TANZIA: Mtangazaji wa Radio Free Africa, Tom Zuberi Msabaha amefariki dunia

Mungu amlaze pema peponi jamaa....then kuna jamaa mmoja akitangaza Kiss Fm Radio miaka ya 2007/09 akijiita kitu kama Kim sikumbuki sana jina lake ila alikuwa anamwaga ung'eng'e balaa yaani alikuwa akiongea anafanya kama anaRap kipindi chake kikiitwa Dj show sijui jamaa naye yupo wapi?muda sana simsikia kwa anaefaham naomba anijulishe.
 
anhaa sawa mkuu..Mungu amrehemu
Kifupi,Zuberi msabaha ni mwenyeji wa kigoma.Chanzo cha kwenda kuishi congo ni vita vya kagera mwaka 1979.Baada ya majigambo ya Nduli Dada kuwa ataifyeka Tanzania ndani ya masaa machache,familia yake waliamua kukimbilia congo kama wakimbizi happo Zuberi akiwa na umri wa miaka minne tu.

Hata baada ya vita ya kagera kuisha waliendelea kuishi huko,mpaka miaka ya tisini walipo amua kurudi home.
 
Kifupi,Zuberi msabaha ni mwenyeji wa kigoma.Chanzo cha kwenda kuishi congo ni vita vya kagera mwaka 1979.Baada ya majigambo ya Nduli Dada kuwa ataifyeka Tanzania ndani ya masaa machache,familia yake waliamua kukimbilia congo kama wakimbizi happo Zuberi akiwa na umri wa miaka minne tu.

Hata baada ya vita ya kagera kuisha waliendelea kuishi huko,mpaka miaka ya tisini walipo amua kurudi home.
anhaa asante kwa hii taarifa mkuu
 
Mungu amlaze pema peponi jamaa....then kuna jamaa mmoja akitangaza Kiss Fm Radio miaka ya 2007/09 akijiita kitu kama Kim sikumbuki sana jina lake ila alikuwa anamwaga ung'eng'e balaa yaani alikuwa akiongea anafanya kama anaRap kipindi chake kikiitwa Dj show sijui jamaa naye yupo wapi?muda sana simsikia kwa anaefaham naomba anijulishe.
Bila shaka unaanisha Borry the Pilot. Alikuwa anamwaga ung'eng'e kama mtoto wa malkia.
Mi nilijuaga ni mzungu.
 
Congo kwa nani? Kilio kipo Mabatini Mwanza! Atazikwa leo saa tisa alasili!
Mkuu,
Hilo usingelijibu sababu unapoteza calories zako bure. Maelezo yametolewa amefia wapi, lini, msiba uko wapi na atazikwa wapi sasa atoke Mtu aulize kama alirudi Lubumbashi au Coma Huyu kusoma hajui au alikuwa Mars wakati Maelezo yakitolewa? Ziro huyo!
 
View attachment 672376
Aliyekuwa mtangazaji wa Radio free afrika kipindi cha bolingo time, Mtangazaji Zuberi Msabaha afariki dunia.

Maziko yanatarajiwa kufanyika leo huko Mabatini, Mwanza. Mungu amuweke anapostaili mtaalamu huyo aliyekuwa na mvuto wake na uhodari wa kuendesha kipindi kupitia redio free Afrika.
View attachment 672372
dafity said;
Mtangazaji mahiri wa Sahara Media (RFA, KISS FM na STARTV) mtajwa hapo juu amefariki usiku wa kuamkia leo Jumatano January 10, 2018. Msiba upo Mabatini Mwanza.

Marehemu alikua mahiri katika kuzichambua nyimbo za Kilingala, KiCongo na Kikasai kutoka DRC na Congo-Brazaville.

Baadhi ya majina ya kazi aliyotumia ni 6000 volts na TonTon. Mazishi ni leo Jumatano saa 10 jioni hapa Mwanza
R.I.P....Tonton Msabaha.
Pamoja na kwamba hiyo Safari yetu sote lakini ya Msabaha imetugusa wengi hasa wapenzi wa bolingo basi! Tuseme "Nzambe Malamo!"
 
Rest In Peace Zuberi Msabaha jamaa alikua mtu safi sana nilikua nakutana nae enzi hizo nipo mwanza kikazi ananitafsria nyimbo za kikongo adi raha...Raha ya Milele Umpe ehhh Mwenyenzi Mungu....Mwenyenzi Mungu awafariji wafiwa na ampokee mja wake..Gone too soon Zuberi imeniuma sana
 
Oooh RIP Zuberi Msabaha ndio nafahamu kifo Chako leo,RFA imepoteza GWIJI,NGULI na MTANGAZAJI MWADILIFU. HAKIKA HAUTAFUTIKA KATIKA KUMBUKUMBU ZA JAMII YA WASIKILIZAJI WA KIPINDI CHAKO ULICHOKIJULIA SANA. AMEN.
 
Back
Top Bottom