Tatizo la kutopata Choo

Tatizo la kutopata Choo

yello masai

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2016
Posts
3,901
Reaction score
4,128
Habar wakuu,
Nimekuwa na tatizo la kutopata choo. Nilikaa kama wiki sijapata choo nikaamua kutumia dawa za "Bisacodyl", zilisaidia nikaharisha sana. Lakini tangu hapo zimepita wiki mbili sijapata choo tena, ikitokea napata kidogo saana kama punje alaf kigumu sana japo nakula chakula kama kawaida na matunda kama parachichi, ndizi, nk.
Imefika hatua naanza kusikia chakula kinajazana karibia kifike kifuani.

Naomba msaada wa ushauri nini nifanye kutatua hili.
 
Habar wakuu,
Nimekuwa na tatizo la kutopata choo. Nilikaa kama wiki sijapata choo nikaamua kutumia dawa za "Bisacodyl", zilisaidia nikaharisha sana. Lakini tangu hapo zimepita wiki mbili sijapata choo tena, ikitokea napata kidogo saana kama punje alaf kigumu sana japo nakula chakula kama kawaida na matunda kama parachichi, ndizi, nk.
Imefika hatua naanza kusikia chakula kinajazana karibia kifike kifuani.

Naomba msaada wa ushauri nini nifanye kutatua hili.
Pole sana ndugu.

Kwa kuwa unakula vyakula vyenye fibre kama parachichi na ndizi, lakini tatizo bado liko pale pale, pendelea kula vyakula vyenye fibres kwa wingi kama viazi vitamu ambavyo vina soluble fibre(pectin) na insoluble fibre(cellulose) kama chakula chako cha kila siku, vyakula vyenye nyuzinyuzi kama mboga mboga.

Iwapo tatizo lako halisababishwi na magonjwa ya mfumo wa chakula, na ni mtu wa kukaa muda mrefu bila kufanya physical body movements hata kidogo, anza kufanya mazoezi hata ya kutembea tembea mara kadha kwa siku, ikibidi kukimbia. Hii itasaidia kuongeza kasi ya chakula kusafiri kwa haraka kwenye utumbo, hasa utumbo mpana ambako mabaki ya chakula yakikaa muda mrefu, maji yote hufyonzwa na kufanya kinyesi kuwa kigumu.

Kunywa maji mengi.

Kwangu hayo yalisaidia baada ya kuhangaika na hilo tatizo zaidi ya mwaka mmoja baada ya kukatishwa tamaa hospitali ambako niliambiwa tatizo ni kutokunywa maji mengi pekee.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom