Jamani naomba msaada wa kitabibu wa tatizo la kutoka vipele na muwasho mkali nikiwa kwenye jua

PRPP synthetase

Senior Member
Mar 16, 2017
193
80
Mimi ni kijana wa miaka 28 mkazi wa Singida japo kwa sasa nipo Iringa.

Mwaka 2018 nilikuwa Mbeya kimasomo ni mwanafunzi wa mambo ya afya katika kada ya afya. Tatizo linalonisumbua ni kuwa mwili huwa unapata msisimko kama aleji, allergy pindi nikipata joto au msisimko wa uoga.

Hali hii ilianza mwaka 2018 nikiwa Mbeya. Nilikuwa siwezi kutoka juani wala kula chakula cha moto kwa sababu ilikuwa inaniletea reaction ambayo naweza kusema ni kama aleji.

Hali hii hutoweka pindi nikikaa kivulini au kujippoza kwa maji. Hii reaction huleta vipele vidogo ambavyo huwa vinasambaa mwili mzima ila vikubwa kama upele hubakia kwenye mikono na tumboni na mgongoni huwa vipele vidogo mithili ya vipele vya msisimko wakati wa baridi.

Vipele huwa vinaota na kuwasha sana na tiba pekee inakuwa ni mimi kukaa kivulini au kujimwagia maji ya baridi ili mwili upoe na baada ya hapo hii hali inaisha hadi nirudi tena kwenye jua au nipate joto kwa kunywa chai ya moto.

Niliwahi kwenda hospitali na kupatiwa hydrocortisone cream kupaka lakini haikufua dafu na hali hiyo iliendelea hadi nilipotoka huo mkoa wa mbeya na kurudi dodoma.

Mwaka huu pia kwenye kipindi cha likizo ya corona nilikuja iringa cha kushangaza hali hii imeendelea kunisumbua na nimekosa matibabu yake.

Ombi langu kwa wataalamu specialist wa ngozi kama wapo huku naomba anayeweza kunisaidia tatizo hili kwani linaninyima raha ya maisha na siwezi kufanya kazi za mikono kwani zikileta joto tu huwa inakuwa shida.
Hali hii nimeipata baada ya kukaa mbeya na iringa.

Haijawahi kunipata katika mikoa mingine ambayo nimewahi kuishi kama Dar, morogoro, singida, pwani na dodoma.

Naomba yeyote anayeweza kunisaidia kupata msaada, iwe hapa au hata pm.
Wasalaamu!
 
Kaka embu rudii NYUMBANI huendaa tukakusaidia ndugu zakoo ama nendaa madukaa ya dawa za asilii za kisunni watakusaidia pole xana
🙏🙏🙏🙏🙏🙏
 
Kutokana na maelezo yako, inaonekana tatizo hukupata unapotembela au kuishi mikoa yenye baridi.

Kuna kipindi fulani katika mihangaiko ya maisha yangu, niliweza kuishi sehemu yenye baridi sana. Nilikuwa napatwa na hali kama yako. Joto la mwili likipanda ghafla, basi mwili wote unakuwa unachoma choma (ila sikuwa natoka vipele).

Na baadhi ya sababu zilizokuwa zinapandisha joto la mwili ni :- kutembea haraka haraka kwa miguu hata kama hakuna jua, kutembea juani, kunywa chai ya moto, na kuoga maji ya moto (japo hii ya kuoga maji ya moto mm ilikuwa ni mara chache sana, japo mwenzangu ndio ilikuwa inamtokea kila anapomaliza kuoga, maana lazima atenge dakika kadhaa zakujikuna)

Sikuwahi kutumia dawa yoyote wala kwenda hospitali. Na ilo tatizo kwasasa sina kabisa/sijakutana nalo nina kipindi kirefu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kijana pole,nitakuelekeza dawa ya asili itakusaidia natatizo ilo ndio mwisho. Tafuta majani ya mpera yanaweza kuwa mabichi au makavu yachemshe kwa muda kisha chuja alafu kunywa kwa siku mala mbili kila siku grasi mbili tu utaitumia kwa siku 30 bila kuacha utakuwa mwisho wa tatizo ilo.
 
Kaka embu rudii NYUMBANI huendaa tukakusaidia ndugu zakoo ama nendaa madukaa ya dawa za asilii za kisunni watakusaidia pole xana
Kurudi nyumbani bila suluhisho sizani kama ni njia sahihi mkuu!
Natafuta matibabu zaidi
 
Kutokana na maelezo yako, inaonekana tatizo hukupata unapotembela au kuishi mikoa yenye baridi.

Kuna kipindi fulani katika mihangaiko ya maisha yangu, niliweza kuishi sehemu yenye baridi sana. Nilikuwa napatwa na hali kama yako. Joto la mwili likipanda ghafla, basi mwili wote unakuwa unachoma choma (ila sikuwa natoka vipele)...
Asante mkuu ngoja nione itakuwaje mana hii hali huwa sio poa!
 
Kijana pole,nitakuelekeza dawa ya asili itakusaidia natatizo ilo ndio mwisho.
Tafuta majani ya mpera yanaweza kuwa mabichi au makavu yachemshe kwa muda kisha chuja alafu kunywa kwa siku mala mbili kila siku grasi mbili tu utaitumia kwa siku 30 bila kuacha utakuwa mwisho wa tatizo ilo.
Asante sana....
Glass moja asubuhi na jioni pia moja au mbili kwa kila muda wa matumizi?
 
Back
Top Bottom