yamindinda
JF-Expert Member
- Jul 29, 2011
- 1,589
- 1,320
CHADEMA IMEKWAMA INAHITAJI AKILI KUBWA KUWANASUA. ACHENI MAANDIKO YATIMIE.
Na Thadei Ole Mushi.
Kwa wale wakristo wenzangu watakuwa wanamfahamu sana Mtume Paulo na barua zake ambazo zinaitwa WARAKA alizowaandikia Waefeso na Wafilipi.
Ulishawahi kujiuliza kwa nini Pulo alitumia njia hiyo kuwasiliana na Waefeso au Wafilipi? Kwa nn aliwaandikia barua? Kwa nn yale aliyoyataka kuwaeleza hakuwaeleza moja kwa moja bila kutumia barua??? Jibu ni moja tu kuwa Mazingira aliyokuwepo hakuwa na fursa ya kufanya hivyo. Ikumbukwe kuwa wakati Paulo anaandika barua hizi kwa wapendwa wake Wafilipi na Waefeso alikuwa akisubiri hukumu ya Kaisari mfalme wa ROMA kipindi hicho yaani alikuwa amefungwa.
Paulo alifanikiwa kupenyeza ujumbe wake kwa wapendwa wake kupitia kwa rafiki yake Timoteo ambaye yeye alikuwa amefungwa ila baadaye aliaachiliwa na kuwa huru. Kitendo cha Timoteo kwenda mara kwa mara kumtembelea rafiki yake Paulo gerezani kilimpa fursa Paulo kuwaandikia ujumbe wa wokovu wapendwa wake hawa.
Ninaposoma maandiko haya na hadithi hizi za kina Paulo zinanifanya niwakumbuke watu watatu waliokuwa chadema Mwigamba, Kitila na Zitto. Nakumbuka ule waraka walioundika wakiwa kifungoni kifungo cha uminyaji wa Demokrasia na kutumia media kuusambaza kama Paulo alivyomtumia Timoteo. Leo wanachadema wamegeuka wayahudi hawasikii la kuambiwa yale yote yaliyotabiriwa na manabii hawa yanatokea kwa sasa.
Kama waraka ule ulivyosema kuwa CHADEMA imekosa hoja za msingi za kusimamia na sasa wanasubiria tu CCM iwatengenezee matukio ili wapate cha kuongea nanukuu kutoka kwenye waraka wenyewe :-
“Nadriki kusema kwamba kwa sasa chama kinakwenda kwa matukio na ni bahati tu kwamba CCM inaendelea kutupatia matukio lakini CCM na serikali yake wakitunyima matukio, CHADEMA chini ya Mkt Mbowe, Katibu mkuu Slaa na Naibu Zitto utakuwa ndo mwisho wake.”
Kauli ya kinabii kwa kina mwigamba na kitila inaanza kujidhihirisha hapa kwani leo hii chadema uhai wake unategemea Hotuba za Magufuli. Magufuli asipohutubia taifa kwa mwezi mzima na Ukawa nao watakosa cha kuzungumza mwezi mzima.
Kama mtakumbuka Kipindi cha kampeni chadema ilisema CCM wamekosea kumteua Magufuli kwa kuwa si mwanasiasa na hajawahi kuwa hata mwenyekiti wa ccm wa Tawi.
Kwangu hii ilikuwa ni projection nzuri kabisa walifanya ila hawakuandaa miundombinu ya ku deal naye kama akishinda. Wao wanataka mtu ambaye si mwanasiasa afanye siasa hii mbinu wakiendelea kuitumia kwa style Hii ya Mh Magufuli Ukawa watapotea kabisa.
Huwezi kufukuza kina slaa, zitto, kitila na Mwigamba halafu utegemee akili za kina Sugu na Lema wa Arusha. Chadema inapaswa ijifanyie tathmini yenyewe wajaribu kuweka opinion poll waangalie wamepoteza wapenzi wangapi. Na hili ni gap kwa watu wa research kutuambia kama uchaguzi ungefanyika leo nani angeshinda.
