Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 69,592
- 123,089
Nakuunga mkono mleta uzi. Ukijaribu kuangalia wale wote wanaotaja na kumsifia Magufuli kwa kiwango kikubwa ni wale aliowapa uteuzi, ama wale wote wanaotegemea kwa kujipendekeza kwao kwake atawapa nafasi ya kufanikiwa kimaisha. Wale wote wenye mapungufu katika sifa ya nafasi walizo nazo hivyo namna pekee ni kuliimba jina la kulinasibisha na kila jambo la nchi hii ili asiwazibie mlo. Mfano halisi wa huu ni rc Makonda, ukijaribu kumsikiliza anaweza kumtaja kila baada ya dk3 hata kama hana sababu ya msingi ya kufanya hivyo, kisa ni huo umiliki wa vyeti vyenye utata.
Pia rais mwenyewe ni mtu anayependa kusifiwa na kunyenyekewa, hivyo wanaomwambudu na kumtegemea kimasha wameshagundua udhaifu huu nao wanatumia udhaifu wake kama fursa. Hata hiki kilichotokea juzi kwa wanaccm kwa kushirikiana na jeshi la polisi kufanya rafu zote ni kutaka kuonyesha Magufuli anakubalika. Wapambe wake hawakuwa tayari kuuona ukweli ambao ungewaumiza. Hivyo waliamua bora heshima yao ishuke kuliko kukabiliana na ukweli ambao ungewaumiza nyoyo zao. Pia kitendo cha rais kuwa na kinga ya kutoshitakiwa kwa kiwango kikubwa imesababisha watu wadhaifu kujinyenyekeza na kujipendekeza kupita kiasi.
Pia rais mwenyewe ni mtu anayependa kusifiwa na kunyenyekewa, hivyo wanaomwambudu na kumtegemea kimasha wameshagundua udhaifu huu nao wanatumia udhaifu wake kama fursa. Hata hiki kilichotokea juzi kwa wanaccm kwa kushirikiana na jeshi la polisi kufanya rafu zote ni kutaka kuonyesha Magufuli anakubalika. Wapambe wake hawakuwa tayari kuuona ukweli ambao ungewaumiza. Hivyo waliamua bora heshima yao ishuke kuliko kukabiliana na ukweli ambao ungewaumiza nyoyo zao. Pia kitendo cha rais kuwa na kinga ya kutoshitakiwa kwa kiwango kikubwa imesababisha watu wadhaifu kujinyenyekeza na kujipendekeza kupita kiasi.