Tanzania ya viwanda: Another failure at first place

Tusi lipo wapi!? Je wewe ni mmoja wa MANIFESTO ile!?
Kweli tuna watz wagonjwa wewe mmoja wao, hii ni hoja na wala siyo shambulizi kwa serikali wala kwa mtu. Upo ugumu ktk utekelezaji wa sera ya viwanda, huku ukiwa huna mitaji, elimu na sera iliyo wazi kwa uwekezaji, wa ndani na huo wa nje. Hujui utauza wapi, hujui utashindana vipi, huwajui wanufaika muda utatuambia kama ni mapenzi basi wewe kwa ccm umekufa kuoza kila saa hila na matusi
 

Kwanza Unapaswa kufahamu kuwa Tanzania ya Viwanda sio Sera ya mtu mmoja isipokuwa Ni muendelezo wa MIPANGO ya serikali . Awamu ya 4 ilisimamia kilimo na baada ya kilimo kukua MIPANGO ilikuwa ni kusimamia Ukuaji wa viwanda ili Nchi iweze kuongeza thamani ya bidhaa kabla ya kuuza NJE eg MADINI au Korosho zilizopita kiwandani kuchakatwa na kuongezewa thamani bei yake kubwa NJE ya Nchi kuliko Korosho inayouzwa kama ilivyotoka shambani.
Pia VIWANDA vita ongeza ajira kwa Vijana wetu wengi. India waliweza kuweka mkazo kwenye ubunifu wa machine za viwanda vidogo na vya kati. Mafundi mchundo wa gerezani wakiendelezwa au Veta wakiendelezwa kwa kupewa exposure ya India, China AU Ujerumani wanaweza wakaja na machine modern mkashangaa. Machine za kubangulia korosho, kukamua mafuta ya Alizeti, pamba, ufuta, machine za kutengeneza Nyuzi, kusaga mazao etc. viwanda vidogo vinaweza kuleta ajira kubwa ajabu ktk kipindi kifupi cha miaka 5-10. Wakati huo huo tukiwa tunatafuta foreign direct investments za type ya kina Dangote, Trump etc kwa kuwawekea vivutio.

Serikali iwekeze kwenye elimu ya ufundi. Ipeleke Vijana China , India, Ujerumaniwakajifunze hata kozi za mwaka mmoja mmoja wale wenye ujuzi kidogo wakipata exposure wakirudi wanaweza kubadili mambo.

Malaysia ina peleka Vijana wengi sana Uk, USA, Australia, China, India kujifunza teknolojia mpya. Tusibaki tunajifungia tu humu wenyewe bila kuwa na sera ya kujenga ujuzi wa Vijana wetu Nchi zilizoendelea. Tuwe na program ya kuchagua best 100 science students tuwatawanye Nchi zilizoendelea, tuwalipie gharama za masomo na kuwasainisha mkataba kuwa wakimaliza wanarudi kuleta ujuzi na huo ujuzi uheshimiwe na tujue tunawapeleka wapi wautumie ujuzi wao kwa faida ya nchi.

ELIMU ya ufundi ni chachu ya Tanzania ya viwanda. Then unawezajua Market iko wapi. Bila ya kuwa na quality products huwezi jua soko liko wapi.


Tunanunua viatu, mikanda ya ngozi, pochi toka China. Tuna ngozi kwanini tusijenge viwanda vya kisasa vya vitu hivyo hapa nchini ambapo soko lipo. Tuna import vitanda, sofa etc Sababu quality ya vyetu Si nzuri. Tunanunua gypsum boards toka Thailand wakati tuna raw material ya gypsum kibao lakini ujuzi wetu hauwafikii wa Thailand. Vitu ni vingi mno. Tujiongeze. Kama National Development plan itasimamiwa vizuri ndani ya 5 years tutasogea.
 
Mbona viwanda vipi zaidi ya 7000 vya kufyatua matofali na washing nguo..?
 
Mnataka viwanda gani jamani.mwijage alishataja viwanda vinavyotakiwa.
 


Kwanza kabisa mleta mada mleta mada amefeli hatua ya kwanza tu. Nawewe hapo hapo ukaingia kwenye mtego wa kufeli vile vile.

