Taratibu za kuvalisha pete ya uchumba

Taratibu za kuvalisha pete ya uchumba

super black Boy

Senior Member
Joined
Oct 15, 2019
Posts
135
Reaction score
169
Rejea kichwa cha habar hapo juu!!

Mimi nilikuwa nahitaji kufahamu ikiwa mtu una mpenzi wako wa muda mrefu na unataka kumvalisha pete ya uchumba.

Je kuna taratibu zipi zinapasawa kufanywa hapa...binafsi nahitaji kujua kuwa ni lazima pande mbili za wazazi wafahamu kwanza kuwa mnamahusiano ndo mnavalishana pete ama tukio la kuvalisha pete ya uchumba haina haja ya kuwataarifu wazazi wote wa pande mbili?

Na Je ni lazima kutoa mahari kwanza ndo unavalisha pete ya uchumba au pete inavalishwa kwanza then ndo mahari inapelekwa?

naombeni msaada kwa wakubwa au kwa vijana wenzangu ambao mmeshapitia hii hatua!!

Ahsanteni na nawatakia jioni njema....
 
Imeitwa 'pete ya uchumba' basi ni wazi kua unapaswa kumtolea mahari ndio umvalishe pete, naona wengi huvalishana ile siku ya kutoa na kupokea mahari ambapo familia zote zinakuwepo inakua jambo flani hivi amazing.

Lakini pia mnaweza kuvalishana wenyewe wawili tu au mkavalishana mbele ya marafiki lakini bomba ni ile ya kumvalisha siku ya mahari.
 
culture gal, Namimi nauliza je kutuma barua yauchumba mpaka uwe namahari hata kidogo au unaweza kutumba barua yauchumba bila hata kutoa mahari kidogo?
 
Barua ya uchumba maana yake ni ombi kama ukikubaliwa wanakutajia mahari kisha utasema unaenda kulipa lini mahari yao.
OK, mkishaelewana mahari si busara kukaa mda gani bila kupunguza au kutoa hiyo mahari mara baada yakukubaliwa nakupata mahari
 
Lakini pia taratibu zinatofautiana kulingana na jamii, ni vema ukaijua jamii unayokwenda kuoa ili kujua wao taratibu zao zikoje, karibu kwenye chama kijana
 
super black Boy,

Hili tukio la kuvalishana pete tumeliiga kutoka kwa mabeberu lakini kwa maoni yangu naona tunalikosea.
Kisayansi, ilitakiwa binti avalishwe pete kwanza, ndio wazazi na ndugu wataarifiwe na mipango mingine ikiwepo mahari ifuate. Hii ni kutokana na ukweli kwamba siku binti anapovalishwa pete ndio siku binti anayotakiwa akubali (au akatae) kuolewa na huyo mwanaume.
Kwa wenzetu mabeberu, watu wanapokutana na kuanza urafiki, hua wanaweza kuwajulisha tu wazazi kwamba wanatoka wote. Hii itaendelea mpaka pale ambapo kijana atamvalisha pete ya uchumba binti. Tukio la kuvalishwa pete huwa ni sapraiz (hakuna sherehe) ambapo ndio jamaa akiwa na pete yake mkononi hupiga goti, na kumuuliza binti kama yupo tayari kuolewa nae. Binti akisema hayupo tayari baasi shughuli nzima inaishia hapo! Akikubali, hapo jamaa atamvalisha pete na ndipo sasa ndugu, jamaa na marafiki wanajulishwa na mipango mingine ya harusi inaanza.
Kwa hali hiyo, kusema mahari yatolewe siku ya kuvalishana pete, au kufanya sherehe ya kuvalishana pete, inapoteza maana nzima ya tukio lenyewe kwa kufanya assumption kwamba binti ameshakubali kuolewa. Na kama tumeshajua kwamba binti ameshakubali, basi hakuna tena haja ya kupiga goti na kumuuliza "will you marry me..?" Ikifuatiwa na kuangua kilio.
 
TheChoji, Ujinga kupiga goti na kulia Kama mtoto
Ni mwendo Wa kucheka tuu
tapatalk_1575219380147.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
MC pilipili anasema hatua ya kwanza ni mwanaume kulia machoz hadharani,mnavalishana Pete then mahari inafuata,huyu anyang'anywe heshima ya ubaharia awe shamba boy,hatufai sisi mabaharia tusioweza kulia hata pale tunapofiwa na wapendwa wetu
 
Back
Top Bottom