ngara23
JF-Expert Member
- Aug 31, 2019
- 15,874
- 36,315
Rais Samia aliapa tarehe March 21, 2021, baada ya Kifo cha Aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Magufuli
Leo ametimiza miaka 4
Rais Samia amekuwa Bora kuliko mtangulizi wake Magufuli
Watanzania tulikuwa gizani kipindi cha utawala wa Magufuli,
Samia alikuta hali mbaya ya Kisiasa kiuchumi, Kidplomasia na kidemocrasia
1. Uhuru wa kujieleza
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Samia ametupa haki ya kujieleza tofauti na mtangulizi wake ambaye hakutaka kukoselewa
2. Mahusiano kidplomasia
Kipindi cha Magufuli nchi ilidorora kidplomasia, Magufuli akijifungia Magogoni ila mama amefanya vyema upande huo
3 Uchumi wa wananchi unaimarika
Kwa Sasa kama unajituma pesa unapata
Mazao yamepanda bei, wafanyabiashara waliokimbia wamerudi, ajira Kwa vijana zipo
Sasa pesa tunazo mfukoni sio kama kipindi cha utawala wa Magufuli alikuwa akipika takwimu za uchumi kujua lakini kiuhalisia mfukoni tulikuwa hoi
4 Huduma za kijamii
Samia ameimarisha ujenzi wa madarasa ya kisasa, Zahanati, umeme,maji n.k
Sio kama kipindi cha Magufuli anazindua hadi choo cha soko, yaani maigizo tu
5 Kufufua shirika la ndege
Magufuli kama alikuja kuliua shirika la ndege.
Ambapo madege yake ya pangaboi kama feni za magetoni Buguruni yaliishia Karakana na shirika likafirisika.
Rais Samia amelifufua na Sasa ATCL inajiendesha Kwa faida
6. Kufufua mifuko ya jamii na Bima
Kipindi cha Magufuli alikomba pesa zote kwenye mifuko ya jamii na hii mifuko ilikuwa na hali mbaya na akaishia kutunga sheria kali Kwa wanafuika
7 Elimu ya juu
Mikopo imeongezeka na sera nzuri watoto wa kitanzania wote wananufaika na mifuko hii
Magufuli alibagua na kutaka wanufaika wawe tu waliosoma government school
8
. Utalii
Watalii wanaongezeka tofauti na zamani
Madhaifu
1. Vitendo vya utekaji
Mwasisi wa wasiojulikana tunamjua, ila hawa watekaji na wauji wameendelea kuwepo hili linamchafua Rais Samia
Naamini Samia akitumia vyombo vyake atagundua waliomteka na kumuua Mzee Kibao na wengine waliopotea
2 Rushwa na Uwajibikaji
Vitendo vya rushwa viko wazi.
Nashauri Rais Samia aimariahe Taasisi ya TAKUKURU kuwabaini, kuwakamata na kuwashitaki wanaohujumu uchumi na madisadi
3. Masai wa Ngorongoro
Kuwahamisha Masai kutoka Ngorongoro ni kati ya kitendo ambacho hakikunifurahisha.
Hasara ni kubwa kuliko hasara na haki za hao Watanganyika wenzetu
4. Ubinafishwaji wa bandari
Naamini washauri wa mama, walimpa ushauri wa ovyo wa kubinafsisha bandari zetu Kwa Warabu.
Apate muda apitie hii sera ya ubinafshaji
5 Kumaliza miradi
Kuna miradi imekaa muda mrefu kama sisi Kanda ya ziwa daraja la Busisi Lina Mika zaidi ya 7 halimaliziki kwanini?
Meli ya Ziwa Victoria kwenda Bukoba miaka mingi haianzi safari kwanini
Hongera Rais Samia Suluhu Hasan
Mungu akupe Maisha marefu
Leo ametimiza miaka 4
Rais Samia amekuwa Bora kuliko mtangulizi wake Magufuli
Watanzania tulikuwa gizani kipindi cha utawala wa Magufuli,
Samia alikuta hali mbaya ya Kisiasa kiuchumi, Kidplomasia na kidemocrasia
1. Uhuru wa kujieleza
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni, Samia ametupa haki ya kujieleza tofauti na mtangulizi wake ambaye hakutaka kukoselewa
2. Mahusiano kidplomasia
Kipindi cha Magufuli nchi ilidorora kidplomasia, Magufuli akijifungia Magogoni ila mama amefanya vyema upande huo
3 Uchumi wa wananchi unaimarika
Kwa Sasa kama unajituma pesa unapata
Mazao yamepanda bei, wafanyabiashara waliokimbia wamerudi, ajira Kwa vijana zipo
Sasa pesa tunazo mfukoni sio kama kipindi cha utawala wa Magufuli alikuwa akipika takwimu za uchumi kujua lakini kiuhalisia mfukoni tulikuwa hoi
4 Huduma za kijamii
Samia ameimarisha ujenzi wa madarasa ya kisasa, Zahanati, umeme,maji n.k
Sio kama kipindi cha Magufuli anazindua hadi choo cha soko, yaani maigizo tu
5 Kufufua shirika la ndege
Magufuli kama alikuja kuliua shirika la ndege.
Ambapo madege yake ya pangaboi kama feni za magetoni Buguruni yaliishia Karakana na shirika likafirisika.
Rais Samia amelifufua na Sasa ATCL inajiendesha Kwa faida
6. Kufufua mifuko ya jamii na Bima
Kipindi cha Magufuli alikomba pesa zote kwenye mifuko ya jamii na hii mifuko ilikuwa na hali mbaya na akaishia kutunga sheria kali Kwa wanafuika
7 Elimu ya juu
Mikopo imeongezeka na sera nzuri watoto wa kitanzania wote wananufaika na mifuko hii
Magufuli alibagua na kutaka wanufaika wawe tu waliosoma government school
8
. Utalii
Watalii wanaongezeka tofauti na zamani
Madhaifu
1. Vitendo vya utekaji
Mwasisi wa wasiojulikana tunamjua, ila hawa watekaji na wauji wameendelea kuwepo hili linamchafua Rais Samia
Naamini Samia akitumia vyombo vyake atagundua waliomteka na kumuua Mzee Kibao na wengine waliopotea
2 Rushwa na Uwajibikaji
Vitendo vya rushwa viko wazi.
Nashauri Rais Samia aimariahe Taasisi ya TAKUKURU kuwabaini, kuwakamata na kuwashitaki wanaohujumu uchumi na madisadi
3. Masai wa Ngorongoro
Kuwahamisha Masai kutoka Ngorongoro ni kati ya kitendo ambacho hakikunifurahisha.
Hasara ni kubwa kuliko hasara na haki za hao Watanganyika wenzetu
4. Ubinafishwaji wa bandari
Naamini washauri wa mama, walimpa ushauri wa ovyo wa kubinafsisha bandari zetu Kwa Warabu.
Apate muda apitie hii sera ya ubinafshaji
5 Kumaliza miradi
Kuna miradi imekaa muda mrefu kama sisi Kanda ya ziwa daraja la Busisi Lina Mika zaidi ya 7 halimaliziki kwanini?
Meli ya Ziwa Victoria kwenda Bukoba miaka mingi haianzi safari kwanini
Hongera Rais Samia Suluhu Hasan
Mungu akupe Maisha marefu