Tanzania ni adui wa nani na ni rafiki wa nani?

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,283
33,889
Kuna zama hadi kwenye hati za kusafiria (Passport) za Tanzania kuna baadhi ya nchi "adui" ziliwekwa kwamba mtanzania haruhusiwi kwenda huko. Ukiangalia nchi nyingi tu duniani marafiki na maadui wa nchi hizo wanafahamika. Kama nchi lazima kuwe na muongozo wa kinchi ni nani ni rafiki na ni nani ni adui.

Mwalimu na wenzake walipoanzisha (Non Alignment Movoment-NAM) hoja ya kutofungamana na upande wowote ilijengwa katika msingi ya kutochaguliwa nani awe rafiki au nani awe adui, si katika misingi ya kufungamana na nchi yoyote ile bila ya nchi hiyo tunayofungamana nayo kukidhi vigezo vinavyotakiwa ili kuwa na urafiki na Tanzania.

Wakati wa vita vya "Biafra" Tanzania iliwaunga mkono watu wa kabila la Igbo waliotaka kujitenga na Nigeria bila ya kujali "marafiki" wengine wa Tanzania walikuwa wanaunga mkono upande upi katika vita ile. Ndivyo baadaye yalipokuja masuala ya Ukombozi wa Southern Rhodesia (Zimbabwe) na hata Afrika ya kusini, msimamo wa Tanzania inamuunga nani mkono ulijulikana na kila mtu.

Hivi nchi yetu kwa sasa kwenye sera za siasa za nje rafiki wa Tanzania ni yupi na adui ni yupi? Jee kwa sasa Tanzania nchi zote za dunia hii ni marafiki zetu ama ni maadui zetu? Urafiki si ujirani wa kijografia Maana hata Kenya waliwahi kuitwa "manyang'au" zama zile baada ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kuvunjika.

Rafiki yetu ni nani na adui yetu ni nani?
 
Mkuu, hongera kwa topic na thread shirikishi...bravo! kwa bahati mbaya Tanzania ya Leo ni tofauti na ya kipindi kile cha ukombozi wa nchi za kusini mwa Africa. Tanzania ya leo haina falsafa ama dira inayo-define road map ya nchi na imebaki ikiendeshwa kama gari lisilokuwa na dereva..very sad! tumeshapoteza marafiki wote wa kweli na waliobaki ni ma-snitch tu. na ukitembea nchi tofauti utaweza kuliona hilo na liko wazi tu. Viongozi wetu nao ni vilaza waliopitiliza na hali ni mbaya kuliko maelezo. niliwahi kusikiliza speech moja ya mzee Robert Mugabe akiongea na Vijana (nafikiri ilikuwa youth summit)-alikuwa akilalamika akiuliza nini kimeikumba Tanzania? kwa bahati mbaya hiyo audio sina hapa-ila nitaendelea kuitafuta na nitakuwekea nikiipata. juzijuzi tu nimepita border ya katima Mulilo nikienda Lusaka (kwa upande wa pili wa border ya zambia-sesheke) kwa issue fulani za kazi, wenzangu wote waliokuwa na passport za RSA,NAMIBIA OR ZIMBABWE walikuwa wanapita bila kupoteza muda. jamaa alivyoniona mwanzoni alikuwa ananichangamkia (Labda alifikiri ni mtu wa huko)...nilivyotoa passport tu akaona ni ya tz aliniweka kando kwanza na kuanza kunihoji...nilijisikia vibaya sana na immigration officer aliligundua hilo! kwa ufupi, nchi yetu haina rafiki wa kweli labda kwa mbali mzee Mugabe. Inasikitisha sana...
 
Kuna zama hadi kwenye hati za kusafiria (Passport) za Tanzania kuna baadhi ya nchi "adui" ziliwekwa kwamba mtanzania haruhusiwi kwenda huko. Ukiangalia nchi nyingi tu duniani marafiki na maadui wa nchi hizo wanafahamika. Kama nchi lazima kuwe na muongozo wa kinchi ni nani ni rafiki na ni nani ni adui.

Mwalimu na wenzake walipoanzisha (Non Alignment Movoment-NAM) hoja ya kutofungamana na upande wowote ilijengwa katika msingi ya kutochaguliwa nani awe rafiki au nani awe adui, si katika misingi ya kufungamana na nchi yoyote ile bila ya nchi hiyo tunayofungamana nayo kukidhi vigezo vinavyotakiwa ili kuwa na urafiki na Tanzania.

