kimsboy
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 11,120
- 24,395
Leo tupeane ushuhuda wa Tarehe 29 ilikukuta wapi, ilikuaje ulivyoshtuka watu wapo barabarani?Na jee kuna story gani za watu waliouliwa uliziskia ukashtuka au zilizokuhuzunisha?Kipi kilikushangaza?Leo tupeane habari kuhusu tarehe 29
Nianze na mimi binafsi kabla ya tarehe 29 na marafiki zangu wanne tulipanga tutatoka kuandamana....Nakumbuka tulifanya kikao jumamosi ya tarehe 25 tukiwa watano tukijadili mambo ya nchi na jinsi tulivyojiandaa kuandamana
Tupo watu watano ambao tunaaminiana sana na tunashirikishana katika mambo nyeti kama haya.Kwa hali ilivyokua social media zilivyokua za moto tulijua kabisa tarehe 29 uhakika wa kutoka ni mkubwa.
Twende mbele kufupisha mambo,tarehe 28 tulikutana tena tukipiga story kuhusu tumejiandaa vipi nakumbuka jamaa yangu mmoja.alisema what if watu hawatotoka?Nikajisemea liwalo na liwe.
Usiku wa kuamkia tarehe 29 nakumbuka tulikua macho mtandaoni mpaka saa 7 usiku, nikaenda kulala nikiwa na shauku kubwa sana.
TAREHE 29 ASUBUHI...
Tuliamshana tutoke mapema saa 11 ila rafiki yangu akanambia tutoke saa 12 muda wa maandamano kuanza.Niliswali nikamuomba Mungu sana na wife alikua siku zote hataki nikaandamane akihofia nitauwawa japo haipendi serikali ya Samia wala ccm lakini alikua ananisihi nisiamandane, lakini nilimweleza ukweli wote kuwa ishu ya kuandamana inaanza na kila mmoja nikisema sitoki na yule akisema hatoki jee ni nani atatoka?
Kusubiriana tulijikuta tukikutana Goba tulikua jumla wanne tu pamoja na mimi yule mmoja tuliona anatuchelewesha
SAFARI IKAANZA
Tulitoka Goba kiukweli palikua hamna hata dalili ya maandamano, tukaenda hadi mbezi mwisho napo hakukua na dalili za maandamano, yule jamaa yetu ambaye alichelewa kutoka alitufata hadi mbezi mwisho kwa boda boda.Tulikaa mpaka saa tatu na robo hamna dalili ya maandamano kabisa kiasi kwamba tukaanza kukata tamaa na kilichoudhi ni kufungua mitandaoni na kuona barabara zote ni nyeupe na hakuna dalili za maandamano yoyote yale.
Tulikaa mahali hapo mbezi tukaanza kuulizana sasa itakuaje?Kiukweli nilijikatia tamaa na nilikua na hasira balaa nikasema why watanzania tumekua waoga kiasi hichi, tulikaa mbezi mpaka tukawaza turudi tu majumbani mwetu hapo nilikua na hasira balaa nikasema nikifika home siongei na mtu yoyote zaidi nitalala tu.
Nilikua nishakata tamaa kabisa, tukaona tuingie mgahawani tunywe tu chai maana tangu tulipotoka tulikua hatujala chochote.
MAANDAMANO YAKAANZA RASMI
Tumemaliza kunywa chai tunaanza kurudi zetu Goba ile tunavuka njia panda ya Goba ndo naona mtandaoni watu wameanza kujikusanya ubungo Kibo, Aisee hatukua na jinsi kwa haraka tulichukua pikipiki kila mmoja hadi Kibo, nilishuhudia watu kwa mamia wakielekea Kibo wakisogelea eneo ya Kibo nyomi za mbezi kimara zote zilielelekea Kibo!!
ITAENDELEA
Nianze na mimi binafsi kabla ya tarehe 29 na marafiki zangu wanne tulipanga tutatoka kuandamana....Nakumbuka tulifanya kikao jumamosi ya tarehe 25 tukiwa watano tukijadili mambo ya nchi na jinsi tulivyojiandaa kuandamana
Tupo watu watano ambao tunaaminiana sana na tunashirikishana katika mambo nyeti kama haya.Kwa hali ilivyokua social media zilivyokua za moto tulijua kabisa tarehe 29 uhakika wa kutoka ni mkubwa.
Twende mbele kufupisha mambo,tarehe 28 tulikutana tena tukipiga story kuhusu tumejiandaa vipi nakumbuka jamaa yangu mmoja.alisema what if watu hawatotoka?Nikajisemea liwalo na liwe.
Usiku wa kuamkia tarehe 29 nakumbuka tulikua macho mtandaoni mpaka saa 7 usiku, nikaenda kulala nikiwa na shauku kubwa sana.
TAREHE 29 ASUBUHI...
Tuliamshana tutoke mapema saa 11 ila rafiki yangu akanambia tutoke saa 12 muda wa maandamano kuanza.Niliswali nikamuomba Mungu sana na wife alikua siku zote hataki nikaandamane akihofia nitauwawa japo haipendi serikali ya Samia wala ccm lakini alikua ananisihi nisiamandane, lakini nilimweleza ukweli wote kuwa ishu ya kuandamana inaanza na kila mmoja nikisema sitoki na yule akisema hatoki jee ni nani atatoka?
Kusubiriana tulijikuta tukikutana Goba tulikua jumla wanne tu pamoja na mimi yule mmoja tuliona anatuchelewesha
SAFARI IKAANZA
Tulitoka Goba kiukweli palikua hamna hata dalili ya maandamano, tukaenda hadi mbezi mwisho napo hakukua na dalili za maandamano, yule jamaa yetu ambaye alichelewa kutoka alitufata hadi mbezi mwisho kwa boda boda.Tulikaa mpaka saa tatu na robo hamna dalili ya maandamano kabisa kiasi kwamba tukaanza kukata tamaa na kilichoudhi ni kufungua mitandaoni na kuona barabara zote ni nyeupe na hakuna dalili za maandamano yoyote yale.
Tulikaa mahali hapo mbezi tukaanza kuulizana sasa itakuaje?Kiukweli nilijikatia tamaa na nilikua na hasira balaa nikasema why watanzania tumekua waoga kiasi hichi, tulikaa mbezi mpaka tukawaza turudi tu majumbani mwetu hapo nilikua na hasira balaa nikasema nikifika home siongei na mtu yoyote zaidi nitalala tu.
Nilikua nishakata tamaa kabisa, tukaona tuingie mgahawani tunywe tu chai maana tangu tulipotoka tulikua hatujala chochote.
MAANDAMANO YAKAANZA RASMI
Tumemaliza kunywa chai tunaanza kurudi zetu Goba ile tunavuka njia panda ya Goba ndo naona mtandaoni watu wameanza kujikusanya ubungo Kibo, Aisee hatukua na jinsi kwa haraka tulichukua pikipiki kila mmoja hadi Kibo, nilishuhudia watu kwa mamia wakielekea Kibo wakisogelea eneo ya Kibo nyomi za mbezi kimara zote zilielelekea Kibo!!
ITAENDELEA