITS ZIWE KUMI NA IANZE NA 0 NA CODE NAMBA YA KAMPUNI MFANO MIMI NABAHATISHA HII NA BILA KUPEWA 0654308777

Sent using Jamii Forums mobile app
Sidhani

Jumbe zinakuja na Code mfano: Tatu Mzuka, SportPesa, BIKO, Mojabet. Kwa maana hiyo ni mtandao unashughulkia hili suala.

Wewe jaribu kutuma kwenye namba yoyote na Jumbe zifike na Code yenye jina lako
 
Mkuu Mimi nilisha wakomesha sportpesa kwenye ile namba inayosumbua 15888.
Fanya kama unaipiga,,,ikisha kaa kwenye call history............then Fanya kama una long-press hiyo namba.
Zitatokea option kadhaa ikiwemo option ya BLOCK

Hapo utaiblock jumla hutapata usumbufu wa aina yoyote.Fanya hivyo kwa namba yoyote inayokusumbua.View attachment VID-20190118-WA0013(0).mp4

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom