Tanzania sasa kutokuwa na ardhi?

Tanzania sasa kutokuwa na ardhi?

Ngekewa

JF-Expert Member
Joined
Jul 8, 2008
Posts
7,705
Reaction score
1,288
Ni wazi kuwa kigezo kikubwa cha nchi ni mipaka yaani mipaka inayoitenganisha hiyo nchi na majirani zake.
Katika mfumo uliopita Zanzibar ilijulikana kwa mipaka yake na Tanzania nayo ilikuwa na mipaka yake ikipakana na Uganda, Kenya,Rwanga Burundi, Msumbiji, Malawi, Congo na Zambia.
Tunataka kwenda kwenye shirikisho kutakuwa na nchi moja tu, Tanzania. Hata hivyo rasilimali na ardhi zitakuwa chini ya Serikali za Tanganyika na Zanzibar. Najiuliza hii nchi ya Tanzania eneo lake ni lipi?
 
... Hata hivyo rasilimali na ardhi zitakuwa chini ya Serikali za Tanganyika na Zanzibar. Najiuliza hii nchi ya Tanzania eneo lake ni lipi?
Ndiyo maana wanasema rais wa shirikisho kama kweli litakuwepo hatakuwa na nguvu.
 
Mimi nitafurai Kuzaliwa kwa mara ya pili kwa nchi yangu ya Tanganyika, kuwa na Ardhi kutokuwa nayo kwa Tanzania kwangu ilo sio ishu.
 
Itabidi Tanzania ikatwe pande nusu kwa nusu Muungano ukifa ,maana mkisema tufuate mipaka kabla ya Muungano hapatatosha maana Zanzibar watataka ile mipaka ya 1820 !
 
Ni wazi kuwa kigezo kikubwa cha nchi ni mipaka yaani mipaka inayoitenganisha hiyo nchi na majirani zake.
Katika mfumo uliopita Zanzibar ilijulikana kwa mipaka yake na Tanzania nayo ilikuwa na mipaka yake ikipakana na Uganda, Kenya,Rwanga Burundi, Msumbiji, Malawi, Congo na Zambia.
Tunataka kwenda kwenye shirikisho kutakuwa na nchi moja tu, Tanzania. Hata hivyo rasilimali na ardhi zitakuwa chini ya Serikali za Tanganyika na Zanzibar. Najiuliza hii nchi ya Tanzania eneo lake ni lipi?

Kwa mujibu wa rasimu ya katiba mpya "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi na Shirikisho lenye mamlaka kamili ambalo limetokana na Muungano wa nchi mbili za Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ambazo kabla ya Hati ya Makubaliano ya Muungano ya mwaka 1964, zilikuwa nchi huru."

Huwezi kuwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ni NCHI na hapohapo ni SHIRIKISHO. Kwenye mfumo wa shirikisho, Tanzania yapaswa ieleweke kuwa ni shirikisho la nchi na sio nchi. . Kama tunakwenda kwenye mfumo wa shirikisho basi Tanganyika na Zanzibar zote zinapaswa zibaki na hadhi ya ki-NCHI. Ni shirikisho la nchi mbili - shirikisho la Tanganyika na Zanzibar. Pia kwenye mfumo wa shirikisho, nchi zina mamlaka yake na shirikisho linakuwa na mamlaka yake. Shirikisho lenye mamlaka kamili maana yake ni nini?

Huwezi kuwa na mfumo wa shirikisho lakini jina likabaki lile lile - jina lapaswa kuwa SHIRIKISHO LA JAMHURI ZA TANZANIA.

(yaani shirikisho la jamhuri za Tanganyika na Zanzibar).

Kipengele hicho cha katiba kiko ki-ujanja zaidi, yaani nchi ni moja - Tanzania - na neno shirikisho limeingizwa tu kuwazuga na kuwanyamazisha watu fulani - wale wa MKATABA?. Wazanzibari changa la macho hilo!
 
Kwa mujibu wa rasimu ya katiba mpya "Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
1.-(1) Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi na Shirikisho lenye mamlaka kamili ambalo limetokana na Muungano wa nchi mbili za Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, ambazo kabla ya Hati ya Makubaliano ya Muungano ya mwaka 1964, zilikuwa nchi huru."

Huwezi kuwa na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ni NCHI na hapohapo ni SHIRIKISHO. Kwenye mfumo wa shirikisho, Tanzania yapaswa ieleweke kuwa ni shirikisho la nchi na sio nchi. . Kama tunakwenda kwenye mfumo wa shirikisho basi Tanganyika na Zanzibar zote zinapaswa zibaki na hadhi ya ki-NCHI. Ni shirikisho la nchi mbili - shirikisho la Tanganyika na Zanzibar. Pia kwenye mfumo wa shirikisho, nchi zina mamlaka yake na shirikisho linakuwa na mamlaka yake. Shirikisho lenye mamlaka kamili maana yake ni nini?

Huwezi kuwa na mfumo wa shirikisho lakini jina likabaki lile lile - jina lapaswa kuwa SHIRIKISHO LA JAMHURI ZA TANZANIA.

(yaani shirikisho la jamhuri za Tanganyika na Zanzibar).

Kipengele hicho cha katiba kiko ki-ujanja zaidi, yaani nchi ni moja - Tanzania - na neno shirikisho limeingizwa tu kuwazuga na kuwanyamazisha watu fulani - wale wa MKATABA?. Wazanzibari changa la macho hilo!

Nakubaliana nawe kabisa kuwa hii imewekwa kwa haraka ili kuwaridhisha wale wanaoogopa kuvunjika kwa muungano. Ni kipengele chenye utata lakini hili si tatizo kwa Wazanzibari.

Kwanza hii ni hatuwa kubwa kwao kwa mapambano ya kutaka kujiamulia mambo yao. Na pili ni kuwa kwao wao jambo muhimu ni uhuru wa kujiamulia mambo yao na iwapo kupatikana kwa jambo hilo kutapelekea kuvunjika kwa muungano basi haitokuwa hasara kwao kwani hadi sasa muungano haujawapa wanachotaka.
 
Mimi nitafurai Kuzaliwa kwa mara ya pili kwa nchi yangu ya Tanganyika, kuwa na Ardhi kutokuwa nayo kwa Tanzania kwangu ilo sio ishu.

Wacha ije ili kila mmoja ajitegemee, kwani si tulidai uhuru ili tujitegemee??
 
Back
Top Bottom