Tatizo hili linaninyima raha na Amani

Tatizo hili linaninyima raha na Amani

Joined
Feb 26, 2026
Posts
14
Reaction score
34
Habari za wakati huu wapendwa,Naomba niwaelezee tatizo langu pengine mnaweza kunisaidia Nina shida moja sijui ni aleji ama ni nini maana niliwai enda hosptal ya wilaya hawakuona tatizo,pia kipato changu ni kidogo cha kuniwezesha kwenda hospital kubwa kwa vipimo vikubwa

Shida yangu ni nikikaa juani au kutembea juani kwamuda mrefu kidogo badae nikaa nikatulia nasikia kama kuna maji yanasambaa kwenye fuvu la kichwa na kushuka chini kuelekea kwenye shingo ni kama barafu iliyokua imeganda sasa imepigwa na jua inayeyuka

Cha kushangaza ni kua nikivaa kofia nikashinda juani kwa muda mrefu hiyo hali aitokei kabisa

Asanteni kwa kunisikiliza, nipo hapa kusoma ushauri wenu na maoni mtakayonipa
 
Uzuri ushajua jinsi ya kukabiliana na hiyo shida yako so tafuta hela nenda hospital kubwa
 
Hii huitwa vasolidation lakini husababishwa na pia Unapokuwa juani mishipa ya damu kichwani hupanuka ili kupunguza joto. Unaporudi kivulini mishipa hiyo huanza kusinyaa kurudi hali ya kawaida. Hisia hiyo ya maji yanayotiririka inaweza kuwa ni mzunguko wa damu unaporejea katika hali yake ya kawaida
 
1. Achana na kelele za wahuni, kata bima hizi nafuu zinazotolewa serikalini nenda hospitalini

2. Kuhusu hlo tatzo
Naliona kama muujiza, wahi hosp haraka, kabla huo muujiza haujawa mkubwa.
 
Je, unapata shida ya usingizi, ganzi viganjani au miguuni, au kichwa kuuma sometimes? Iki jibu ni ndio kati ya maswali hayo basi kuna uwezekano unatatizo la mfumo wa wa fahamu. Chukua hatua kwani inaweza sababisha body paralyze
 
Back
Top Bottom