farajakwangu
JF-Expert Member
- Jun 13, 2015
- 1,942
- 701
We ukiona simba kakamatwa sharubu alaumiwe nani ???Kaka Petro , Msome Jabiri Makame👇
ZANZIBAR: JE INAWEZEKANAJE KURA ZA RAIS WA ZANZIBAR NA WAWAKILISHI ZIWE BATILI NA ZILE ZA RAIS WA JMT NA WABUNGE ZIWE HALALI?
Jabiri Omari Makame
Katika uchaguzi wa Zanzibar, utaratibu ni kwamba Watanzania Zanzibar wanapiga kura 5, yaani Rais wa Zanz, Mwakilishi na diwani. Pia wanapiga kura ya Rais wa JMT na Mbunge.
Kwenye kituo cha kupigia kura kuna meza 2. Moja ni ya tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC) na nyingine ni ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Meza ya NEC ina watumishi wake na Meza ya ZEC ina watumishi wake.
Watumishi wa NEC wanaripoti moja kwa moja kwa NEC na watumishi wa ZEC wanaripoti moja kwa moja kwa ZEC,
Meza ya ZEC inashughulikia uchaguzi wa Rais wa Zanz, Mwakilishi na Diwani na Meza ya NEC inashughulikia uchaguzi wa Rais wa JMT na Mbunge,
ZEC wanaongozwa na katiba ya Zanzibar ya 1984 na NEC wanaongozwa na Katiba ya Tanzania ya 1977,
Pia vyama vya siasa wanaweka mawakala wa aina mbili, moja kwenye meza ya NEC na pili kwenye meza ya ZEC,
Hata katika kuhesabu kura hawa watu hawaingiliani, ZEC na mawakala wao wanahesabu kura zao na NEC na mawakala wao wanahesabu kura zao.
Pia kuna ballot boxes tofauti. Zipo za ZEC kwa ajili ya Kura ya Rais wa Zanzibar, Mwakilishi na Diwani na NEC kwa ajili ya Kura ya Rais wa JMT na Mbunge,
Mzanzibari anapokwenda kupiga kura kwanza anakwenda kwenye meza ya ZEC, anatoa kitambulisho na anapewa kura tatu, Rais wa Zanz, Mwakilishi na Diwani. Anapiga kura na anapakwa wino kidole kimoja.
Baada ya hapo anakwenda kwenye Meza ya NEC anapewa kura 2, Rais wa JMT na Mbunge. Anapiga kura na kuzitumbukiza kwenye masanduku ya NEC ambayo ni tofauti na yale ya ZEC. Anapakwa wino kidole cha pili.
Wakati wa kuhesabau hawa watu hawaingiliani, wasimamizi wa ZEC na Mawakala wa vyama vya siasa wanaosimamia Rais wa Zanzibar, Mwakilishi na Diwani wanakuwa sehemu yao na wasimamizi wa NEC na Mawakala wa vyama vya siasa wanaosimamia kura ya Rais wa JMT na Mbunge wanakuwa sehemu yao,
Kwa hiyo, hapo kuna michakato 2 tofauti hivyo kasoro zilizojitokeza katika kura za ZEC, hasa kuongezeka kwa idadi ya wapiga kura tofauti na wale waliojiandikisha bila kuathili kura za NEC ni kutokana na KUTOINGILINA katika MCHAKATO na majukumu yao.
Udanganyifu umefanyika kwenye meza ya ZEC ndiyo maana walibaini hizo kasoro walipokuwa wanahakiki lakini kwenye meza ya NEC hapakuwa na udanganyifu wowote ndiyo maana hapakuwa na kasoro zozote zilizobainika.
SWALI; Anayepiga kura ZEC, ndiyo yule anayepiga kura NEC. Kwa nini idadi iongezeke ZEC halagu NEC idadi ya wapiga kura isiongezeke?.
Jibu ni kwamba, siyo lazima udanganyifu ufanyike kwa kuongezeka kwa idadi ya wapiga kura, la hasha! Kuna uwezekano wapiga kura ni walewale waliopiga Kura ZEC, wakapiga Kura NEC kwa idadi ileile bila kuzidi idadi ya waliojiandikisha kwenye daftari. Baadhi yao wakaingia na kura fake na wakafanikiwa kupiga kura zaid ya moja kwa upande wa viongozi wa Zanzibar lakini wanapokwenda meza ya NEC wasifanye huo udanganyifu.
Pili Watumishi wa ZEC wanaweza kutoa ballot paper zaidi ya moja kwa mpiga kura kwa lengo la kufanya udanganyifu kwa lengo la kupendelea wagombea wa chama fulani (Rejea kauli ya Mwenyekiti wa ZEC Ndugu JECHA ya kwamba ndani ya tume kuna watumishi wanasukumwa na matakwa ya kisiasa) na watumishi wa NEC wasifanye huo idanganyifu,
Tatu udanganyifu unaweza kufanyika wakati wa kuhesabu kura na kwa upande wa ZEC wakaongeza idadi ya kura lakini upande wa NEC wasifanye hivyo.
KWA HIYO, kutokana na hayo, ni dhahiri kwamba KASORO ZILIZOJITOKEZA KWENYE MATOKEO YA UCHAGUZI WA ZEC HAZIJAATHIRI MATOKEO YA KURA ZA NEC.
Hoja za Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ni za msingi na hoja za Mwenyekiti wa tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ni za msingi, hazipaswi kupuuzwa kwa mustakabali wa taifa letu.
#Amani ni Tunda adimu-Tulikumbatie.
Last edited by a moderator: