Cochabamba
Member
- Feb 4, 2014
- 76
- 98
Wizara ya Ujenzi kupitia Waziri wake Dkt.Magufuli wamekagua mzani wa Kisasa kabisa na wa kwanza ktk nchi hii pale Vigwaza Mkoani Pwani. Mzani huo unaruhusu magari kupima bila kusimama, kwa kimombo " Weigh-In-Motion (WIM)".
Utaratibu huu utaondoa kabisa ile dhana yiliyozoeleka ya msongamano wa malori pindi yapimapo uzito. Mzani huu ni mwendelezo wa mizani ya kisasa inayojengwa nchini kote.
Katika safari hiyo Waziri huyo alipita na kukagua barabara ya Kibamba - Kwembe - Makondeko yenye urefu wa kilomita 17. Barabara hii itatoa huduma katika Chuo Kikuu cha Muhimbili kinachojengwa Mloganzila, Kibamba Jijini Dar es Salaam.
Matukio katika Picha:
Mzani mpya wa Vigwaza Mkoani Pwani ambao ni wa kwanza na wakisasa kabisa kujengwa nchini ambao unaruhusu magari kupima bila kusimama na kuondoa ile dhana ya msongamano wa malori ktk mizani.
Mhandisi Kileo kutoka Wakala wa Barabara akionyesha jinsi Mzani mpya wa Vigwaza utakavyokuwa ukipima magari yakiwa yanatembea " Weigh-In-Motion".
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe kushoto akitoa maelezo kuhusu ujenzi wa Mzani huo.
Waziri wa Ujenzi akizungumza na wananchi kuhusu Mzani mpya unaopima magari wakati yakitembea Vigwaza mkoani Pwani.
Ukaguzi wa kazi za ujenzi inayofanyika katika Chuo Kikuu cha Muhimbili kilichopo katika eneo la Mloganzila Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Waziri alipitia akikagua ujenzi wa barabara ya Kibamba kupitia kwembe hadi Makondeko inayojengwa kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Kilometa 17. Aliweza pia kuzungumza na wakazi wa Kwembe.
Katika ziara hiyo aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe (Aliyevaa koti jeusi), picha ya kushoto akizungumza na Meneja wa Wakala wa Barabara mkoa wa Dar es salaam Mhandisi Julius Ndyamukama kuhusu ujenzi wa Barabara yakutoka Kibamba-Kwembe hadi Makondeko yenye urefu wa Kilomita 17
Nawasilisha!
Utaratibu huu utaondoa kabisa ile dhana yiliyozoeleka ya msongamano wa malori pindi yapimapo uzito. Mzani huu ni mwendelezo wa mizani ya kisasa inayojengwa nchini kote.
Katika safari hiyo Waziri huyo alipita na kukagua barabara ya Kibamba - Kwembe - Makondeko yenye urefu wa kilomita 17. Barabara hii itatoa huduma katika Chuo Kikuu cha Muhimbili kinachojengwa Mloganzila, Kibamba Jijini Dar es Salaam.
Matukio katika Picha:
Mzani mpya wa Vigwaza Mkoani Pwani ambao ni wa kwanza na wakisasa kabisa kujengwa nchini ambao unaruhusu magari kupima bila kusimama na kuondoa ile dhana ya msongamano wa malori ktk mizani.
Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe kushoto akitoa maelezo kuhusu ujenzi wa Mzani huo.
Ukaguzi wa kazi za ujenzi inayofanyika katika Chuo Kikuu cha Muhimbili kilichopo katika eneo la Mloganzila Kibamba nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam. Waziri alipitia akikagua ujenzi wa barabara ya Kibamba kupitia kwembe hadi Makondeko inayojengwa kwa kiwango cha lami yenye urefu wa Kilometa 17. Aliweza pia kuzungumza na wakazi wa Kwembe.
Katika ziara hiyo aliambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Mussa Iyombe (Aliyevaa koti jeusi), picha ya kushoto akizungumza na Meneja wa Wakala wa Barabara mkoa wa Dar es salaam Mhandisi Julius Ndyamukama kuhusu ujenzi wa Barabara yakutoka Kibamba-Kwembe hadi Makondeko yenye urefu wa Kilomita 17
Nawasilisha!