Tazama uhusiano wa NEC na ZEC

Tazama uhusiano wa NEC na ZEC

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2012
Posts
10,346
Reaction score
26,138
Salamu zenu wadau!

Leo nawadokeza mambo mawili makubwa ambayo yanawahusisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi-NEC na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar- ZEC. Mambo haya mawili ndiyo hasa yanayoonyesha uhusiano uliopo kati ya NEC na ZEC.

Mosi, ZEC ni mawakala wa NEC kusimamia uchaguzi wa ngazi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Zanzibar. ZEC hukaimishwa na kukasimishwa mamlaka yote ya NEC kule Zanzibar wakati wa uchaguzi wa Rais na Wabunge wa JMT. ZEC hufanya kazi za NEC Zanzibar.

Pili, kulingana na Ibara ya 66 ya Katiba ya Tanzania ya sasa,wabunge watano wa Bunge la JMT huchaguliwa na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kutoka miongoni mwa Wawakilishi wote. Ndiyo kusema,BWZ lina haki ya kuwa na Wabunge/Wawakilishi watano kwenye Bunge la JMT.

Uchaguzi wa Wawakilishi kule Zanzibar husimamiwa na ZEC. Na hata Wabunge wa Bunge la JMT kutoka majimbo ya Zanzibar husimamiwa na ZEC kama mawakala wa NEC. Kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar-wa Wawakilishi ni kutokuwepo kwa Baraza la Wawakilishi na kutokuwepo kwa Wabunge watano wanaotokana na Baraza hilo.

Bunge halitakamilika bila Wabunge toka Baraza la Wawakilishi la Zanzibar. Wabunge wa Tanzania Bara wametokana na uratibu wa NEC. ZEC nao husababisha kupatikana kwa Wabunge kama nilivyoeleza hapo juu.

Hivyobasi, NEC na ZEC zinahusiana vya kutosha. Nasema tena na tena,kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar kuna athari kwa Tanzania nzima.
 
Logically huhitaji kuumiza akili .... Uchaguzi umevurugwa mwanzo mwisho ...
 
Kutwawala kimabu ndo kunasabisha kupindisha sheria, kungekuwa na serikali tatu tusingekuwa na noma namshukuru mungu kwa kuwajibu ukawa
 
Si kweli..NEC wanatumia facilities za ZEC kupunguza gharama. Hata uchaguzi wa Jamhuri unatofauti na ule wa Zanzibar.Mfano..kadi ya mpiga kura ya ZEC inatumika tu kwenye uchaguzi wa Zanzibar. Uchaguzi wa Jamhuri unausajili wake tofauti na wa ZEC. Sisi watu wa bara haturuhusiwi kupiga kura Zanzibar kwasababu hatuna kadi za Zec.Ila kama kuna uchaguzi wa Jamhuri tunapiga kura popote ..hata Zanzibar lakini kwa kadi ya Nec.
Na hata wazanzibar wanakadi mbili..ya Zec na Nec.
 
Si kweli..NEC wanatumia facilities za ZEC kupunguza gharama. Hata uchaguzi wa Jamhuri unatofauti na ule wa Zanzibar.Mfano..kadi ya mpiga kura ya ZEC inatumika tu kwenye uchaguzi wa Zanzibar. Uchaguzi wa Jamhuri unausajili wake tofauti na wa ZEC. Sisi watu wa bara haturuhusiwi kupiga kura Zanzibar kwasababu hatuna kadi za Zec.Ila kama kuna uchaguzi wa Jamhuri tunapiga kura popote ..hata Zanzibar lakini kwa kadi ya Nec.
Na hata wazanzibar wanakadi mbili..ya Zec na Nec.

Issue sio kadi hap,issue ni mamlaka inayosimamia uchaguzi bara ni hiyohiyo inayosimamia znz kupitia wakala wake yaani zec.

Pili huwezii kuunda bunge bara bila kuwepo wabunge wa znz.
 
Kwa hiyo yale matokeo ya urais wa TZ bara waliyopiga wazanzibari yametumika au wametatoa kwenye mahesabu?
 
Si mhilpo tu mustakabali mkubwa ni kuwa kama matokeo ZEC imayafuta na nwalisimamia ina maana inafuta ya wale wa mUUNGANO maana kura zilipigwa siku na wakati mmoja!! HILO HALIHITAJI Sungusia ama Palagamanabanda Kabudi kuanisha mbona katiba na sheria zapindwa?
 
Nasikia kura zote uraisi wa JMT kule zanzibar na pemba tume imeamua kumpa Lowassa ili kuondoa ubishi!
 
