Kuna movement kubwa ya chinichini naiona Tanzania. Tofauti na mwaka 2016 kuna mabadiliko makubwa matatu
1. Wananchi hawaogopi tena vyombo vya usalama kama zamani wala kesi za kubambikizwa. Na badala yake Mahakama, polisi na hata Jeshi haviheshimiki kama zamani kwasababu ya kuingizwa kwenye siasa
2. Siasa za Tanzania zimekuwa za kimataifa kuanzia Lissu apigwe risasi. Lissu kitu ambacho wengi hawajui kila tukio kubwa ana rekodi na kutuma kwenye email list ya viongozi wote Duniani ambao anajua wanapenda demokrasia. Kwa sasa kuanzia EU mpaka US kuna wabunge wanajua siasa za Tanzania sana kuliko hata Watanzania wengine
3. Umri wa Watanzania. Watanzania wengi ni watoto chini ya miaka 25 ni 75% sasa mwa miaka minne hii kuna vijana ambao walikuwa watoto miaka minne lakini sasa sio watoto tena na ni wengi sana. Sasa hawa karibu wote wapo kwenye mitandao na kwenye mitandao upinzani unafanya vizuri kueleza sera kuliko serikali. Serikali inaonekana ni ya wazee. kibaya zaidi hakuna kazi kwa vijana na wanaona maendeleo ni kama ya watu wazima pekee. Hawa vijana hawana magari ya kuendesha kwenye madaraja mapya, hawana pesa ya kupanda ndege mpya, hawaoni mbwawa, hawajui na hawajawahi kufika kwenye Mbuga. Hawa vijana hawajui umeme vijijini na wala hawaumwi sana kujua kwamba tuna zahanati. Hawa vijana wanachoona ni kwenye mitandao hakuna Mkenya mpinzani yuko jela wanaona wapinzani Tanzania wako jela. Wanaona wanasiasa wanapigwa risasi auwako mahakamani kila siku. Hii taswira sio nzuri kwa vijana.
Kitu kimoja ambacho ni sehemu ya kukua ni kuwa mpingaji lakini vijana wetu hawana sehemu zaidi ya mitandao. Hivyo navyoona hata kwenye mitandao na WhatApp groups kuna uoga uliokuwepo ambao haupo tena hata pale watu wanapojua wana rekodiwa kinyume na sheria. Kibaya ambacho serikali inafanya ni kwamba serikali inafanya vitu ambavyo ni tofauti na mila zetu. Nyumbani na jamii za kitanzania zinaongea hakuna kufungana, kupigana risasi wala kunyanyasana kwa kutofautiana kwenye mawazo pekee. Kitu kimoja tu ambacho Watanzania wote waliungana kupinga na kutaka Watanzania wenzao wafungwe ni kwenye ufisadi tu. Lakini hakuna ushahidi wowote kwamba wapinzani ni mafisadi. Sasa kijana wa kawaida anasema kama hawa sio mafisadi na wanafugwa je wanapigania nini sasa. Wakina Msigwa, Lema , Mdee wanawajibu ni demokrasia tu na hilo wanaanza kulielewa sasa. Sudan walijifunza kwa waarabu wa Tunisia hivihivi kwenye mitandao. Lakini baya zaidi viongozi wa nchi za nje siku hizi wamemulika sana Tanzania na Kenya. Kenya kwa kukuza demokrasia na sisi kwa kubomoa.
Miradi mingi ni mizuri sana lakini itachukua muda sana kuleta matunda. Plant ya gas ni miaka 20-30, treni kufika Rwanda na Congo miaka sio chini ya 10, miradi ya umeme mpaka umeme ushuke bei ni miaka 10, bomba la gas la Uganda miaka 10. Pamoja na miradi mizuri hawa vijana hawawezi kuielewa au huwezi kuwaeleza wakuunge mkono kwa miradi ambayo kwasasa hawana hata uelewa wa faida zake. Hivyo wataanza kuwa na misimamo mikali hasa kama uchaguzi usipokuwa huru
1. Wananchi hawaogopi tena vyombo vya usalama kama zamani wala kesi za kubambikizwa. Na badala yake Mahakama, polisi na hata Jeshi haviheshimiki kama zamani kwasababu ya kuingizwa kwenye siasa
2. Siasa za Tanzania zimekuwa za kimataifa kuanzia Lissu apigwe risasi. Lissu kitu ambacho wengi hawajui kila tukio kubwa ana rekodi na kutuma kwenye email list ya viongozi wote Duniani ambao anajua wanapenda demokrasia. Kwa sasa kuanzia EU mpaka US kuna wabunge wanajua siasa za Tanzania sana kuliko hata Watanzania wengine
3. Umri wa Watanzania. Watanzania wengi ni watoto chini ya miaka 25 ni 75% sasa mwa miaka minne hii kuna vijana ambao walikuwa watoto miaka minne lakini sasa sio watoto tena na ni wengi sana. Sasa hawa karibu wote wapo kwenye mitandao na kwenye mitandao upinzani unafanya vizuri kueleza sera kuliko serikali. Serikali inaonekana ni ya wazee. kibaya zaidi hakuna kazi kwa vijana na wanaona maendeleo ni kama ya watu wazima pekee. Hawa vijana hawana magari ya kuendesha kwenye madaraja mapya, hawana pesa ya kupanda ndege mpya, hawaoni mbwawa, hawajui na hawajawahi kufika kwenye Mbuga. Hawa vijana hawajui umeme vijijini na wala hawaumwi sana kujua kwamba tuna zahanati. Hawa vijana wanachoona ni kwenye mitandao hakuna Mkenya mpinzani yuko jela wanaona wapinzani Tanzania wako jela. Wanaona wanasiasa wanapigwa risasi auwako mahakamani kila siku. Hii taswira sio nzuri kwa vijana.
Kitu kimoja ambacho ni sehemu ya kukua ni kuwa mpingaji lakini vijana wetu hawana sehemu zaidi ya mitandao. Hivyo navyoona hata kwenye mitandao na WhatApp groups kuna uoga uliokuwepo ambao haupo tena hata pale watu wanapojua wana rekodiwa kinyume na sheria. Kibaya ambacho serikali inafanya ni kwamba serikali inafanya vitu ambavyo ni tofauti na mila zetu. Nyumbani na jamii za kitanzania zinaongea hakuna kufungana, kupigana risasi wala kunyanyasana kwa kutofautiana kwenye mawazo pekee. Kitu kimoja tu ambacho Watanzania wote waliungana kupinga na kutaka Watanzania wenzao wafungwe ni kwenye ufisadi tu. Lakini hakuna ushahidi wowote kwamba wapinzani ni mafisadi. Sasa kijana wa kawaida anasema kama hawa sio mafisadi na wanafugwa je wanapigania nini sasa. Wakina Msigwa, Lema , Mdee wanawajibu ni demokrasia tu na hilo wanaanza kulielewa sasa. Sudan walijifunza kwa waarabu wa Tunisia hivihivi kwenye mitandao. Lakini baya zaidi viongozi wa nchi za nje siku hizi wamemulika sana Tanzania na Kenya. Kenya kwa kukuza demokrasia na sisi kwa kubomoa.
Miradi mingi ni mizuri sana lakini itachukua muda sana kuleta matunda. Plant ya gas ni miaka 20-30, treni kufika Rwanda na Congo miaka sio chini ya 10, miradi ya umeme mpaka umeme ushuke bei ni miaka 10, bomba la gas la Uganda miaka 10. Pamoja na miradi mizuri hawa vijana hawawezi kuielewa au huwezi kuwaeleza wakuunge mkono kwa miradi ambayo kwasasa hawana hata uelewa wa faida zake. Hivyo wataanza kuwa na misimamo mikali hasa kama uchaguzi usipokuwa huru