Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 16,095
- 24,323
Katika siku za hivi karibuni kumekuwa na tabia inayolalamikiwa sana na madereva wa usafiri wa mtandao (Bolt, Farasi, Paisha n.k.) katika eneo la Kivukoni Ferry, Dar es Salaam.
Baadhi ya madereva wa bodaboda wanaopaki karibu na Pantoni wamekuwa wakifanya kitendo cha kuchomoa funguo za bodaboda, au gari la dereva wa Bolt anapofika kuchukua abiria aliyeshuka kwenye pantoni, kisha wanampa askari ambaye askari huchua fedha ambazo hazijulikani ni kiasi gani kwakuwa hakuna control number wanayopewa ili kulipa fedha hiyo.
Ni muhimu kukumbusha jambo moja la msingi: hakuna sheria inayomkataza dereva wa Bolt au usafiri wa mtandao kumchukua abiria wake katika eneo la ferry, iwapo dereva huyo hafanyi kosa la barabarani. Vilevile, hakuna kibao cha barabarani kinachokataza magari ya aina hiyo kufika katika eneo hilo kwa ajili ya kupakia au kushusha abiria.
Kitendo cha mtu kuchomoa funguo za gari la mtu mwingine bila mamlaka ya kisheria kinaweza kuchukuliwa kama uvunjifu wa utulivu na kuingilia mali ya mtu, jambo ambalo si sahihi katika jamii inayoheshimu sheria.
Ni lazima tukubali kwamba dunia imebadilika. Leo hii teknolojia imeleta mifumo mipya ya usafiri kama Bolt, Uber na mingineyo ambayo inawawezesha abiria kuagiza usafiri kwa simu zao. Hii ni sehemu ya maendeleo ya uchumi wa kidijitali na haiwezi kuzuiwa kwa nguvu au vitisho.
Badala ya kulinda “vijiwe” vya zamani kwa migogoro, ni busara zaidi kwa vijana na madereva wa bodaboda kukumbatia teknolojia. Leo hii hata bodaboda zinaweza kujiunga kwenye majukwaa ya kidijitali na kupata wateja wengi zaidi bila ugomvi.
Ujumbe ni rahisi:
Baadhi ya madereva wa bodaboda wanaopaki karibu na Pantoni wamekuwa wakifanya kitendo cha kuchomoa funguo za bodaboda, au gari la dereva wa Bolt anapofika kuchukua abiria aliyeshuka kwenye pantoni, kisha wanampa askari ambaye askari huchua fedha ambazo hazijulikani ni kiasi gani kwakuwa hakuna control number wanayopewa ili kulipa fedha hiyo.
Ni muhimu kukumbusha jambo moja la msingi: hakuna sheria inayomkataza dereva wa Bolt au usafiri wa mtandao kumchukua abiria wake katika eneo la ferry, iwapo dereva huyo hafanyi kosa la barabarani. Vilevile, hakuna kibao cha barabarani kinachokataza magari ya aina hiyo kufika katika eneo hilo kwa ajili ya kupakia au kushusha abiria.
Kitendo cha mtu kuchomoa funguo za gari la mtu mwingine bila mamlaka ya kisheria kinaweza kuchukuliwa kama uvunjifu wa utulivu na kuingilia mali ya mtu, jambo ambalo si sahihi katika jamii inayoheshimu sheria.
Ni lazima tukubali kwamba dunia imebadilika. Leo hii teknolojia imeleta mifumo mipya ya usafiri kama Bolt, Uber na mingineyo ambayo inawawezesha abiria kuagiza usafiri kwa simu zao. Hii ni sehemu ya maendeleo ya uchumi wa kidijitali na haiwezi kuzuiwa kwa nguvu au vitisho.
Badala ya kulinda “vijiwe” vya zamani kwa migogoro, ni busara zaidi kwa vijana na madereva wa bodaboda kukumbatia teknolojia. Leo hii hata bodaboda zinaweza kujiunga kwenye majukwaa ya kidijitali na kupata wateja wengi zaidi bila ugomvi.
Ujumbe ni rahisi:
- Tuheshimu sheria.
- Tuheshimu kazi za wengine.
- Tukubali mabadiliko ya teknolojia.