Si kweli..NEC wanatumia facilities za ZEC kupunguza gharama. Hata uchaguzi wa Jamhuri unatofauti na ule wa Zanzibar.Mfano..kadi ya mpiga kura ya ZEC inatumika tu kwenye uchaguzi wa Zanzibar. Uchaguzi wa Jamhuri unausajili wake tofauti na wa ZEC. Sisi watu wa bara haturuhusiwi kupiga kura Zanzibar kwasababu hatuna kadi za Zec.Ila kama kuna uchaguzi wa Jamhuri tunapiga kura popote ..hata Zanzibar lakini kwa kadi ya Nec.
Na hata wazanzibar wanakadi mbili..ya Zec na Nec.


Nani aliekwambia wazanzibar wanazo kadi mbili za kupigia kura!!?? Kama jambo hulijui ni bora unyamaze kimya kuliko kujifanya unajua mengi

Hakuna mzanzibar hata mmoja ambae yumo katika daftari la wapiga kura la Zanzibar ambae pia yumo katika daftari la wapiga kura wa muungano.

Daftari la wapiga kura la muungano linapokuja Zanzibar linawaandikisha wale wote ambao hawana sifa za kuwemo katika daftari la wapiga kura Zanzibar!!!

Kwa ufupi msimamizi wa uchaguzi wa kuwachagua wabunge na raisi wa muungano kwa upande wa zanzibar ni ZEC!!! Kwa ufupi MZANZIBAR HAIJUI NEC NI MDUDU GANI.
 
Kwa hiyo yale matokeo ya urais wa TZ bara waliyopiga wazanzibari yametumika au wametatoa kwenye mahesabu?


Matokeo ya uraisi wa muungano pamoja na wabunge wake yaliyosimamiwa na ZEC ndio hayo hayo waliyoyatumia kuwatangaza wabunge Wa Zanzibar pamoja na kura za uraisi wa muungano.
 
Salamu zenu wadau!

Leo nawadokeza mambo mawili makubwa ambayo yanawahusisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi-NEC na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar- ZEC. Mambo haya mawili ndiyo hasa yanayoonyesha uhusiano uliopo kati ya NEC na ZEC.

Mosi, ZEC ni mawakala wa NEC kusimamia uchaguzi wa ngazi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Zanzibar. ZEC hukaimishwa na kukasimishwa mamlaka yote ya NEC kule Zanzibar wakati wa uchaguzi wa Rais na Wabunge wa JMT. ZEC hufanya kazi za NEC Zanzibar.

Pili, kulingana na Ibara ya 66 ya Katiba ya Tanzania ya sasa,wabunge watano wa Bunge la JMT huchaguliwa na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kutoka miongoni mwa Wawakilishi wote. Ndiyo kusema,BWZ lina haki ya kuwa na Wabunge/Wawakilishi watano kwenye Bunge la JMT.

Uchaguzi wa Wawakilishi kule Zanzibar husimamiwa na ZEC. Na hata Wabunge wa Bunge la JMT kutoka majimbo ya Zanzibar husimamiwa na ZEC kama mawakala wa NEC. Kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar-wa Wawakilishi ni kutokuwepo kwa Baraza la Wawakilishi na kutokuwepo kwa Wabunge watano wanaotokana na Baraza hilo.

Bunge halitakamilika bila Wabunge toka Baraza la Wawakilishi la Zanzibar. Wabunge wa Tanzania Bara wametokana na uratibu wa NEC. ZEC nao husababisha kupatikana kwa Wabunge kama nilivyoeleza hapo juu.

Hivyobasi, NEC na ZEC zinahusiana vya kutosha. Nasema tena na tena,kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar kuna athari kwa Tanzania nzima.


ZEC wanatumia sheria ya 1984. NEC wanatumia sheria ya 1987. Hivyo ni vyombo viwili tofauti.
 
Si kweli..NEC wanatumia facilities za ZEC kupunguza gharama. Hata uchaguzi wa Jamhuri unatofauti na ule wa Zanzibar.Mfano..kadi ya mpiga kura ya ZEC inatumika tu kwenye uchaguzi wa Zanzibar. Uchaguzi wa Jamhuri unausajili wake tofauti na wa ZEC. Sisi watu wa bara haturuhusiwi kupiga kura Zanzibar kwasababu hatuna kadi za Zec.Ila kama kuna uchaguzi wa Jamhuri tunapiga kura popote ..hata Zanzibar lakini kwa kadi ya Nec.
Na hata wazanzibar wanakadi mbili..ya Zec na Nec.

acha kupotosha ndugu yake mzanzibar ana kadi moja tu ya Zec na ndio anayoitumia kupiga kura ya Zanzibar na Tanzania
 
Salamu zenu wadau!