Wakati wa vita vya "Biafra" Tanzania iliwaunga mkono watu wa kabila la Igbo waliotaka kujitenga na Nigeria bila ya kujali "marafiki" wengine wa Tanzania walikuwa wanaunga mkono upande upi katika vita ile. Ndivyo baadaye yalipokuja masuala ya Ukombozi wa Southern Rhodesia (Zimbabwe) na hata Afrika ya kusini, msimamo wa Tanzania inamuunga nani mkono ulijulikana na kila mtu.

Hivi nchi yetu kwa sasa kwenye sera za siasa za nje rafiki wa Tanzania ni yupi na adui ni yupi? Jee kwa sasa Tanzania nchi zote za dunia hii ni marafiki zetu ama ni maadui zetu? Urafiki si ujirani wa kijografia Maana hata Kenya waliwahi kuitwa "manyang'au" zama zile baada ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kuvunjika.

Rafiki yetu ni nani na adui yetu ni nani?
Hakuna uzalendo kwa sasa.Kwa hiyo unafiki kwenye vyama vya siasa,unafiki kwenye mamlaka za uteuzi na kujifanya kujua kila kitu ndio kumeharibu nchi yetu.

Ngoja waendelee na uhakiki ambao hauishi maana umempata raisi aliekua anajaribu zari!
 
Kuna zama hadi kwenye hati za kusafiria (Passport) za Tanzania kuna baadhi ya nchi "adui" ziliwekwa kwamba mtanzania haruhusiwi kwenda huko. Ukiangalia nchi nyingi tu duniani marafiki na maadui wa nchi hizo wanafahamika. Kama nchi lazima kuwe na muongozo wa kinchi ni nani ni rafiki na ni nani ni adui.

Mwalimu na wenzake walipoanzisha (Non Alignment Movoment-NAM) hoja ya kutofungamana na upande wowote ilijengwa katika msingi ya kutochaguliwa nani awe rafiki au nani awe adui, si katika misingi ya kufungamana na nchi yoyote ile bila ya nchi hiyo tunayofungamana nayo kukidhi vigezo vinavyotakiwa ili kuwa na urafiki na Tanzania.

Wakati wa vita vya "Biafra" Tanzania iliwaunga mkono watu wa kabila la Igbo waliotaka kujitenga na Nigeria bila ya kujali "marafiki" wengine wa Tanzania walikuwa wanaunga mkono upande upi katika vita ile. Ndivyo baadaye yalipokuja masuala ya Ukombozi wa Southern Rhodesia (Zimbabwe) na hata Afrika ya kusini, msimamo wa Tanzania inamuunga nani mkono ulijulikana na kila mtu.

Hivi nchi yetu kwa sasa kwenye sera za siasa za nje rafiki wa Tanzania ni yupi na adui ni yupi? Jee kwa sasa Tanzania nchi zote za dunia hii ni marafiki zetu ama ni maadui zetu? Urafiki si ujirani wa kijografia Maana hata Kenya waliwahi kuitwa "manyang'au" zama zile baada ya Jumuiya ya Afrika ya Mashariki kuvunjika.

Rafiki yetu ni nani na adui yetu ni nani?

Mijitu mingine inaturudisha nyuma miaka 50 iliyopita.
 
Nadhani kinachofanya kuwe na rafiki au adui baina ya nchi na nchi ni kutokana na mrengo wa nchi husika, mfano kipindi hicho mrengo wetu ulikua wa kijamaa so marafiki wa ukweli kabisa walikua ni wale wa kijamaa na wale mabepari hawakua maadui zetu kiivyo ila ulikua urafiki wa mashaka mashaka.

Sasahivi nchi yetu haina sera zinazoeleweka sio ujamaa au ubepari kutokana na hali hiyo kila mtu anakua rafiki yetu as long as anaweza kutusaidia(MASIKINI HAWEZI CHAGUA RAFIKI)
 
NCHI ISIYO FUNGAMANA NA UPANDE WOWOTE!
Mwenye ENZI MUNGU YUKO UPANDE WA MAMA TANZANIA IT IS TIME, BELIEVE!
 
Kwa mtu mwenye mawazo ya kibepari na kibeberu kama mimi I don't care who's our enemy and who's our friend but I care more about who's our partner...!!!

Mshirika ndo kila kitu kwangu... mshirika katika maslahi! Sio maslahi ya kutwangana bali maslahi ya kujenga uchumi!!

Remember, hata adui yako anaweza kuwa mshirika wako na kinyume chake hata ndugu yako, let alone rafiki yako anaweza asiwe mshirika wako!

