DuaZaMama
JF-Expert Member
- Jun 2, 2025
- 1,882
- 4,129
Huu ni muhtasari wa athari za kiuchumi za kuzimwa kwa mtandao Tanzania siku na baada ya uchaguzi mkuu Oktoba 2025
▪︎ Nini Kilitokea?
•Tanzania ilikumbana na kuzimwa mtandao nchini kote wakati na baada ya siku ya uchaguzi mkuu kuanzia 29 Oktoba hadi 3 Novemba 2025, na intaneti ilizimwa kwa takribani siku 5-6
•Mtandao wa kijamii wa 𝕏 (zamani Twitter) umefungwa nchi nzima tangu 21 Mei 2025, huku kukiwa na upunguzwaji wa kasi ya mtandao (bandwidth throttling) kutoka kwa watoa huduma (ISPs)
▪︎ Hasara za kiuchumi
•Kwa mujibu wa Paradigm Initiative (PIN) na data kutoka NetBlocks Cost of Shutdown Tool (COST), hasara ya pamoja kutokana na kuzimwa kwa mtandao na kufungiwa kwa mtandao wa 𝕏 inazidi US$238 Milioni (takribani TZS 560 bilioni)
•Kuzimwa kwa mtandao pekee yake kunakadiriwa kugharimu takribani US$72 Milioni (takribani TZS 178 bilioni) kwa siku 5 za kuzimwa kwa mtandao - karibu US$13.8 Milioni kwa siku
•Kufungiwa kwa mtandao wa 𝕏 (the ongoing suspension of 𝕏) kulichangia hasara ya takribani US$165.8 Milioni (takribani TZS 390 bilioni) katika hasara za kiuchumi (economic losses)
▪︎ Nini kiliathirika?
•Kuzima mtandao kuliathiri sehemu kuu za uchumi wa kidijitali
•Uzalishaji na biashara katika majukwaa ya mitandaoni
•Huduma za malipo ya kifedha za kidijitali ambazo ni biashara kubwa na nyingi na watu binafsi hutegemea
•Huduma za afya na kijamii zinazotumia mifumo ya mtandao
•Minada ya kilimo na mauzo ya nje – biashara ya korosho, ilihairishwa kutokana na kukosekana kwa mtandao
▪︎ Maoni, hatua muhimu
•Makundi ya haki za kidijitali yanaeleza; kuzima mitandao kunakiuka uhuru wa kujieleza, kupata habar na haki ya maendeleo chini ya mifumo ya haki za binadamu ya kikanda
•Hatua za kisheria zimechukuliwa kupinga uhalali wa kuzima mitandao – mashauri yamefunguliwa Mahakama za ndani na nje
▪︎ Kwanini ni Muhimu?
Wachumi na watetezi wa haki wanaonya kwamba, vikwazo vya kujirudia katika matumizi ya huduma za kidijitali vinaweza;
•Kuzuia uwekezaji katika sekta ya teknolojia
•Kudhoofisha uaminifu katika masoko ya kidijitali
•kuzima ubunifu na ujasiriamali, miongoni mwa wafanyabiashara wadogo na watengeneza maudhui wanaotegemea majukwaa ya mitandao ya kijamii.
▪︎ Nini Kilitokea?
•Tanzania ilikumbana na kuzimwa mtandao nchini kote wakati na baada ya siku ya uchaguzi mkuu kuanzia 29 Oktoba hadi 3 Novemba 2025, na intaneti ilizimwa kwa takribani siku 5-6
•Mtandao wa kijamii wa 𝕏 (zamani Twitter) umefungwa nchi nzima tangu 21 Mei 2025, huku kukiwa na upunguzwaji wa kasi ya mtandao (bandwidth throttling) kutoka kwa watoa huduma (ISPs)
▪︎ Hasara za kiuchumi
•Kwa mujibu wa Paradigm Initiative (PIN) na data kutoka NetBlocks Cost of Shutdown Tool (COST), hasara ya pamoja kutokana na kuzimwa kwa mtandao na kufungiwa kwa mtandao wa 𝕏 inazidi US$238 Milioni (takribani TZS 560 bilioni)
•Kuzimwa kwa mtandao pekee yake kunakadiriwa kugharimu takribani US$72 Milioni (takribani TZS 178 bilioni) kwa siku 5 za kuzimwa kwa mtandao - karibu US$13.8 Milioni kwa siku
•Kufungiwa kwa mtandao wa 𝕏 (the ongoing suspension of 𝕏) kulichangia hasara ya takribani US$165.8 Milioni (takribani TZS 390 bilioni) katika hasara za kiuchumi (economic losses)
▪︎ Nini kiliathirika?
•Kuzima mtandao kuliathiri sehemu kuu za uchumi wa kidijitali
•Uzalishaji na biashara katika majukwaa ya mitandaoni
•Huduma za malipo ya kifedha za kidijitali ambazo ni biashara kubwa na nyingi na watu binafsi hutegemea
•Huduma za afya na kijamii zinazotumia mifumo ya mtandao
•Minada ya kilimo na mauzo ya nje – biashara ya korosho, ilihairishwa kutokana na kukosekana kwa mtandao
▪︎ Maoni, hatua muhimu
•Makundi ya haki za kidijitali yanaeleza; kuzima mitandao kunakiuka uhuru wa kujieleza, kupata habar na haki ya maendeleo chini ya mifumo ya haki za binadamu ya kikanda
•Hatua za kisheria zimechukuliwa kupinga uhalali wa kuzima mitandao – mashauri yamefunguliwa Mahakama za ndani na nje
▪︎ Kwanini ni Muhimu?
Wachumi na watetezi wa haki wanaonya kwamba, vikwazo vya kujirudia katika matumizi ya huduma za kidijitali vinaweza;
•Kuzuia uwekezaji katika sekta ya teknolojia
•Kudhoofisha uaminifu katika masoko ya kidijitali
•kuzima ubunifu na ujasiriamali, miongoni mwa wafanyabiashara wadogo na watengeneza maudhui wanaotegemea majukwaa ya mitandao ya kijamii.
