Tanzania yazindua mgodi

Tanzania yazindua mgodi

kama wazungu wamecheua serikali itaweza kumeza? Ujanja ujanja wenu tutauona unapoishia kwa maana viwanda na mashirika madogomadogo yamewashinda leo mnakia kwenye mgodi? tutawasikieni muda si mrefu mnapigizana makelele
 
Huo siyo mgodi mpya, ni ule ulewa Tulawaka ambao Afeican Barrick Gold wamechimba dhahabu karibu yote, ndiyo Stamico wameachiwa mapango wakombeleze mabaki. Hahahahahaa... Watanzania fungu la kukosa!

Siyo kukombeleza tu,bali mwisho wa siku kufukia mashimo yale iwe kazi yao!
 
kama wazungu wamecheua serikali itaweza kumeza? Ujanja ujanja wenu tutauona unapoishia kwa maana viwanda na mashirika madogomadogo yamewashinda leo mnakia kwenye mgodi? tutawasikieni muda si mrefu mnapigizana makelele

Mkuu MAGAMBA KILLER tena kurun mgodi kwa Public Procurement Act,ngoja tuone
 
Kuna miradi rahisi kiasi kama kilimo nafikiri ndio ingeweza kutusaidia kwa haraka kuliko complications za migodi ambayo inahitaji hitech
 
Acha kuongea pumba, una facts za kujustfy ur nonesence?

Hivi wewe umesoma hoja kwanza kabla hujanijibu. Mimi nilidhani migodi imemilikiwa na Wabongo siku zote, nashangaa kumbe ndio umezinduliwa wa kwanza utakaomilikwa na kuwanufaisha wazawa.
 
NILIMSIKILIZA MKUU WA WILAYA LEO ASUBUH ANAZUNGUMZIA HUO MGODI ANASEMA MPAKA SAHV WAMEPATA TOFALI 2 ZA DHAHABU AMBYO NI SAWA NA 25KG KILA TOFALI AMBAYO SAWA NA 50KG YA DHAHABU,NAWAMEUZA KWA SH BILION 2.2.nilikuwa najiuliza je hzo 50kg gold ni thamani hicho kweli?au ni aina gani ya dhahabu wanachmba pale?
 
jamaa washajua wabongo wajinga wanaendeshwa kwa vitu vidogo..
mgodi moja unatatua vipi swala la ajira? kwani wanaemploy watu milioni? Mjinga tu ndo atasema wanapiga step, ajira tungeitatua kwa kufix elimu na kuondoa siasa kwenye elimu, hamna solution zaidi ya kucheza na elimu ili tupunguze idadi ya wajinga tanzania, ikikaribia kampeni miaka yote unasikia kiwango cha kufaulu kimeongezeka, miaka mingine ovyo. this ignorance unapigiwa makofi ni moja ya sababu naona bongo kweli vichwa maji wengi, prof mzima naye anaona kafanya jambo kubwa sana...
 
du!mi tatizo langu bei ya dhahabu.hivi hizo kg 50 wameuza bil.1:5 au 2:2?na wamezalisha kwa muda gani kupata hizo kg?anaejua anijibu.
 
Kumbe inawezekana!!!! Basi kuanzia sasa migodi yote nchini itayogunduliwa siku za usoni isiwe na wawekezaji toka nje. STAMICO wapewe mtaji mkubwa wa kuwawezesha kusimamia migodi hii ambayo itakuwa haina wawekezaji hata kwa asilimia 1.
 
nitajie mradi mmoja Kenya mkubwa wa uchimbaji madini ambao unamilikiwa na Wazawa Kenya! Tuanze magadi? titanium Kwale? Tsavorite? gold in Migori? FYI Tanzania ipo mbele kwenye hii sector compared to Kenya!
 
Hapo watajazana ndugu zao mpaka mseme basi.Wewe kabwela utapata maeneo ya ufagizi
 
wewe prof. ni msomi sana, haiwezekani miradi mikubwa kama hiyo iwe ya kutatua ajira tu. kwa hiyo nchi ina tatizo la ajira pekee? au ndo miradi ya kampeni? kuajiri watu tu hata kama hamna uzakishaji? nafurahi kusikia miradi kama hii inafunguliwa lakini you have to focus, broadly, what to address, ongezea basi kwamba mradi utaongeza pato la taifa, kupunguza matatizo ya afya, elimu, kisha ujenzi wa miradi mingine kutokana nao (multiplier effect).

ONYO: najua hapa kuna wafia serikali/chama watakuja kuharisha kama kawaida yao kwa sababu hawajui kuelewa kilichoandikwa, nawasubiri. cc MSALANI Lizaboni

Naona umejishtukia mapema ili kujilinda
 
Back
Top Bottom