Hongera pekee iende kwa vyama vya upinzani manake mengine yote yanayopoteza amani nchi zingine na Wapinzani wa Tanzania wanafanyiwa; lakini for the sake of amani yetu, wanaamua kutumia busara ili kutoivuruga nchi!
Maalim Seif amenyang'anywa ushindi mchana kweupe lakini badala ya kuwahamasisha wafuasi wa CUF kupigania ushindi wao; ndo kwanza akawahamasisha watulie!
Ni nani asiyejua hicho ni moja ya vyanzo vya uvurugikaji wa amani Africa?
Mbowe akaitisha UKUTA na watu wakahamasika! Lakini kwa kuchelea UKUTA ungevuruga amani; Mbowe aka-call off dakika za mwisho!!
Tanzania ni moja ya nchi chache sana Africa ambako, moja ya viongozi waandamizi nchini wanaponea chupuchupu kuuawa lakini bado viongozi wakuu wanawapoza wafuasi!!
Hongereni Vyama vya Upinzani na Wafuasi wenu manake pamoja na kwamba serikali imeoonesha dalili zote za kidhalimu na kupenda damu za raia wasio na hatia; nyie kwa busara zenu mmeepusha kutoa kafara ya damu za wanadamu kwa Mazimwi yala watu!
God bless Tanzania!