CULCULUS
JF-Expert Member
- Nov 17, 2011
- 316
- 619
WAZIRI wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta amegoma kusaini mikataba ya Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) unaohusu sera za ardhi, ulinzi na mambo ya nje. Sitta ambaye anaongoza ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano wa Baraza la Mawaziri wa EAC unaofanyika Burundi, aliwaambia waandishi wa habari kuwa suala hilo wamelikataa ili lirejeshwe kwa wakuu wa nchi kwa uamuzi.
Hali hiyo ilifanya mkataba huo kusainiwa na nchi nne tu za Afrika ya Mashariki, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda hivyo kuiacha nafasi ya saini ya Tanzania kubakia wazi.
Katibu Mkuu wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki, Stragomena-Tax Bamwenda alisema jambo hilo ni nyeti, lakini akaweka bayana kuwa ujumbe wa Tanzania utapaswa kutoa taarifa kwa baraza kufafanua msimamo wao.
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Lazaro Nyalandu aliweka wazi kwamba suala la ardhi halipaswi kuwa sehemu ya EAC. Alionya kwamba kuna mazingira yanayoashiria kuwa baadhi ya wajumbe wa nchi za jumuia hiyo wamekuwa wakiangalia ardhi ya Tanzania kwa jicho la husuda.
Mbunge huyo wa Singida Kaskazini alisema Tanzania ina ardhi kubwa ambayo inawapa nafasi Watanzania kuchagua eneo la kwenda kuishi.Lakini akasisitiza kuwa ardhi hiyo lazima ibakie kwa ajili ya Watanzania na vizazi vijavyo.
Tanzania imekuwa ikilalamikiwa na baadhi ya wanachama wa Jumuia kwa msimamo wake kuhusu ardhi hivyo kukwamisha juhudi za kuimarisha EAC
Source:
Tanzania yagoma kutia saini sera ya ardhi EAC
Hali hiyo ilifanya mkataba huo kusainiwa na nchi nne tu za Afrika ya Mashariki, Kenya, Uganda, Burundi na Rwanda hivyo kuiacha nafasi ya saini ya Tanzania kubakia wazi.
Katibu Mkuu wa Baraza la Mawaziri wa Afrika Mashariki, Stragomena-Tax Bamwenda alisema jambo hilo ni nyeti, lakini akaweka bayana kuwa ujumbe wa Tanzania utapaswa kutoa taarifa kwa baraza kufafanua msimamo wao.
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki wa Tanzania, Lazaro Nyalandu aliweka wazi kwamba suala la ardhi halipaswi kuwa sehemu ya EAC. Alionya kwamba kuna mazingira yanayoashiria kuwa baadhi ya wajumbe wa nchi za jumuia hiyo wamekuwa wakiangalia ardhi ya Tanzania kwa jicho la husuda.
Mbunge huyo wa Singida Kaskazini alisema Tanzania ina ardhi kubwa ambayo inawapa nafasi Watanzania kuchagua eneo la kwenda kuishi.Lakini akasisitiza kuwa ardhi hiyo lazima ibakie kwa ajili ya Watanzania na vizazi vijavyo.
Tanzania imekuwa ikilalamikiwa na baadhi ya wanachama wa Jumuia kwa msimamo wake kuhusu ardhi hivyo kukwamisha juhudi za kuimarisha EAC
Source:
Tanzania yagoma kutia saini sera ya ardhi EAC