Leo nawadokeza mambo mawili makubwa ambayo yanawahusisha Tume ya Taifa ya Uchaguzi-NEC na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar- ZEC. Mambo haya mawili ndiyo hasa yanayoonyesha uhusiano uliopo kati ya NEC na ZEC.

Mosi, ZEC ni mawakala wa NEC kusimamia uchaguzi wa ngazi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa upande wa Zanzibar. ZEC hukaimishwa na kukasimishwa mamlaka yote ya NEC kule Zanzibar wakati wa uchaguzi wa Rais na Wabunge wa JMT. ZEC hufanya kazi za NEC Zanzibar.

Pili, kulingana na Ibara ya 66 ya Katiba ya Tanzania ya sasa,wabunge watano wa Bunge la JMT huchaguliwa na Baraza la Wawakilishi la Zanzibar kutoka miongoni mwa Wawakilishi wote. Ndiyo kusema,BWZ lina haki ya kuwa na Wabunge/Wawakilishi watano kwenye Bunge la JMT.

Uchaguzi wa Wawakilishi kule Zanzibar husimamiwa na ZEC. Na hata Wabunge wa Bunge la JMT kutoka majimbo ya Zanzibar husimamiwa na ZEC kama mawakala wa NEC. Kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar-wa Wawakilishi ni kutokuwepo kwa Baraza la Wawakilishi na kutokuwepo kwa Wabunge watano wanaotokana na Baraza hilo.

Bunge halitakamilika bila Wabunge toka Baraza la Wawakilishi la Zanzibar. Wabunge wa Tanzania Bara wametokana na uratibu wa NEC. ZEC nao husababisha kupatikana kwa Wabunge kama nilivyoeleza hapo juu.

Hivyobasi, NEC na ZEC zinahusiana vya kutosha. Nasema tena na tena,kufutwa kwa uchaguzi wa Zanzibar kuna athari kwa Tanzania nzima.

Wewe Mselemwa acha ushabiki mkuu. Hao wabunge watano wanaochaguliwa toka baraza la wawakilishi watachaguliwa baada ya uchaguzi halali kufanyika. Na hii sio sababu ya kuiunganisha NEC na ZEC bali inaunganisha baraza la wawakilishi na Bunge la Jamhuri ya Muungano. Upotoshaji haukufikishi popote.
 
ZEC wanatumia sheria ya 1984. NEC wanatumia sheria ya 1987. Hivyo ni vyombo viwili tofauti.
Hujapata kina cha maelezo. Kuwa na sheria mbili hakuzuii hoja iliyotolewa. Je ZEC ya sheria ya 1984 haifanyi kazi za NEC ya sheria ya 1987? Zanzibar hakuna NEC bali majukumu yake yanafanywa na ZEC - na hii ni kwa mujibu wa sheria hizo mbili. Udhaifu wa ZEC katika kusimamia na kutekeleza majukumu hayo na kwa wakati mmoja haiwezi kuathiri kipande kimoja tu kikakiacha kingine!
 
Kaka Petro , Msome Jabiri Makame👇

ZANZIBAR: JE INAWEZEKANAJE KURA ZA RAIS WA ZANZIBAR NA WAWAKILISHI ZIWE BATILI NA ZILE ZA RAIS WA JMT NA WABUNGE ZIWE HALALI?

Jabiri Omari Makame

Katika uchaguzi wa Zanzibar, utaratibu ni kwamba Watanzania Zanzibar wanapiga kura 5, yaani Rais wa Zanz, Mwakilishi na diwani. Pia wanapiga kura ya Rais wa JMT na Mbunge.

Kwenye kituo cha kupigia kura kuna meza 2. Moja ni ya tume ya uchaguzi Zanzibar (ZEC) na nyingine ni ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Meza ya NEC ina watumishi wake na Meza ya ZEC ina watumishi wake.

Watumishi wa NEC wanaripoti moja kwa moja kwa NEC na watumishi wa ZEC wanaripoti moja kwa moja kwa ZEC,

Meza ya ZEC inashughulikia uchaguzi wa Rais wa Zanz, Mwakilishi na Diwani na Meza ya NEC inashughulikia uchaguzi wa Rais wa JMT na Mbunge,

ZEC wanaongozwa na katiba ya Zanzibar ya 1984 na NEC wanaongozwa na Katiba ya Tanzania ya 1977,

Pia vyama vya siasa wanaweka mawakala wa aina mbili, moja kwenye meza ya NEC na pili kwenye meza ya ZEC,

Hata katika kuhesabu kura hawa watu hawaingiliani, ZEC na mawakala wao wanahesabu kura zao na NEC na mawakala wao wanahesabu kura zao.

