Tatizo la maji Morogoro

1800

JF-Expert Member
Dec 27, 2010
2,215
603
Leo ni siku ya kumi hakuna maji Morogoro,maeneo kama ya Kola,Bigwa,Nane nane nk ni makame kabisa na hakuna hata tone la maji,mamlaka husika (MOROWASA) imekaa kimya haitoi sababu yeyote wala haikutoa tahadhari yoyote kabla,mnatudondoshea ma bill tu na kukimbilia kuja kukata mabomba wakati huduma hamtoi na zinazidi kuzorota kadri ya siku ziendavyo!maji yakitoka ni machafu,yanakuja na mchanga na mizizi kama vile tumekwenda kuchota mtoni na si maji yanayokua treated na mamlaka husika!tunaomba kujuzwa ubabaishaji huu kwenye kila idara muhimu za serikali utakoma lini?tunahitaji maji Morogoro,sio blah blah!
 
Maeneo ya bigwa maji yalitoka juzi saa sita usiku tena madogo hatari. Sasa kwani maji yatoke usiku wa manane wakati watu wamelala.
 
Maeneo ya bigwa maji yalitoka juzi saa sita usiku tena madogo hatari. Sasa kwani maji yatoke usiku wa manane wakati watu wamelala.

Hii nchi hawa watendaji wetu ni wababaishaji sana,kila idara ni uozo,sioni sababu ya Morogoro kukosa maji siku zote hizo wakati vyanzo vya maji ni vya uhakika,miundombinu nayo iko vizuri,huu ni uzembe na ubabaishaji wa viongozi mamlaka husika,na yote inasababishwa na kukosa umakini kwa viongozi wa wizara husika!wanatoa maji saa nane usiku ili wachote kina nani sasa?huyu mbunge wetu nae yuko wapi kusimamia ili?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom