Kwa wanaoangalia hivi huyu jamaa kasimama ama amepewa kiti na kukaa...maana hapa nasikia sauti tu...
Unakuwa na uwezo wa aina gani kuweza ongea pumba mfululizo kwa masaa matatu.
NASHAURI KUWE NA MATANGAZO YA BIASHARA KULIONGEZEA PATO TAIFA!!!
JK kweli amenisikitisha. JK Kama alithubutu ku freeze Account ya Kighoma A Malima ya offshore kabla ya uchaguzi mwaka 1995 akiwa waziri wa fedha inakuwaje mafisadi wanamshinda akiwa rais?, au anataka amwachie rais wa awamu ya Tano aje kuwashitaki mafisadi wa EPA na kina Chenge, Mkapa,...,
Jamani mie mtakuwa mnanipata kwenye segment ya Mambo ya kikub.. huku kwenye politics nimechoka jamaa tuliyekuwa tunamtegemea hategemeki kweli hili ni changa la majivu tangulia baba tangulia JK
Kwangu mie naona kama amefanya kazi kubwa sana ya kuwaondolea wananchi wengi wasi wasi, na maelezo yake juu ya utekelezaji wa EPA angalau ulinipa matumaini kwamba serikali inajitahidi kufanya kazi kwa kufuata sheria ni siyo kufukuza wala kufunga watu ovyo ili kuwaridhisha waandishi wa habari na malcontents wengine.
Tehe Tehe unajua haya mambo yanatuchekesha ila kwa kweli yanapaswa kutuliza!Unajua wabunge siriasi mule walikuwa hawacheki kabisa!Hivi ulihesabu mara ngapi Muungwana aliwataja Wamarekani? Kweli twaliwa ili tule!Kwa kweli hiyo ni kauli mbiu hasa maana aliisisitiza sana kama alivyokuwa anasisitiza ili kauli mbiu ya enzi zile!Tuliwe kwa ari mpya, kasi mpya, na nguvu mpya ili tule!
Amemaliza sasa ni wakati wa kurate hiyo hutuba.
Swala la
- Zanzibar.................................. A
- Swala la Shilingi ...................... F
- Swala la kipato cha mtanzania ..... C
- Swala la wafanyakazi ................ B
- Swala la Michezo ....................... A+
- Swala la EPA ......................... F
- Swala la Rushwa ....................... F
- Kuchukulia Hatua Wezi wa mali za umma C
Kweli JMushi, ila hofu yangu ni kwamba tunakuwa vipofu wa makusudi kuhusu how change really occurs. inachukua muda. sisemi kwamba serikali yake kikwete is on point kwa kila kitu, kwa mfano hizo sekondari za kata za vodafasta kweli ni dangaya toto: bila waalimu wazuri tutavuna kizazi cha watanzania wasioajirika huko mbele ya safari kwasababu ya uduni wa elimu. Ila nadhani leo hotuba ya rais imeashiria kwamba tupende tusipende Kikwete anafanya kazi kwa mantiki, anayo system yake, na anapenda kutoa majibu kamili ya utendaji baada ya kufanya kazi badala ya kuropoka ovyo.
wapinzani wa ndani na nje ya bunge wametuzoeza hizi sera na politics za kugrand-stand. hata ninavyo wapenda wapiganaji akina chadema crew na baadhi ya wabunge wa CCM, ninawaamini zaidi watendaji ambao wanafanya mambo yao kimya na kutoa majibu kwa kufikiria kama akina Pinda (and perhaps Kikwete to some extent). Sasa nitapenda kuwaona wapinzani watakavyompaka matope knowing that it is always far easier to criticize someone who is making an attempt- kwani wao hawajapata nafasi ya kupambana na changamoto za kuendesha nchi (siyo majimba na halmashauri tu) huku wakitukanwa hadharani kila siku. tusizoee ku-underestimate kazi za serikali.
Hakika sikuyaamini masikio yangu baada ya Hotuba ndefu ya Mr President iliyochukua takribani masaa manne 4 lakini ikiwa imebeba upupu. Hotuba hii imekuja kufunikwa na Hotuba ya Bwana spika iliyochukua chini ya dakika kumi ikiwa imebeba ujumbe mzito wenye matumaini.
I dont understand what type of this president we have na sijui kama tutaweza kuvuka katika dhahama hizi. Any way sijui wana JF mnamchukuliaje Mr president wenu
Kuna umuhimu wa kupima IQ kwa wale wote wanaotaka kugombea uongozi ili Vichwa Pumba wote waenguliwe mapema.
Point ya muhimu katika hotuba ya Rais ni kuwa hakuna atayeshtakiwa katika sakata la EPA.
Kuna umuhimu wa kupima IQ kwa wale wote wanaotaka kugombea uongozi ili Vichwa Pumba wote waenguliwe mapema.
Where can I get a copy of the speech that y'all are debating about.