TCRA mko wapi mpaka hiki kinatokea ?

TCRA mko wapi mpaka hiki kinatokea ?

MUUZA NGADA

JF-Expert Member
Joined
Jan 21, 2018
Posts
340
Reaction score
497
Tangu Biashara ya Ubashiri na Bahati nasibu kwa njia ya mtandao ianze, sasa hivi imekua kero Hapa nchini hasa kwa watu ambao, hawapo "Interested " na Huduma Hizo!!

Labda utakuwa bado hujaelewa namaanisha nn?? Au nataka kuujuza nini umma na Kupitia Kichwa cha Habari TCRA Inahusikaje ?

Makampuni ya Kamali kama Sportpesa, Moja bet, BIKO, Tatu mzuka na mengineyo, BAADHI huwatumia watu Jumbe mbalimbali kuhusu huduma zao HATA KAMA hujajiunga Na huduma Zao, tena BURE!!!

Point Yangu Inaanzia Hapa!! Sawa kwamba Hizo jumbe zinakuja kwangu BURE na SILAZIMISHWI KUJIUNGA!! Lakini hapa kuna Maswali kadhaa Najiuliza Na Nataka Sasa TCRA pia Mjiulize

i) Haya Makampuni Yanapewa na Nani Namba Yangu mpaka Wakaweza Kumudu Kunitumia Ujumbe??

ii) Iwapo Mitandao Ya Simu Wana "Details " zote khusu mimi, Kwa Misingi ipi mpaka wanawapa, Makampuni ya Kamali namba yangu ya Simu bila Ridhaa Yangu??

"ATLEAST " Wangetoa hizo taarifa zangu kwenye Chombo cha Dola Wala Nisingepata SHAUKU ya Kuhoji Lakini Siyo kwa Kampuni ya Kamali

Hizi jumbe ni kero tena kero kwa watu ambao hawapo "Interested" na Kamali & Bahati Nasibu kwa Ujumla HATA KAMA JUMBE ZINAKUJA BURE " Moja kwa moja Inakua Usumbufu , Jaribu Kufikilia Kwa Kina Yafuatayo

i) Sms hizo zinapowafikia VIONGOZI WETU WA DINI Unazani Wanafurahishwa nazo? Mtu ambaye ameshikamana na Dini unazani anakuwa kwenye hali gani pale ambapo Sms imeingia, Anaacha Shughuli zake Kisha Anafungua anakuta Sms Hizo??

ii) Kama hiyo haitoshi, Jaribu kuvuta picha kwamba una matatizo, Kuna mgonjwa amelazwa Hospitali, au Watoto wamefukuzwa shule kisa Ada, au Umefukuzwa kazi na Upo kwenye Msongo wa Mawazo na Znaingia sms kama hizo halafu HUPENDI Huduma hizo ? (Najua kama ni mtu wa Kutokuwa na fikra pevu Utajibu majibu ya ajabu ajabu kupitia statement hii)

Mimi ni Mhanga wa Huduma hizi na Kiukweli SIZIPEDI, Mm ni mtumiaji wa mtandao wa Vodacom Tanzania, na Kila Siku lazima Nitumiwe Sms na Sportpesa!!!


79647870fcfce06500919d94efd2e08a.jpg



Nilichokifanya Nikapiga Hudum kwa wateja, ambapo kwa Maelezo yao Wanadai Nimetumiwa sms kupitia System!! Sasa nikashangaa hiyo System Sportpesa wameitoa Sayari gani wakati wao wanajihusisha na kamali? Namba yangu wameitoa wapi kama siyo Vodacom? Au system za Mitandao ya Simu na Biashara ya Kamali Zinafanana? Au Kuna Interest Vodacom wanapata Kupitia Huduma za Kampuni Hizi na Ndyo maana Wakawapa Namba zangu?

Katika Najibizano na Watoa huduma, Mwisho wakasema Niende Voda shop na nitaweza Kusaidiwa!!
Kitu cha Ajabu nafika Voda shop pale Samora, naambiw a Wao Hawawezi ila NIWAPIGIE Sportpesa waweze Kuzuia Sms zao kuja kwangu!!!

Kitu Kinachonishangaza hapa ni Kwamba

i) Namba ya Sportpesa nikipiga nakatwa hela, "Upuuzi" wao wanatuma kwangu "Free of Charge " !!!!

ii) Kama hiyo haitoshi Iweje mimi Nipoteze muda wangu na Fedha zangu Kuwapigia?


Hapa Sasa Ndipo TCRA Nawaamsha Kutoka Usingizi Na Mlifanyie Kazi Hili Ili Kutusaidia Sisi Wavuja Jasho na Walala hoi

~MUUZA NGADA~
 
Unajua hapa Tanzania makampuni yanacheza sana kwa sababu wanajua wananchi hawaendi mahakamani... Ila hakuna kitu wanachoogopa makampuni kama kesi kwa sababu inaharibu image ya kampuni
 
mtoa mada upo sahihi kabisa ...hawajamaa wanakera mnooo..TCRA wanapaswa kulitolea macho hili
 
Hao moja bet wananikera hakuna mfano.......... Hadi Saa saba usiku wanakutumia huo ujinga wao, ukiamkaa tu asubuhi unakutana na upuuzi wao tena.

Bora wangekuwa wakikutumia hizo SMS wanaweka na namna ya kujitoa ili usiwe unatumiwa huu UJINGA.

TCRA waamke sasa tumechoshwa na huu upuuzi.
 
e8a3e5845a48030f4f72c997d4a69997.jpg

Kuna hawa wapuuzia wanakera sana unakuta unasubiri msg ya pesa af inaingia msg kama hii.ni ujinga sana
Ofcourse Inakera Sana, Kwasababu Hawajazitoa Namba Zako Mbinguni!!! Kampuni Husika Ndyo Imetoa!! Swali la Msingi ni KWANINI WATOE?
 
Unajua hapa Tanzania makampuni yanacheza sana kwa sababu wanajua wananchi hawaendi mahakamani... Ila hakuna kitu wanachoogopa makampuni kama kesi kwa sababu inaharibu image ya kampuni
Mkuu, sheria inasemaje kuhusu hili ? Ikiwezekana niiweke bondi 4×4 yangu ili niendeshe kesi
 
Jamaa wanakera sana hao yaani kutwa nzima SMS ni zao tu ndo zinapishana kwenye simu tena kama namba za voda ndo wamezidi bora hata na airtel kidogo.
 
Back
Top Bottom