Tanzia: Mama Hawa Ngulume afariki dunia!

Tanzia: Mama Hawa Ngulume afariki dunia!

Lol! Mkuu watu8, Wasukuma wa bonde la Usangu wakikusikia ukisema huyo mama RIP watatamani wakuloge na wewe,kama tunavyoweza kuamini kuwa walimloga mmbabe huyo aliye kuwa akiwacharaza viboko wasukuma wa bonde la usangu na kuwatia hasara kubwa sana kwa kutaifisha mifugo yao. Kama unaamini uchawi basi huyu mama kalogwa na wasukuma waliodhurumika dhuruma kuu chini ya uongozi wake alipokuwa mkuu wa wilaya ya Mbarali.

Wewe acha za kuleta wote wanaokufa kwa cancer wamelogwa na nani? Unaujua ugonjwa utakao kuua? Fikra kama hizi ndizo zinazosababisha maendeleo kurudi nyuma. Kila kitu kutafuta kisingizio cha rejareja. Tuwe na mtazamo wa kisayansi watanzania tuache ushabiki.
 
Yeye amekwenda. Zamu yako nayangu inasogea umejiaandaje? Hasa wewe kongosho
 
Alikuwa mtata na mbabe sana, alijua ataishi maisha yake yote akiwa kiongozi hivyo akaacha kujipanga kimaisha, magamba walimtupa mara baada ya kuanza kuugua, ilibidi aje hadharani kuomba msaada.

Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina la Bwana litukuzwe.

Wanadamu wengi tuna ile silika ya kufikiri kuwa tutaishi milele na Mama yetu Hawa ni binadamu pia. Hakuna hata mmoja wetu ambaye ni msafi wengi tumefanya makosa sana mengine ni ya sirini hayako dhahiri. Mungu ndiye anayejua mioyo yetu. CCM wako bize na wale wenye nguvu ya kuendeleza wanayoyataka hawako tayari kupoteza muda na wagonjwa au wenye shida. Mama Hawa amekwenda kwa Muumba apumzike kwa amani. Sisi tuliobaki tujiulize tunataka kutumika na kuacha taswira gani tutakapoondoka hapa duniani?
 
That is where we are going. The way is clear if you believe before the presence of God.
 
Huyu mama alimchapa viboko ndugu yangu kwa kosa la kuhuza mahindi mabichi. Yaani yeye alikua anavizia saa 4 usiku
 
Mkuu chama nimeanza kulipa na ninaendelea kulipa taratibu hadi mwaka 2015 ndio nategemea kumaliza.

Big up huo ndio uzalendo sio wengine kama jamaa yangu ndani ya JF haishi kulalama kuhusu bodi ya mikopo wakati wake halipa na vibaya zaidi uwezo anao.
Chama
Gongo la mboto DSM
 
Atakumbukwa kwa ubabe wake usio na tija ! . RIP H. Ngulume
 
Mimi namkumbuka kwa matusi huyu mama kinywa chake kilikuwa kichafu! Poleni wanafamilia na wote mlioguswa na msiba huu
 
Salaam wakuu,
Taarifa nilizozipata hivi punde ni kuwa aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni mama Hawa Ngulume amefariki dunia muda mfupi uliopita.

Mama Hawa Ngulume alikuwa akisumbuliwa na kansa kwa muda mrefu.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahali pema peponi, Amina.

Innalilah wa innalilah Rajuun.

RIP Mama.
Ulitusaidia usafi wa barabara kwa kuhakikisha malori ya mchanga yanafunikwa usichafue njia wakati unasafirishwa hapa mjini!
 
Tangulia, tunakufuata... Ulitelekezwa na chama cha magamba, .. ambacho sasa kimefanya wastani wetu wa kuishi miaka 48.... Tusipokufa kwa njaa,... tutapitia mabwepande!...
 
[h=6]Goodmorning the friend of Mine! I hope you are doing good. May you pray for FUNERAL ACTIVITIES of our beloved Mother HAWA NGULUME ( kicked the backet yesterday) which will be held tomorrow at MTINKO village -SINGIDA (rural area) from 11 a.m to 1.00pm. The VOYAGE from dar to sgd will commence at 4pm today.
R.I.P OUR MUM
NGULUME.jpg[/h]
 
Nitoe pole kwa familia ya Marehemu Mama Hawa Ngulume.
Huyu Konisaga kama nakumbuka vizuri nilikwenda kwake kusainisha "loan form" wakati huo akiwa DC Temeke alikuwa nunda kweli kweli, huo mkwara aliokuwa anatuchimba kama mtu una roho nyepesi unakimbia. Wakati huo salamu kutoka kinondoni zilikuwa zinatisha.
Sasa mkuu biti la huyo wa temeke tu lilikutisha, ungekwenda kinondoni nadhani ungeishia getini.

Nakumbuka mama alitusumbua, ikabidi tumwanzishie zengwe. Tukaenda hadi kwa makamba wakati huo akiwa mkuu wa mkoa. Makamba akatupatia barua ikimtaka mama huyo atusaidie. Tulipompa barua mama akaitupilia mbali huku akijinadi eti yeye ameteuliwa na rais na wala siyo makamba. Mama alikuwa jiwe balaa.
 
Salaam wakuu,
Taarifa nilizozipata hivi punde ni kuwa aliyewahi kuwa mkuu wa wilaya ya Kinondoni mama Hawa Ngulume amefariki dunia muda mfupi uliopita.

Mama Hawa Ngulume alikuwa akisumbuliwa na kansa kwa muda mrefu.

Mwenyezi Mungu aipumzishe roho ya marehemu mahali pema peponi, Amina.

Innalilah wa innalilah Rajuun.

R.I.P mama Hawa Ngullume,Mungu amekupenda zaidi,
 
Back
Top Bottom