The major difference is: Mshirika ambae ni adui si salama kwako kiusalama... yaani mnafanya mambo with extra cautious... huku mkidukuana! Is like mende wanapolala kitanda kimoja-- hakuna wa kulala hapo!!! Mmoja akijitikisa kidogo tu, hata kama aling'atwa na mbu, mwenzake atahoji "jombaa vp bhana... mbona hutulii!"

Kinyume chake, ndugu au rafiki hawezi kukuhujumu kiusalama lakini linapokuja suala la maslahi anaweza kukuhujumu kwa manufaa ya mshirika wake!

So, to sum up; sina shaka tuna marafiki wengi sana... Hawa ni wale ambao ndio walikuwa focus yetu kabla diplomasia haijabadilika duniani kutoka Foreign Relation to Foreign Cooperation!!

Nchi nyingi za SADC ni marafiki zetu wazuri but I don't see them anywhere near being our partners! Trust me, they can carry their guns and march ahead with their tanks and fight for us but when it comes to business, they might not do business with us....!!!

Kuhusu adui; sidhani kama tuna adui lakini kuna nchi tunatakiwa kuwa cautious nazo kutokana na leadership zao!!

Kaskazini Magharibi mwa nchi yetu tuna majirani ambao viongozi wao wana lust for power. Hawa hata kama sio maadui zetu lakini katu huwezi kuwaamini kesho watafanya nini! Hawa ni watu wanaotakiwa kudukuliwa 24/7 ingawaje kwa bahati mbaya sana ni wao ndio wenye access kubwa ya kutudukua sisi kuliko sisi kuwadukua wao!
 
Kiunafiki tu USA na washirika wake ndiyo adui zetu (ULAYA). Wakati CHINA na washirika zake ndiyo rafiki zetu,,,,,,,,,,,,,,,,,,, Ukitazama hapo utaona kwa unafiki wa TANZANIA huwa misaada mingi inatoka USA na washirika wake angalia gari zote zenye plate number nyekundu zote za misaada DFPA, DFP na mengineyo wakati wale CHINA sijaona msaada wowote na wakitoa msaada ujue lazima pembe za Tembo na Madini yasepe tena kwa UWIZI
 
Mijitu mingine inaturudisha nyuma miaka 50 iliyopita.
Dunia ndivyo ilivyo mimi sishangai. Kuna mijitu inayojua wapi dunia inaelekea na kuna watu wenye upungufu wa ufahamu. Unadhani Marekani na Iran ni marafiki, ama urafiki wa Marekani na Israel ni sawa na ule na Palestina?

Kwa nini Trump anashutumiwa kwa "kuvujisha" siri kwa Urusi. Jee unadhani hizo "siri" angekuwa kaambiwa Waziri Mkuu wa Uingereza kungekuwa kuna zogo kubwa kama hili lililopo hivi sasa? Kwa maelezo yako inaonesha ni kwa jinsi gani umetuama kwenye ugoto wa ufahamu wa mambo wa jinsi nchi zinavyoendeshwa.

Prof Negan The Dead brazoo ISIS chige na King klax nashukuru sana kwa michango yenu muruwa. Lakini kwa mtizamo wangu ili muwe "Partners" nadhani ni lazima muoneshane kwanza aina fulani hivi ya kuaminiana na kuwa na malengo yanayofanana angalau kwa nje hata kama kwa ndani kila mtu anawaza lake!

Hao washirika kwenye siasa ama uchumi ni lazima kuwe kuna kufanana kwa aina fulani kwenye baadhi ya mambo. Marekani wanafanya biashara na Uchina lakini si kama wafanyavyo na Ujerumani. Hoja mpya niliyoiona toka kwa Chinge ni hii ya kudukuana.

Kudukuana ndiyo msingi wa "urafiki" wa dunia hii. Kwanza ni lazima ufanye udukuzi kujua kama kweli rafiki yako hakusaliti na maslahi yako yanalindwa na huyo rafiki yako. Lakini udukuzi pia husaidia kujua kama kuna maslahi mapya kutoka kwake na ni nchi gani miongoni mwa nchi marafiki mnashindania hiyo fursa.

Udukuzi wa kinchi dhidi ya nchi nyingine inahitajika kuwe na sera za mambo ya nchi za nje ambazo zinaeleweka. Kwani unapofanya udukuzi kwa Mshirika wako si sawa kwa udukuzi unaoufanya kwa asiye mshirika wako. Kwa mfano Marekani ni Mshirika wa Saudia kibiashara lakini si mshirika wake wa kuaminika likija suala la mtizamo kuhusu Israel. Kwa ivo udukuzi wa Marekani kwa saudi na saudia kwa Marekani linapokuja suala kama la ISIS haufanani.
 
