TASWIRA; Magogoni leo!!

Kiganyi

JF-Expert Member
Apr 30, 2012
1,242
765

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Januari Makamba, kuwa Naibu Waziri wa Mawasiliano, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Shamsi Vuai Nahodha, kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Saada Mkuya Salum, kuwa Naibu Waziri wa Fedha, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha , Stephen Maselle, kuwa Naibu Waziri Nishati na Madini , wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha , Amos Makala, kuwa Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.

Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha , Janeth Mbene, kuwa Naibu Waziri wa Fedha, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha , Dkt. Fenella E. Mukangara, kuwa Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha , Eng. Christopher Chiza, kuwa Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha ,George Simbachawene , kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha Dkt. Hussein Mwinyi kuwa Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Rais Jakaya Kikwete, akimuapisha, Angela Jasmine Kairuki, kuwa Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Sehemu ya watu waliohudhuria hafla hiyo kwenye Viwanja vya Ikulu.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akizungumza na Mbunge wa Kigoma Kaskazini kupitia CHADEMA Zitto Kabwe kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam, leo, wakati wa hafla fupi ya kuwaapisha Mawaziri wapya wateule.
Rais Jakaya Kikwete, akimkabidhi nyaraka za Serikali, Dkt. William Mgimwa, baada ya kumuapisha kuwa Waziri Fedha, wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akifurahia jambo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Terezya Huvisa na Naibu Waziri wa Ofisi ya Makamu wa Rais, Charles Kitwanga 'Mawe Matatu', wakati wa hafla ya kuapishwa Mawaziri wapy iliyofanyika leo kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akisalimiana na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, baada ya hafla ya kuapishwa Mawaziri wapya walioteuliwa wiki iliyopita. Hafla hiyo ya kuwaapisha ilifanyika leo katika Viwanja vya Ikulu jijini Dar es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa katika picha ya pamoja ya kumbukumbu na Mawaziri wa Ofisi yake baada ya kuapishwa Mawaziri wapya wakati wa hafla fupi ya kuwaapishwa mawaziri iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es salaam leo. Kushoto ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano) Samia Suluhu, Wa pili (Kulia) ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Terezya Huvisa na Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais, aliyeteuliwa wiki iliyopita na kuapishwa leo, Charles Kitwanga 'Mawe Matatu'.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakiwapongeza baadhi ya Mawaziri na Manaibu baada ya kuapishwa wakati wa hafla fupi iliyofanyika kwenye Viwanja vya Ikulu Dar es Salaam leo.
Wazir wa Uchukuzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, akihojiwa na waandishi wa habari baada ya kuapishwa rasmi leo kushika wadhfa huo.
Rais Jakaya Kikwete, Makamu wake Dkt. Mohammed Gharib Bilal na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda na Katibu Mkuu Kiongozi, wakiwa katika picha ya pamoja na Mawaziri wateule baada ya kuapishwa rasmi leo Ikulu Dar es Salaam.
Mawaziri wakisubiri kuapishwa leo

Makamanda wakipozi kwa picha wakati wa hafla hiyo.
 
uchafu mtupu subirini waonje asali na hao kitabu kitajaa hiko cha kelele za bunge hawa wapya ndio hatari wanataka vya fasta
 
Nilijuwa tu Zitto Kabwe huwa akosekani sehemu kama hizi, ila kwa upande wa Baraza wanaotalajia jipya nawapa pole sana na mna moyo kweli kweli!!
 
haya ndo muda wao wa kuchapa kazi kwa wachapa kazi, kutanua kwa wanamatanuzi, kufisadi kwa mafisadi etc
 
Back
Top Bottom