mankachara
JF-Expert Member
- Sep 27, 2013
- 6,161
- 3,495
Ndani ya timu ya taifa wamo ukawa ndio maana hawaoneshi
Ukweli mkuu inasikitisha mno lakini nadhani mazowea ya watangazaji kusema uongo kwenye radio ndio kunakofanya washindwe kutumia TV wakati ni chombo cha umma.Tanzania kwa nini timu ya taifa inapocheza iwe ni mechi za kimashindano au kirafiki televisheni yetu ya taifa isionyeshe mechi live tofauti na nchi nyingi za afrika timu ya taifa ikicheza utaona tv ya taifa husika inaonyesha kama bafana wakicheza utaona sabc inaonyesha hata kama supersport wanaonyesha au tv yetu hawana uwezo
Moja kati ya mambo yenye gharama kubwa kwenye utangazaji TV ni kuonyesha tukio moja kwa moja (live). Ndio maana hata kwenye mechi za kimataifa zionyeshwazo moja kwa moja, wakati wa mapumziko huwa hakuonyweshi kinachotokea uwanjani. Ndio maana vituo vingi vya TV hasa kwa nchi zinazoendelea hushindwa kununua haki za kurusha matangazo ya aina hiyo.Kwa hivyo tukio lolote la moja kwa moja mara nyingi hutegemea wadhamini kufidia gharama hizo. Udhamini nao hutegemea mvuto wa tukio linalotaka kuonyeshwa. Kama meachi za Stars hazina mvuto,TBC watalazimika kubeba matangazo hayo wao wenyewe. Inaweza kuwa ni sehemu ya wajibu wao kwa jamii kama Shirika (corporate social responsibility). Lakini umma ukizowea hivyo, TBC watalazimika kugharimika kwenye kila mechi ya Stars. Wema hautakiwi kuzidi uwezo.
TBC hii imechujuka kupita kiasi. Hivi ilikuwaje Tido Mhando akaondolewa? Yule binadamu alikuwa tayari ameshaibadilisha TBC kuwa ya kitaifa na kimataifa badala ya kuwa kituo kama cha serikali ya mtaa !!!!!!!!!
Tunataka Mhando arudishwe TBC.