Kuti cha kwanza mlichofeli wote mmeandika tungo kama hadithi ambavyo havina references zozote.
Unapoanza kueleza sera na dira za nchi ni vyema ukaziweka hapa ili kila mmoja amweze kuzisoma na kuzielewa aweze kuchangia.
Sasa unapotoa maneno matupu kutoka kichwani mwako bila references watu wenye akili timamu watajua tu kuwa wewe ni mchawi fulani una ajenda nyuma ya taarifa yako. Mtu kama GT hawezi kuongea maneno matupu tu.

Kwanza tembelea katika tovuti ya ofisi ya raisi kuhusu mipango hapa:
http://www.mipango.go.tz/
Hapa kuna mambo mengi utajifunza na kujua ili uwezekutoa duku duku lako usikilizwe ukiwa kwenye mstari.

Kisha soma hapa 5 years plan ya taifa

Vile vile unaweza kutembelea hapa
Tovuti Kuu ya Serikali: Dira 2025 Upate dira ya taifa ifikapo mwaka 2025.

Ukija kwenye upande wa sera zipo sera nyingi tu ambazo lengo lake kubwa ni maendeleo ya jamii. Kuna sera zilizotungwa mda mrefu uliopita na zipo zinazoendelea kutungwa na kuboreshwa.


Jambo ambalo limenishangaza kwako ndugu yangu ni kuhusu kuwa na kikao cha pamoja kama taifa. Hapa sijui unaongelea nini? Sijui unataka tuwe na mkutano mkuu wa nchi nzima. Sijui tutakaa wapi watu mil50.
Hujui kuwa wabunge ndio wanaowakilisha wananchi? Hujui bungeni kuna kamati mbalimbali kazi yao ni kuwa karibu na serikali katika utungaji wa sera. Ndio maana kuna wizara ya Sera na Bunge. Wizara hiyo moja ya kazi yake ni kuunganisha Bunge na serkali. Kwahiyo sera zote na utekelezaji wake wananchi wanajua kupitia wabunge wao. Ambao ni wawakilishi wao.

Halafu jambo la pili:-
Viwanda vilivyo kufa ni kutokana na sababu nyingi tu. Moja wapo ni vita baridi kati ya Nchi za kijamaa na nchi za kipepari. Ambazo nchi kubwa za USSR na Marekani ziliingia katika vita baridi. Kitendo cha kuanguka kwa dora ya kisovieti ilisababisa madhara makubwa kwenye nchi yetu. Na ikichukuliwa nchi yetu ilikuwa bado changa. Na kuna vitu vingi tu vilitokea kipindi kile bila hata ya kuhusianisha na vita ya kagera.

Kwahiyo Ile industrial revolution ya Ulaya ni ya kipindi kile hatuwezi tukaanza kulima kwanza kisha tuanzishe viwanda. Ni lazima kuvifungamanisha vyote kwa pamoja.
Ndio maana sasa Uwekezaji mkubwa katika Umeme unafanyika. Ndio maana ikaanzishwa REA kwaajiri ya kusimamia usambazaji wa umeme vijijini. Kuna mkongo mkubwa wa umeme ambao unamalizika sio mda mrefu wenye uwezo wa MV 400. Unaunganisha nchi ya Zambia Tanzania Kenya. Kiasi kwamba Tanzania inaweza kutoa au kupata umeme toka nchi za Zambia na Ethiopia.

Lile jambo la kuiweka Reli ya kati kuwa Stadard ni moja ya kufungamanisha usafirishaji na viwanda. Ujenzi wa barabara usiesme chochote kwaajiri ya usafiri. Ni mambo mengi tu
 

Attachments

Ni kweli mkuu...wengi wananunua juice ya shilingi 100 inayowekwa kwenye chupa za maji zilizotumika. Kwa kweli tunahitaji mipango na mikakati madhubuti ili kufikia kuitwa Tz ya viwanda...
 
