Tatizo la msongamano mizani kuisha

Tatizo la msongamano mizani kuisha

Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mizani ya kisasa Vigwaza, mkoani Pwani, Dk Magufuli alisema Ruvu ina eneo kubwa linalotosha kujenga bandari kavu na pia kuna reli ya Tazara inayotoka bandarini, hivyo itakuwa ni jambo jema malori ya mizigo yakiwa yanaanzia safari katika eneo hilo na kuendelea mikoani na nchi za jirani"

Chalinze.

Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli ameshauri kuanzishwa kwa bandari kavu katika Mji wa Ruvu ili kupunguza foleni katika Jiji la Dar es Salaam na kuzuia malori kuingia katikati ya jiji.

Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mizani ya kisasa Vigwaza, mkoani Pwani, Dk Magufuli alisema Ruvu ina eneo kubwa linalotosha kujenga bandari kavu na pia kuna reli ya Tazara inayotoka bandarini, hivyo itakuwa ni jambo jema malori ya mizigo yakiwa yanaanzia safari katika eneo hilo na kuendelea mikoani na nchi za jirani.

"Kulikuwa hakuna sababu ya kuyapeleka malori makubwa mpaka bandarini yakatengeneze foleni Barabara ya Morogoro na Mandela wakati Ruvu ina maeneo makubwa ya kutosha na Reli ya Tazara inapita, hii ni changamoto ya kwetu sote na siyo wizara pekee," alisema Dk Magufuli.

Alisema suala la udhibiti wa foleni jijini Dar es Salaam linahusisha taasisi nyingi za serikali wakiwamo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wizara za Uchukuzi na Ujenzi na Serikali za Mitaa kupitia sheria zake ndogondogo.

Iwapo wazo hilo litakubaliwa, Dk Magufuli alisema watafunga mizani ya Kibaha na kutumia ya Vigwaza.

Mizani ya kisasa ya Vigwaza ni ya kwanza nchini ambayo itakuwa iking'amua magari yaliyozidisha mizigo pekee ili yapimwe na kutozwa faini kwa uvunjifu wa sheria.

Akizungumzia mizani hiyo, Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Mhandisi Mussa Iyombe alisema imegharimu Sh11 bilioni na itasaidia kupunguza foleni za magari ambayo hupitia mizani bila ya kuwa na mizigo au kuzidisha uzito.

Chanzo:Mwananchi

 
Kama ni kwa maana nyingine sawa lakini kama ni kuondoa foleni wala haisaidii,kama serikali ya mkoa imeshindwa kuchonga na kuziwekea lami barabara za vichochoro na zile za mbezi-majumba6,mbezi-mbezi n.k bado foleni itakuwa palepale hata wakijenga flyovers mji mzima
 
sasa MAKONTENA KOTOKA BANDARI MAJI KWENDA BANDARI KAVU YATABEBWA NA NDEGE???
acha kukurupuka soma habari nzima. Unakuwa kama ukawa, haya mzembe wewe ngoja nikunukulie kidogo:

"Akizungumza baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mizani ya kisasa Vigwaza, mkoani Pwani, Dk Magufuli alisema Ruvu ina eneo kubwa linalotosha kujenga bandari kavu na pia kuna reli ya Tazara inayotoka bandarini, hivyo itakuwa ni jambo jema malori ya mizigo yakiwa yanaanzia safari katika eneo hilo na kuendelea mikoani na nchi za jirani"
 
Ni kweli kuwa bandari kavu zikiwa Ruvu zitapunguza foleni kwa kiasi kikubwa but barabara zetu bado zitaendelea kuharibika kwa kuendelea kutumia usafiri wa barabara badala ya reli ambazo zinatakiwa ziboreshwe kwa maana ya miundo mbinu na speed. Reli inatakiwa iwekewe mkakati angalau wa miaka 5 mpaka 10. Itakuwa bora Kuweka bandari kavu Kahama na Mbeya baada ya kuboresha miundo mbinu ya reli.Mbeya ihudumie nchi za Malawi, Zambia na Congo na Kahama ihudumie Burundi, Rwanda na Uganda.
 
Yeye ndiye mwenye jukumu. Sasa anaposhauri anataka nani atekeleze. Yeye ndie kapewa kila kitu. Anashauri anamshauri nani? Huu ndio ubaya wetu. Kila mtu analalamika. Huu ndio mwanzo wa porojo maana uchaguzi umekaribia. Hivi tujiulize suala la barabara za juu. Wazo hilo alilileta siku ya kwanza anaingia wizara hiyo kwa mara ya kwanza. Ni kitu gani kimekekelezwa.?? Nina wasi hata hizi blaa blaa zinazoendelea pale Tazara kama ndio mwanzo wa barabara zenyewe au mwanzo wa kampeini.
 
Nadhani itasaidia kwa kiasi fulani.
Tatizo litajitokeza kama malori hayo ofisi zao nyingi ziko huku mijini na maeneo ya Kurasini.
Serikali imejipangaje juu ya hilo?
 
Kama mezani tu ya vigwaza imegharimu 11bilioni..Mradi mkubwa kama huo wakujenga bandari kavu Ruvu si utafilisi nchi kwa matrlion ya pesa?
Kuliko kujenga mradi huo kwa nini pesa zake zisitumike kwa kuiboresha Reli ya kati ni pamoja na kununua mabehewa mapya ya mizigo ili tutu mie Bandari kavu ya Isaka kwa Mizigo ya Burundi, Ruwanda,Congo na Uganda.
Mm naamini hatutaweza kuondoa misongamano ya Mizigo bandarini na masogamano ya foleni bila kuiboresha Trl na Tazara.
 
Kimizani chenyewe kina ile barabara nyembamba ya kuingilia kupima afu kimekua curved sijui kama wajagonga zile kingo za barabara madrivers.


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mzani upo mbali na barabara na ile expressway itajengwa tofauti kabisa ni hii iliyopo kwa kuwa mradi huo utakuwa wa ubia kati ya Serikali na makampuni binafsi yaani PPP na hivyo kutenga njia ya watakaoshindwa kulipia(hii iliyopo sasa) na watakaolipia ( itajengwa kwa kutumia ardhi nyingine kabisa lakini parallel na ya sasa)

Kama ni hivo itakuwa poa
 
Hivi BMK huyu alimuhusu? au ataenda siku ya kupiga kura tu? atakuwa amejadili nini?
 
Back
Top Bottom