Tanzania yashika nafasi ya 57 kwa watu wenye ukarimu duniani

kirerenya

JF-Expert Member
Aug 27, 2013
1,696
2,252
_92125882_a4139be0-0455-47bd-9093-06d836f28fab.jpg


Kenya imeorodheshwa miongoni mwa nchi 20 zenye watu wakarimu zaidi duniani. Kenya inashikilia nafasi ya 12 kwenye orodha ya takwimu za mwaka 2015 ambayo inaongozwa na Myanmar ambayo zamani ilifahamika kama Burma.

Myanmar ilishikilia nafasi hiyo pia mwaka 2015 na kwa pamoja na Marekani mwaka 2014.

Tanzania imeorodheshwa ya 57 na Uganda ya 26.

Orodha hiyo ilizingatia uwezekano wa watu kuwasaidia wageni, watu kutoa pesa za kusaidia wengine na watu kujitolea muda wao kuwasaidia wengine.

Kwenye orodha hiyo, ambayo hutayarishwa na shirika la Charities Aid Foundation, nchi ambazo raia wake waliwasaidia wageni kwa urahisi ni nchi ambazo zinakabiliwa na mizozo ya kivita.

Somalia ni ya nne kwenye orodha ya watu wanaojitolea kushiriki katika wasaidia wengine sana duniani. Orodha hiyo inaongozwa na Iraq, ikifuatwa na Libya, na nambari tatu Kuwait. Malawi ni ya sita kwenye orodha hiyo na Botswana ya saba.

Shirika hilo liliwahoji watu takriban 1,000 kutoka kila moja ya nchi 140 zilizoangaziwa.

Orodha ya jumla ya nchi kwa ukarimu mwaka 2015
Taifa Nambari
Myanmar 1
Marekani 2
Australia 3
New Zealand 4
Sri Lanka 5
Canada 6
Indonesia 7
Uingereza 8
Ireland 9
Umoja wa Milki za Kiarabu 10
Uzbekistan 11
Kenya 12
Uholanzi 13
Norway 14
Turkmenistan 15
Malta 16
Iceland 17
Bhutan 18
Kuwait 19
Denmark 20
Ujerumani 21
Malaysia 22
Switzerland 23
Finland 24
Sweden 25
Uganda 26
Mongolia 27
Singapore 28
Guatemala 29
Austria 30
Iraq 31
Ubelgiji 32
Panama 33
Kyrgyzstan 34
Cyprus 35
Jamhuri ya Dominika 36
Thailand 37
Malawi 38
Nepal 39
Slovenia 40
Saudi Arabia 41
Cyprus Kaskazini 42
Israel 43
Libya 44
Iran 45
Sierra Leone 46
Ufilipino 47
Sudan Kusini 48
Luxembourg 49
Taiwan 50
Cameroon 51
Liberia 52
Haiti 53
Botswana 54
Chile 55
Nigeria 56
Tanzania 57
Somalia 58
Uruguay 58
Kosovo 60
Afrika Kusini 61
Costa Rica 62
Zambia 63
Vietnam 64
Peru 65
Syria 66
Msumbiji 67
Brazil 68
Guinea 69
Bolivia 70
Jordan 71
Burkina Faso 72
Colombia 73
Honduras 74
Korea Kusini 75
Nicaragua 76
Ghana 77
Afghanistan 78
Spain 79
Lebanon 80
France 81
Italy 82
Argentina 83
Ethiopia 84
Congo 85
El Salvador 85
Tajikistan 87
Mauritania 88
Gabon 89
Portugal 90
India 91
Pakistan 92
Romania 93
Senegal 95
Kazakhstan 96
Ecuador 97
Cambodia 98
Mali 99
Belarus 100
Paraguay 101
Benin 102
Togo 103
Cote d'Ivoire 104
Albania 105
Ukraine 106
Mexico 107
Zimbabwe 108
Poland 109
Moldova 110
Chad 111
Misri 112
Latvia 113
Japan 114
Niger 115
Rwanda 116
Venezuela 117
Estonia 118
Macedonia 119
Georgia 120
Jamhuri ya Czech 121
Tunisia 122
Morocco 123
Lithuania 124
Slovakia 124
Urusi 126
Croatia 127
Bosnia na Herzegovina 128
Bulgaria 129
Armenia 130
Azerbaijan 131
Madagascar 132
Montenegro 133
Hungary 134
Serbia 135
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo 136
Ugiriki 137
Yemen 138
Maeneo ya Palestina 139
China 140

Chanzo: BBC Swahili
 
Nadhani tulistahili kuwa wa mwisho kwenye hiyo orodha. Imagine nchi ambayo chombo kikipata ajali "binadamu" badala ya kutoa msaada kwa waathirika wanawamalizia majeruhi ili waweze kuwapora vizuri pasi na ushahidi. Nchi ambayo binadamu akidhalilishwa hadharani badala ya kumsitiri wao hushangilia. Nchi ambayo walinda usalama wako tayari kuwapiga risasi wananchi wema ili waweze kuwapora; Ref. Kesi ya Zombe na wenzie... Nchi ya ajabu sana hii.
 
Huuu ni nadhani ni upumbavu sio utafiti watu wakarimu wanauna kila siku
Iraq
Libya
Somalia etc
Hivi kweli wakenya ni wakarimu kuliko Tz?
 
Nadhani tulistahili kuwa wa mwisho kwenye hiyo orodha. Imagine nchi ambayo chombo kikipata ajali "binadamu" badala ya kutoa msaada kwa waathirika wanawamalizia majeruhi ili waweze kuwapora vizuri pasi na ushahidi. Nchi ambayo binadamu akidhalilishwa hadharani badala ya kumsitiri wao hushangilia. Nchi ambayo walinda usalama wako tayari kuwapiga risasi wananchi wema ili waweze kuwapora; Ref. Kesi ya Zombe na wenzie... Nchi ya ajabu sana hii.

Lakini bado tuko vizuri kusaidiana sisi kwa sisi mkuu
 
Nadhani tulistahili kuwa wa mwisho kwenye hiyo orodha. Imagine nchi ambayo chombo kikipata ajali "binadamu" badala ya kutoa msaada kwa waathirika wanawamalizia majeruhi ili waweze kuwapora vizuri pasi na ushahidi. Nchi ambayo binadamu akidhalilishwa hadharani badala ya kumsitiri wao hushangilia. Nchi ambayo walinda usalama wako tayari kuwapiga risasi wananchi wema ili waweze kuwapora; Ref. Kesi ya Zombe na wenzie... Nchi ya ajabu sana hii.
Hawa ndo watz mkuu
 

Attachments

  • 1477730379738.jpg
    1477730379738.jpg
    14.1 KB · Views: 37
Licha ya kujazana ulokole kila mahala bado hali ni tete!.... Sisi ni magaidi wa uvunguni. Wanafki wa uvunguni!!!!!!!!!!!!
 
Nafasi ya 57 tumebebwa, tuwashukuru wazanzibar, wakarimu na wapole sana wale watu. Tangu Uhuru chichiem haijawahi kushinda visiwani ndo waliotupa credits. Wavumilivu sana.
 
Tangu lini Wakenya wamekuwa wakarimu hivyo wakuelekeze njia bila kukudai pesa?
 
Back
Top Bottom