ndege joni
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 689
- 1,126
Habari zenu wadau...
Mimi ni mmiliki wa gari ya abiria na pia ni konda wa gari yangu. nafanya route kutoka sehemu moja mkoani mwanza.
Kinachonipa shida ni hawa askari wa barabarani, wanatusumbua sana.
Nielezee kidogo kero. Wametuwekea utaratibu wa kuwapa rushwa kila siku tsh.... kila kituo walipo hawa askari. Hii haijalishi gari ni bovu au zima, sasa unakuta wilaya moja mf. Misungwi wana vituo vingi sana barabarani. Utalipa nauli zote ulizokusanya kwa hawa jamaa. Usipowapa ndo wanaanza kukagua gari, na lazima wakukute na kosa. Mara hujavaa uniform, mara tairi, kioo kina kreki, tiketi, mkanda n.k takataka kibao. Utalipa kila kosa 30,000. Usipolipa gari inapelekwa kituoni. Shotikati ni rushwa tu
Haliishii hapa, hawa ni askari tu wa barabarani. Ikatokea akaja vehicle, haangalii ushalipa ama bado. Ndo anakagua upya na lazima ulipe. Na tochi walizowapa ni kwa ajili ya ulaji wao na sio kusaidia abiria. Kwa sababu gari zinapunguza spidi wakipeana ishara kuwa kuna tochi.
Waziri wa mambo ya ndani uko wapi? Tunaomba tusaidiwe muweke utaratibu vizuri. Maaskari wanapata pesa nyingi kuliko hata wamiliki wa magari, tuna majukumu mengi na familia tuangalieni. Kama gari ina tatizo... bora itolewe barabarani kuliko kuwatesa watu kiasi hicho. Abiria pia wanaathirika kiasi kikubwa, tunawachelewesha kwenda kwenye kazi zao kwa sababu ya hawa wala rushwa.
Raisi wetu mtukufu tumempa kura atusaidie, tunamwomba kwa misimamo yake tunayoiona atuangalie. Magari mengi ya mkopo tunaumia. Maaskari wa barabarani hawamsaidii kusaidia wananchi, wanakula zao tu. Ukiangalia ndio watumishi pekee wanaojenga nyumba bila shida. Na ndio wanaomiliki magari
Mimi ni mmiliki wa gari ya abiria na pia ni konda wa gari yangu. nafanya route kutoka sehemu moja mkoani mwanza.
Kinachonipa shida ni hawa askari wa barabarani, wanatusumbua sana.
Nielezee kidogo kero. Wametuwekea utaratibu wa kuwapa rushwa kila siku tsh.... kila kituo walipo hawa askari. Hii haijalishi gari ni bovu au zima, sasa unakuta wilaya moja mf. Misungwi wana vituo vingi sana barabarani. Utalipa nauli zote ulizokusanya kwa hawa jamaa. Usipowapa ndo wanaanza kukagua gari, na lazima wakukute na kosa. Mara hujavaa uniform, mara tairi, kioo kina kreki, tiketi, mkanda n.k takataka kibao. Utalipa kila kosa 30,000. Usipolipa gari inapelekwa kituoni. Shotikati ni rushwa tu
Haliishii hapa, hawa ni askari tu wa barabarani. Ikatokea akaja vehicle, haangalii ushalipa ama bado. Ndo anakagua upya na lazima ulipe. Na tochi walizowapa ni kwa ajili ya ulaji wao na sio kusaidia abiria. Kwa sababu gari zinapunguza spidi wakipeana ishara kuwa kuna tochi.
Waziri wa mambo ya ndani uko wapi? Tunaomba tusaidiwe muweke utaratibu vizuri. Maaskari wanapata pesa nyingi kuliko hata wamiliki wa magari, tuna majukumu mengi na familia tuangalieni. Kama gari ina tatizo... bora itolewe barabarani kuliko kuwatesa watu kiasi hicho. Abiria pia wanaathirika kiasi kikubwa, tunawachelewesha kwenda kwenye kazi zao kwa sababu ya hawa wala rushwa.
Raisi wetu mtukufu tumempa kura atusaidie, tunamwomba kwa misimamo yake tunayoiona atuangalie. Magari mengi ya mkopo tunaumia. Maaskari wa barabarani hawamsaidii kusaidia wananchi, wanakula zao tu. Ukiangalia ndio watumishi pekee wanaojenga nyumba bila shida. Na ndio wanaomiliki magari