Tatizo la ngozi msaada unahitajika

Tajirimsomi

JF-Expert Member
Jan 12, 2017
4,824
5,563
Habari zenu ndugu zangu !bila kupoteza mda nijikite kwenye mada nimekuwa na tatizo la ngozi yangu kutokurleweka kwa mda mrefu ikiwemo kutokuwa na specific colour Mara mweupe Mara mweusi Mara mabakamabaka japo sio sana na ni baadhi ya maeneo ya mwili.

Sasa hizi siku za karibuni nimekuwa nikiwashwa sana mwili kuanzia mabegani shingo hadi mgongoni ngozi imekauka imetokeza vidude kama vibalango hata nikipaka mafuta haviishi
6b0717f999bff02f8736b0f3c88d979f.jpg
90847adc5d21d6bdc68197dcda1c05f9.jpg
749ffa6d50d22ee4deeacbd89a1edcda.jpg


Sielewi tatizo nini wakuu
Mafuta nayotumiaga ni samona nishajaribu kutumia mafuta tofauti tofauti hata losheni ila naona ngozi yangu haitulii
83f7049a7dac409b57c479a96c7190c3.jpg

Naombeni msaada wakuu hili tatizo ni nini na tiba yake unaweza kuwa nini?
 
fanya mpango umuone daktari bingwa wa ngozi Dermatologist na ukianza matibabu fua nguo zote ulizotumia pamoja na mashuka na mataulo uyapige pasi. Kua mvumilivu matibabu yanaweza kuwa ni ya muda mrefu.
 
fanya mpango umuone daktari bingwa wa ngozi Dermatologist na ukianza matibabu fua nguo zote ulizotumia pamoja na mashuka na mataulo uyapige pasi. Kua mvumilivu matibabu yanaweza kuwa ni ya muda mrefu.
Asante mkuu kwa ushauri japo naogopa sana tiba za hospital
 
Kwa hiyo ulikuja hapa ukitegemea utaalamu wa tiba mbadala?
Vyovyote ila unajua humu kuna watu wana experience na magonjwa kama ayo nipate ushauri walifanyaje mpaka wakapona ila ushauri wako ntauzingatia maana nawashwa mpaka najisikia kama homa nikijimwagia maji ndo balaa
 
Chukua alovera menya ule utando wake wa ndani ponda mpk upate mchuzi ukishaoga usiku paka sehemu zote zilizoathirika kwa muda wa wiki 3 utaniambia
 
Chukua alovera menya ule utando wake wa ndani ponda mpk upate mchuzi ukishaoga usiku paka sehemu zote zilizoathirika kwa muda wa wiki 3 utaniambia
Sawa mkuu ngoja ntaifatfa hiyo aloevera japo nilipo ni adimu kuipata na sijawai kuiona
 
Back
Top Bottom