Tathmini yangu ya utendaji wa Rais Magufuli kwa kipindi cha miaka mitatu na nusu cha uongozi

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Mar 1, 2016
12,695
31,478
Habari za asubuhi wana JF.

Kwa heshima na taadhima naomba nitoe tathmini ya haki kwa utendaji wa Mh Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kimsingi, miaka mitatu na nusu ni kipindi kizuri cha kupima utendeaji na kutolea mapendekezo ya kuboresha kwenye kipindi cha mwaka mmoja na nusu uliobakia, kama hatakuwa na nia ya kugombea kipindi kingine.

Kwanza kabisa naomba nieleze bayana ninampima Raisi kwa kutumia vigezo vifuatavyo:

1. Ustawi wa uchumi wa Taifa;
2. Ustawi wa kiuchumi wa wananchi wa Tanzania;
3. Usalama wa nchi;
4 Usalama wa wananchi na mali zao; na
5. Uhimilivu kwenye siasa za kimataifa

Ustawi wa Uchumi wa Taifa
Uchumi wa taifa unakua kwa kiwango cha kuridhisha, japokuwa imani ya wawekezaji ilipotea hapo awali lakini uwekezaji unaanza kuja japo si kwa kasi sana. Ila uchumi upo imara na uwekezaji katika miundombinu ni wa hali ya juu sana. Kwangu mimi, nampa sifa nyingi sana kwa uwekezaji unaofanyika hususani kwenye reli, barabara, viwanja vya ndege, bandari, maji na umeme. Hali hii ikiendelea kwa miaka mitano ijayo taifa letu litakua limeingia kwenye kundi la nchi za uchumi wa kati.

Ustawi wa kiuchumi wa wananchi
Kimsingi serikali kazi yake ni kutengeneza miuondombinu wezeshi itakayofanya wananchi waweze kujiongeza kiuchumi. Miundombinu wezeshi ipo na sehemu kubwa ya wananchi wamepewa fursa kufanya shughuli zao bila ya kubugudhiwa na intervention mbali mbali zimefanyika ili kuweka mazingira wezeshi na hili pia nampongeza sana Mh. Raisi.

Usalama wa Nchi
Nchi yetu iko salama na hili si lakuzungumza sana

Usalama wa wananchi na mali zao
H
Ili kidogo linaleta mjadala, kuna hisia baadhi ya wananchi hawapo na mali zao hazipo salama na sehemu kubwa ya wananchi hawa ni wale wakosoaji. Naendelea kusisitiza wanachi wote na mali zao wanapaswa wawe salama bila kujali mitazamo yao kiitikadi. Kwa hili kidogo Mh. Raisi anapaswa kulifanyia kazi

Uhimilivu kwenye siasa za kimataifa
Niko kifua mbele kuona nchi yangu inasimamia mambo inayoyaamini bila kuogopa wala kujali mashinikizo kutoka kwa nchi zilizoendelea. Kwangu mimi hili ni jambo linalonipa faraja kuona tunapigania sovereignty yetu. Hongera sana Mh. Raisi, tulipata uhuru 1961 hakuna kurudi nyuma

Haya ni maoni yangu kama unayo ya kwako si vibaya ukaendelea bila kutokwa na povu
 
Habari za asubuhi wana JF.

Kwa heshima na taadhima naomba nitoe tathmini ya haki kwa utendaji wa Mh Raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.

Kimsingi, miaka mitatu na nusu ni kipindi kizuri cha kupima utendeaji na kutolea mapendekezo ya kuboresha kwenye kipindi cha mwaka mmoja na nusu uliobakia, kama hatakuwa na nia ya kugombea kipindi kingine.

Kwanza kabisa naomba nieleze bayana ninampima Raisi kwa kutumia vigezo vifuatavyo:

1. Ustawi wa uchumi wa Taifa;
2. Ustawi wa kiuchumi wa wananchi wa Tanzania;
3. Usalama wa nchi;
4 Usalama wa wananchi na mali zao; na
5. Uhimilivu kwenye siasa za kimataifa

Ustawi wa Uchumi wa Taifa
Uchumi wa taifa unakua kwa kiwango cha kuridhisha, japokuwa imani ya wawekezaji ilipotea hapo awali lakini uwekezaji unaanza kuja japo si kwa kasi sana. Ila uchumi upo imara na uwekezaji katika miundombinu ni wa hali ya juu sana. Kwangu mimi, nampa sifa nyingi sana kwa uwekezaji unaofanyika hususani kwenye reli, barabara, viwanja vya ndege, bandari, maji na umeme. Hali hii ikiendelea kwa miaka mitano ijayo taifa letu litakua limeingia kwenye kundi la nchi za uchumi wa kati.

Ustawi wa kiuchumi wa wananchi
Kimsingi serikali kazi yake ni kutengeneza miuondombinu wezeshi itakayofanya wananchi waweze kujiongeza kiuchumi. Miundombinu wezeshi ipo na sehemu kubwa ya wananchi wamepewa fursa kufanya shughuli zao bila ya kubugudhiwa na intervention mbali mbali zimefanyika ili kuweka mazingira wezeshi na hili pia nampongeza sana Mh. Raisi.