Kwa mtu mwenye mawazo ya kibepari na kibeberu kama mimi I don't care who's our enemy and who's our friend but I care more about who's our partner...!!!

Mshirika ndo kila kitu kwangu... mshirika katika maslahi! Sio maslahi ya kutwangana bali maslahi ya kujenga uchumi!!

Remember, hata adui yako anaweza kuwa mshirika wako na kinyume chake hata ndugu yako, let alone rafiki yako anaweza asiwe mshirika wako!

The major difference is: Mshirika ambae ni adui si salama kwako kiusalama... yaani mnafanya mambo with extra cautious... huku mkidukuana! Is like mende wanapolala kitanda kimoja-- hakuna wa kulala hapo!!! Mmoja akijitikisa kidogo tu, hata kama aling'atwa na mbu, mwenzake atahoji "jombaa vp bhana... mbona hutulii!"

Kinyume chake, ndugu au rafiki hawezi kukuhujumu kiusalama lakini linapokuja suala la maslahi anaweza kukuhujumu kwa manufaa ya mshirika wake!

So, to sum up; sina shaka tuna marafiki wengi sana... Hawa ni wale ambao ndio walikuwa focus yetu kabla diplomasia haijabadilika duniani kutoka Foreign Relation to Foreign Cooperation!!

Nchi nyingi za SADC ni marafiki zetu wazuri but I don't see them anywhere near being our partners! Trust me, they can carry their guns and march ahead with their tanks and fight for us but when it comes to business, they might not do business with us....!!!

Kuhusu adui; sidhani kama tuna adui lakini kuna nchi tunatakiwa kuwa cautious nazo kutokana na leadership zao!!

Kaskazini Magharibi mwa nchi yetu tuna majirani ambao viongozi wao wana lust for power. Hawa hata kama sio maadui zetu lakini katu huwezi kuwaamini kesho watafanya nini! Hawa ni watu wanaotakiwa kudukuliwa 24/7 ingawaje kwa bahati mbaya sana ni wao ndio wenye access kubwa ya kutudukua sisi kuliko sisi kuwadukua wao!

Mkuu, nimefurahishwa na aina yako ya uchambuzi, huku ukijaradia points kwa kejeli na nderemo...heko mkuu! kwa bahati mbaya/nzuri nimetembea karibia nchi zote za SADC na sijaona nchi mshirika na Rafiki wa kweli who can carry their guns and march ahead with their tanks and fight for us...though with exception to Zimbabwe! ndugu, ki-uhalisia Tanzania ni yatima!
 
Na bora tuendelee kubaki yatima ivyo ivyo tu kuliko Kulazimisha urafiki wa kinafiki.!! Kama undugu tunaoulazimisha na Kenya.. Ohh !! Hell NO.


Samahani lkn huwa nna karoho ka umaskini jeuri mimi
 
Mkuu, nimefurahishwa na aina yako ya uchambuzi, huku ukijaradia points kwa kejeli na nderemo...heko mkuu! kwa bahati mbaya/nzuri nimetembea karibia nchi zote za SADC na sijaona nchi mshirika na Rafiki wa kweli who can carry their guns and march ahead with their tanks and fight for us...though with exception to Zimbabwe! ndugu, ki-uhalisia Tanzania ni yatima!
Prof. Hapa nazungumzia maslahi mapana ya taifa, naichungulia Tanzania ya kesho kwenye uelekeo huu wa dunia isiyo na huruma. SHAMAC Kuna dhana dhaifu sana miongoni mwetu kwamba maskini hachagui rafiki. Lakini maskini asiyechagua rafiki ni yule tu ambaye ameshakata tamaa na kukubali hali aliyonayo kwamba ndiyo majaaliwa yake. Lakini maskini anayetaka kubadili hali yake ni lazima achague rafiki atakayejali maslahi yake ili aondokane na umaskni alio nao.

Pascal Mayalla kwenye bandiko lake moja akielezea mtizamo wake kuhusu Ujenzi wa bomba la Gesi, alishangaa mkopo tuliopewa na Benki ya EXIM ya Uchina jinsi ulivyo na masharti magumu yenye sifa zote za dhuluma. Kama nchi maslahi yetu yalilindwa kweli kwenye mkataba wa mkopo ule. Au kwa kuwa sisi ni maskini basi tunakubali kila sharti tunalopewa na "Rafiki" zetu China?
 
Back
Top Bottom