Tz itabaki dampo la bidhaa za nchi za magharibi
 
Tz kufanikiwa ni ngumu sana mimi huwa nakwenda Zambia na kamtaji kangu ka nyanya nanunua bidhaa sample 4 nakuja nazo dukani kufila boda wananiambia unahitaji kuwa na IMPORT PERMIT masharti yake kila bidhaa unazotegemea utakuwa unaingiza upeleke 5pcs TFDA kanda waende wakale ili wajue kama ni bidhaa tam je, wamenisha nifilisike au vipi¿
 
Stimulus package muhimu, huwezi kuwa unabana matumizi, mishahara midogo halafu unataka muwekezaji aje hapa, wananchi masikini bidhaa hazitanunulika
hii ni moja ya setbacks ya hiyo dream ya Tanzania ya viwanda
I wish huyu jamaa angekuwa anafanyiwa consultation hata monthly
 
Kitulo kuna hoja imetolewa kwamba kabla ya kuuza nje ni lazima kwanza kujenga uwezo wa watanzania kwenye kununua vitu vitakavyozalishwa nchini. Lakini inaonekana kama vile kuna mpango mahsusi wa kupunguza uwezo wa watanzania kwenye kununua.
Uwezo wa kununua utachochewa na ajira katika hivyo viwanda na ongezeko la uzalishaji mali hasa kwa vijana kuanzisha ajira binafsi kama kufuga samaki na nyuki ambvyo vitapelekwa viwandani kuchakatwa.
Nia ipo pale pale kamanda Allen Kilewella
 
Jambo la kwanza kabisa ni lazima tuelewe nini maana ya Tanzania ya viwanda? Kama hatujui nini maana yake, basi kila mtu atakuwa anaongea kutokana na anavyofikiria yeye.



Kwa hiyo, kifungu (i) ndicho watu wanachokishikia bango. Kifungu hicho basically kinamaanisha kuwa kuiondoa Tanzania katika mfumo wake wa sasa wa kiuchumi (Agrarian ) na kuwa Industrialized. Lakini, kwenda kuwa industrialized, you have to pass through some stages.

Ndiyo maana, by 2025 Tanzania ina lengo la kuwa semi-industrialized country (mind you, not industrialized). By 2020 haya ndiyo malengo.





Haya malengo yakifikiwa kwa miaka mitano ijayo, siyo kwamba tutakuwa semi-industrialized Nation, tutakuwa kwenye transformation ya kuelekea kwenye semi - industrialized economy.

According to UNIDO, nchi zimekuwa categorized based on their CIP ( Competitive Industrial Perfomance Index) itafikia 0.01 Tanzania Ina 0.007. Pia ni lazima iwe out of Least Developed Nations (LDCs) yaani GDP iwe above 1045$ per capita.

Sasa baada ya kukubaliana na hayo au kurekebishana, labda niyo tunaweza kuanza kujadiliana jinsi muelekeo ulivyo. Other than that tutakuwa hatuna jinsi ya kupima tulipo na tunapoelekea.
cc. Allen Kilewella , Nguruvi3 , barafu , Eric Cartman , ycam
 

Attachments

  • upload_2016-12-12_2-55-37.png
    68.3 KB · Views: 36
Hieanda walimanisha vowanda vya maneno matupu kama hapa kazi Tu!
 
Hivyo viwanda vinatoka wapi na kwa Sera IPI...???
Tatizo uwezo wako ni mdogo. Na mwisho wa siku utakuwa pungu wani. Nenda kwenye tovuti za Serikali mipango ukajifunze na kusoma dira ya maendeleo na Sera mbalimbali. La sivyo utabaki kuwa na kichwa kikubwa bila akili.
 
Kama mfumo wa haki ungekuwepo bongo, hii serikali ilitakiwa kufikishwa mahakamani na watu waka-resign maana kwenye kampeni watu waliambiwa kwamba serikali itajenga viwanda halafu baada ya kuanza kazi waziri anasema serikali haitajenga kiwanda na kazi ya serikali ni kupiga saundi ili wawekezaji waje! Kama ndivyo basi hakukuwa na haja ya kuwadanganya wapiga kura kwa sababu awamu zote zilipiga saundi ili kuvutia wawekezaji.
 
Mtu wa kwanza kupelekwa Mahakamani ni Mtei na Mbowe.
 
upo sahihi ila ant kuelewa watakupinga kazi kutukana wenzao kuwaita nyumbu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…