Usalama wa Nchi
Nchi yetu iko salama na hili si lakuzungumza sana

Usalama wa wananchi na mali zao
H
Ili kidogo linaleta mjadala, kuna hisia baadhi ya wananchi hawapo na mali zao hazipo salama na sehemu kubwa ya wananchi hawa ni wale wakosoaji. Naendelea kusisitiza wanachi wote na mali zao wanapaswa wawe salama bila kujali mitazamo yao kiitikadi. Kwa hili kidogo Mh. Raisi anapaswa kulifanyia kazi

Uhimilivu kwenye siasa za kimataifa
Niko kifua mbele kuona nchi yangu inasimamia mambo inayoyaamini bila kuogopa wala kujali mashinikizo kutoka kwa nchi zilizoendelea. Kwangu mimi hili ni jambo linalonipa faraja kuona tunapigania sovereignty yetu. Hongera sana Mh. Raisi, tulipata uhuru 1961 hakuna kurudi nyuma

Haya ni maoni yangu kama unayo ya kwako si vibaya ukaendelea bila kutokwa na povu
Wee endelea kujipendekeza.
 
Kwa kumbukumbu zangu wewe ni critic mkali wa JPM, kwa mnyumbuliko huu wa Hoja itoshe kusema taratibu mnaanza kumuelewa JPM japo kwa kuchelewa

๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘
 
Kwa kumbukumbu zangu wewe ni critic mkali wa JPM, kwa mnyumbuliko huu wa Hoja itoshe kusema taratibu mnaanza kumuelewa JPM japo kwa kuchelewa

๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘๐Ÿ‘
Kwanza niweke kumbu kumbu sawa mimi si critic wa JPM au mtu mwingine yoyote, nina jenga hoja na kuzitetea. Ninasema yale ninayoyaamini na sina sababu ya kumpinga mtu bila sababu yoyote. Pili, siitajiki kumuelewa au kutomuelewa Mh Raisi, yeye ameomba kura kwa wa-Tanzania ili awatumikie na hiyo ni kazi yake na sisi wananchi tutampima utendaji wake kama nilivyofanya hapo juu.
 
Kwanza niweke kumbu kumbu sawa mimi si critic wa JPM au mtu mwingine yoyote, nina jenga hoja na kuzitetea. Ninasema yale ninayoyaamini na sina sababu ya kumpinga mtu bila sababu yoyote. Pili, siitajiki kumuelewa au kutomuelewa Mh Raisi, yeye ameomba kura kwa wa-Tanzania ili awatumikie na hiyo ni kazi yake na sisi wananchi tutampima utendaji wake kama nilivyofanya hapo juu.
Acha kukataa bhana wewe ni ufipa au unataka ushaidi? ๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
 
Kwenye huo "ustawi wa uchumi wa wananchi" ulioulezea, umewalenga wananchi wepi hao kwa mfano? Mama ntilie, bodaboda, wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara, au kundi gani hasa? Ni wananchi wote wamenufaika na utawala wake?

Maana kwa sisi wafanyakazi tunamuona kama kiumbe mmoja hivi asiye na faida yoyote ile kwetu. Maana eidha ameyarudisha maisha yetu nyuma, au ameyafanya yabakie pale yalipo.

Ametusumbua tu bila sababu kwenye zoezi lake la uhakiki wa vyeti, ametuongezea makato ya bodi kutoka 8% mpaka 15% huku akiwa hajawahi kuongeza mshahara kama mtangulizi wake, madaraja yanapandishwa kwa kuvizia! wengi hawajapandishwa na utaratibu umevurugika kabisa, nk.
 
Ni uamuzi wako kuniweka kwenye kundi lolote utakalo, ila sina chama na si shabiki wa siasa zenu uchwara
๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚ Tatizo ufipa wenzako wataanza kutunanga kwamba tumekununua kumbe ni uchapa kazi wa JPM umekukosha
 
Kwenye huo "ustawi wa uchumi wa wananchi" ulioulezea, umewalenga wananchi wepi hao kwa mfano? Mama ntilie, bodaboda, wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara, au kundi gani hasa? Ni wananchi wote wamenufaika na utawala wake?

Maana kwa sisi wafanyakazi tunamuona kama kiumbe mmoja hivi asiye na faida yoyote ile kwetu. Ametusumbua tu bila sababu kwenye zoezi lake la uhakiki wa vyeti, ametuongezea makato ya bodi kutoka 8% mpaka 15% huku akiwa hajawahi kuongeza mshahara kama mtangulizi wake, madaraja yanapandishwa kwa kuvizia! wengi hawajapandishwa na utaratibu umevurugika kabisa, nk.
Mkuu, ni kweli wafanyakazi hamjaongezwa mishahara na pia mnakatwa makato ya mikopo ya kulipia gharama za chuo, ila wafanyakazi wanawakilisha asilimia ndogo sana ya wananchi wa Tanzania. Nchi hii asilimia zaidi ya 60% ni wakulima na sehemu nyingine ni wafanya biashara, wavuvi, wafugaji, wawindaji na wadangaji. Hivyo, mazingira wezeshi yamewekwa kwa jamii kubwa zaidi na hili linanipa kibali kusema hayo niliyosema
 
Kwenye huo "ustawi wa uchumi wa wananchi" ulioulezea, umewalenga wananchi wepi hao kwa mfano? Mama ntilie, bodaboda, wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara, au kundi gani hasa? Ni wananchi wote wamenufaika na utawala wake?