Pia kuna ballot boxes tofauti. Zipo za ZEC kwa ajili ya Kura ya Rais wa Zanzibar, Mwakilishi na Diwani na NEC kwa ajili ya Kura ya Rais wa JMT na Mbunge,

Mzanzibari anapokwenda kupiga kura kwanza anakwenda kwenye meza ya ZEC, anatoa kitambulisho na anapewa kura tatu, Rais wa Zanz, Mwakilishi na Diwani. Anapiga kura na anapakwa wino kidole kimoja.

Baada ya hapo anakwenda kwenye Meza ya NEC anapewa kura 2, Rais wa JMT na Mbunge. Anapiga kura na kuzitumbukiza kwenye masanduku ya NEC ambayo ni tofauti na yale ya ZEC. Anapakwa wino kidole cha pili.

Wakati wa kuhesabau hawa watu hawaingiliani, wasimamizi wa ZEC na Mawakala wa vyama vya siasa wanaosimamia Rais wa Zanzibar, Mwakilishi na Diwani wanakuwa sehemu yao na wasimamizi wa NEC na Mawakala wa vyama vya siasa wanaosimamia kura ya Rais wa JMT na Mbunge wanakuwa sehemu yao,

Kwa hiyo, hapo kuna michakato 2 tofauti hivyo kasoro zilizojitokeza katika kura za ZEC, hasa kuongezeka kwa idadi ya wapiga kura tofauti na wale waliojiandikisha bila kuathili kura za NEC ni kutokana na KUTOINGILINA katika MCHAKATO na majukumu yao.

Udanganyifu umefanyika kwenye meza ya ZEC ndiyo maana walibaini hizo kasoro walipokuwa wanahakiki lakini kwenye meza ya NEC hapakuwa na udanganyifu wowote ndiyo maana hapakuwa na kasoro zozote zilizobainika.

SWALI; Anayepiga kura ZEC, ndiyo yule anayepiga kura NEC. Kwa nini idadi iongezeke ZEC halagu NEC idadi ya wapiga kura isiongezeke?.

Jibu ni kwamba, siyo lazima udanganyifu ufanyike kwa kuongezeka kwa idadi ya wapiga kura, la hasha! Kuna uwezekano wapiga kura ni walewale waliopiga Kura ZEC, wakapiga Kura NEC kwa idadi ileile bila kuzidi idadi ya waliojiandikisha kwenye daftari. Baadhi yao wakaingia na kura fake na wakafanikiwa kupiga kura zaid ya moja kwa upande wa viongozi wa Zanzibar lakini wanapokwenda meza ya NEC wasifanye huo udanganyifu.

Pili Watumishi wa ZEC wanaweza kutoa ballot paper zaidi ya moja kwa mpiga kura kwa lengo la kufanya udanganyifu kwa lengo la kupendelea wagombea wa chama fulani (Rejea kauli ya Mwenyekiti wa ZEC Ndugu JECHA ya kwamba ndani ya tume kuna watumishi wanasukumwa na matakwa ya kisiasa) na watumishi wa NEC wasifanye huo idanganyifu,

Tatu udanganyifu unaweza kufanyika wakati wa kuhesabu kura na kwa upande wa ZEC wakaongeza idadi ya kura lakini upande wa NEC wasifanye hivyo.

KWA HIYO, kutokana na hayo, ni dhahiri kwamba KASORO ZILIZOJITOKEZA KWENYE MATOKEO YA UCHAGUZI WA ZEC HAZIJAATHIRI MATOKEO YA KURA ZA NEC.

Hoja za Mwenyekiti wa tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) ni za msingi na hoja za Mwenyekiti wa tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ni za msingi, hazipaswi kupuuzwa kwa mustakabali wa taifa letu.

#Amani ni Tunda adimu-Tulikumbatie.
 
Last edited by a moderator:
Issue sio kadi hap,issue ni mamlaka inayosimamia uchaguzi bara ni hiyohiyo inayosimamia znz kupitia wakala wake yaani zec.

Pili huwezii kuunda bunge bara bila kuwepo wabunge wa znz.

Hii tamu sana, bunge linaanza lini jaman?
 
Back
Top Bottom