Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,242
- 34,917
Aidha, Taslima amesema kuwa wanachama wa CUF na wananchi kiujumla wanatakiwa kujua kwamba kauli aliyoitoa Lipumba hivi karibuni ya kutengua barua yake ya kujiuzulu aliyomwandikia Katibu mkuu wa chama hicho Maalim Seif Shariff Hamad, haitazuia uchaguzi wa chama hicho kufanyika.
“Tulitaka tuweke mambo sawa kwa wananchi kwamba kauli ya Lipumba ya kutengua barua ya kujiuzulu kwake haimaanishi kwamba bado anashikilia wadhifa wa uenyekiti, bali kamati ya uongozi iko pale pale hadi mkutano mkuu wa kuchagua viongozi utakapofanyika,” amesema Taslima.
Amesema kauli inayotolewa na baadhi ya wananchama wa CUF ya kwamba hakuna mwanachama wa chama hicho mwenye uwezo wa kurithi na kuvaa viatu vya Lipumba si ya kweli na kwamba wako wanachama wenye uwezo huo na zaidi.
“Hao wanachama wanaosema kuwa Lipumba kwanza chama baadae na kwamba hakuna mwanachama atakayeweza vaa viatu vyake si wa kweli, chama hiki ni cha kila mtu na nafasi za uongozi zinastahili kugombaniwa na kila mtu,” amesisitiza