Maana kwa sisi wafanyakazi tunamuona kama kiumbe mmoja hivi asiye na faida yoyote ile kwetu. Maana eidha ameyarudisha maisha yetu nyuma, au ameyafanya yabakie pale yalipo.

Ametusumbua tu bila sababu kwenye zoezi lake la uhakiki wa vyeti, ametuongezea makato ya bodi kutoka 8% mpaka 15% huku akiwa hajawahi kuongeza mshahara kama mtangulizi wake, madaraja yanapandishwa kwa kuvizia! wengi hawajapandishwa na utaratibu umevurugika kabisa, nk.
Huo mkopo unaoulalamikia mwanao akiukosa chuoni utaanza tena kulalamikia serikali bila kujua ni JPM ndio kaongeza idadi ya loan beneficiaries zaidi ya mara 5 ya awamu ya 4
 
Mkuu, ni kweli wafanyakazi hamjaongezwa mishahara na pia mnakatwa makato ya mikopo ya kulipia gharama za chuo, ila wafanyakazi wanawakilisha asilimia ndogo sana ya wananchi wa Tanzania. Nchi hii asilimia zaidi ya 60% ni wakulima na sehemu nyingine ni wafanya biashara, wavuvi, wafugaji, wawindaji na wadangaji. Hivyo, mazingira wezeshi yamewekwa kwa jamii kubwa zaidi na hili linanipa kibali kusema hayo niliyosema

Ni asilimia ndogo lakini ina athari nyingi chanya kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi Leo hii biashara nyingi mtaani ziko hoi, wakulima wanauza mazao na bidhaa zao kwa bei ya chini kabisa, nk. Sababu kuu ni hiyo tu!

Purchasing power imekuwa chini kwa sababu ya wafanyakazi kulazimishwa kuishi maisha yale yale tangu mwaka 2015 kwa kisingizio cha kununua ndege na kujenga standard gauge.This is unfair!

Wafanyakazi ni wachache, lakini ndiyo wanunuzi wakuu wa hizo bidhaa za wakulima, wafanyabiashara, nk. Hayo makundi matatu siku zote hutegemeana.
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Njoo na statistics za ulinganishi kati ya Tanzania na nchi nyingine pia ulinganishi kati ya mwaka 2015 na 2018.

If there is statistical significance to agree with your tathimini
 
Huo mkopo unaoulalamikia mwanao akiukosa chuoni utaanza tena kulalamikia serikali bila kujua ni JPM ndio kaongeza idadi ya loan beneficiaries zaidi ya mara 5 ya awamu ya 4

Haitokuja itokee nikaruhusu mtoto wangu asome kwa kutegemea huo mkopo wa serikali. Labda Mungu anipende zaidi kabla ya huo muda wa wao kusoma hiyo elimu ya juu kuwadia. Na siombei hilo hata siku moja.
 
Ni asilimia ndogo lakini ina athari nyingi chanya kwenye ukuaji wa uchumi wa nchi Leo hii biashara nyingi mtaani ziko hoi, wakulima wanauza mazao na bidhaa zao kwa bei ya chini kabisa, nk. Sababu kuu ni hiyo tu!

Purchasing power imekuwa chini kwa sababu ya wafanyakazi kulazimishwa kuishi maisha yale yale tangu mwaka 2015 kwa kisingizio cha kununua ndege na kujenga standard gauge.This is unfair!

Wafanyakazi ni wachache, lakini ndiyo wanunuzi wakuu wa hizo bidhaa za wakulima, wafanyabiashara, nk. Hayo makundi matatu siku zote hutegemeana.
Mkuu, hiyo ni dhana potofu ambayo inabidi kwanza uondokane nayo. Uchumi wetu ni private sector driven na kwa kuangalia kwa macho ya kawaida ni small and medium enterprises na si wafanyakazi wa serikali. Ukishajua hilo hapo ndipo utakapojua kwamba serikali, kwa wingi, haijafikisha wafanyakazi milioni moja na je hao watu waliosalia zaidi ya milioni hamsini na tatu wanafanya shughuli gani?
 
Bila shaka kuna kitu umekisahau kukiandika kwenye hii thread yako
Anyway acha na wenzangu waje na wao waseme
 
Njoo na statistics za ulinganishi kati ya Tanzania na nchi nyingine pia ulinganishi kati ya mwaka 2015 na 2018.

If there is statistical significance to agree with your tathimini
Mkuu hii ni tathmini kwa ajili ya matumizi ya watu wa kawaida kama mimi. Ukitaka niweke statistics na kufanya comparative analysis hili jambo litakua kubwa sana, itoshe kuwa tahmini tu
 
Back
Top Bottom