TCRA CCC Mkowapi Tunaibiwa Bando za Internet?

TCRA CCC Mkowapi Tunaibiwa Bando za Internet?

Siku zenyewe ndio hizi boss... mie hili ndio bundle langu la mwisho kutumia, baada ya hapa simu itakaa tu ndani, mwenye shida anioigie ... nimejikuta kwa wiki natumia zaidi ya 20,000... kuja kushtuka nikajionea huruma kabisaa

Kama huna kazi inayo itaji internet au kazi ya kupiga simu kwa wingi.. unaweka simu yako ndani ..unakuwa zako weekend unaweka bundle then unasoma yote ya mtandaoni na kupigia ndugu zako wa karibu
 
Halotel wana ile 1GB kwa 1000 wiki kwenye Halopesa lakini kinaisha siku 3 tu. Halotel nimeshaiogopa. Ni wezi balaa
Sio hivyo tu,hata ukishalinunua hilo bando lako utagundua mtandao una shuka speed,kitu cha kudownload dakika 3 unatumia dakika 10...
 
ndio voda hao wanatufanya wa tz chuma ulete......
Sio voda na tigo wapo hivyo hivyo.
Mfano tigo wanahuduma ya niwezeshe unaweza kopa dakika, mb au salio. Walivyo wajinga ukikopa salio badala wakupe salio lenyewe wanakupangia dakika, sms na mb. Mb zenyewe ni 40 hapo umekopa salio la 1500. Na bado utatakiwa kulipa na riba juu.
 
Hii kweli pasua kichwa, hasa hawa wa kuitwa Voda...Mie nimeamua utaratibu wangu mwenyewe, badala ya kununua kifurushi natumia salio la kawaida kuperuzi, maana kwa sasa sioni tofauti kati ya kifurushi na salio la kawaida.
 
Back
Top Bottom