[HASHTAG]#KINACHOTOKEA[/HASHTAG] KWA SASA AMBACHO HAKIONEKANI.
1. Vyombo vya habari ikiwa ni magazeti, television na radio zimepunguza kwa asilimia 70 kuripoti habari zinazohudu Chadema ikilinganishwa na kipindi cha January 2014 -October 2015.
2. Mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na social media zote na vijiweni vijana wa Chadema kwa aslimia 90 wamekosa hoja na wanatukana matusi makubwa sana. Kama Malisa au Yericko hataandika kitu kupinga yanayofanywa na CCM basi watabaki kutukana hata kwa mambo ya msingi. Unapokosa vijana ambao wanaweza kujenga hoja kwenye hizi social media ni umeruhusu watu kupenyeza propaganda.
3. Uungwaji mkono toka makundi mengine nao umepungua. Makundi haya ni yale ya taasisi za kidini kama wachungaji, Mashekhe, na taasisi za elimu ya juu.
Makundi haya kila moja yameonekana kuunga mkono juhudi za serikali ya CCM kuliko maigizo ya Chadema.
4. Wanaoondoka Chadema ni wale wenye akili tu wanawaacha hawa vijana wanaotukana, vijana ambao hawana uwezo wa kutoa hata mkakati mmoja wa kukisaidia chama hii ni hatari kubwa sana kwa uhai wa Chama.
5. Kitendo cha Chadema kuanza kujiondoa kwenye chaguzi ni kiashiria tosha kuwa kinaanza kupoteza Uhai.
Kwa akili hizi za Kina Lema za kuota ndoto na kufanya mazishi ya mbwa kitaifa kazi mnayo sana.
Ole Mushi
Na Thadei Ole Mushi.
Kwa wale wakristo wenzangu watakuwa wanamfahamu sana Mtume Paulo na barua zake ambazo zinaitwa WARAKA alizowaandikia Waefeso na Wafilipi.
Ulishawahi kujiuliza kwa nini Pulo alitumia njia hiyo kuwasiliana na Waefeso au Wafilipi? Kwa nn aliwaandikia barua? Kwa nn yale aliyoyataka kuwaeleza hakuwaeleza moja kwa moja bila kutumia barua??? Jibu ni moja tu kuwa Mazingira aliyokuwepo hakuwa na fursa ya kufanya hivyo. Ikumbukwe kuwa wakati Paulo anaandika barua hizi kwa wapendwa wake Wafilipi na Waefeso alikuwa akisubiri hukumu ya Kaisari mfalme wa ROMA kipindi hicho yaani alikuwa amefungwa.
Paulo alifanikiwa kupenyeza ujumbe wake kwa wapendwa wake kupitia kwa rafiki yake Timoteo ambaye yeye alikuwa amefungwa ila baadaye aliaachiliwa na kuwa huru. Kitendo cha Timoteo kwenda mara kwa mara kumtembelea rafiki yake Paulo gerezani kilimpa fursa Paulo kuwaandikia ujumbe wa wokovu wapendwa wake hawa.
Ninaposoma maandiko haya na hadithi hizi za kina Paulo zinanifanya niwakumbuke watu watatu waliokuwa chadema Mwigamba, Kitila na Zitto. Nakumbuka ule waraka walioundika wakiwa kifungoni kifungo cha uminyaji wa Demokrasia na kutumia media kuusambaza kama Paulo alivyomtumia Timoteo. Leo wanachadema wamegeuka wayahudi hawasikii la kuambiwa yale yote yaliyotabiriwa na manabii hawa yanatokea kwa sasa.
Kama waraka ule ulivyosema kuwa CHADEMA imekosa hoja za msingi za kusimamia na sasa wanasubiria tu CCM iwatengenezee matukio ili wapate cha kuongea nanukuu kutoka kwenye waraka wenyewe :-
“Nadriki kusema kwamba kwa sasa chama kinakwenda kwa matukio na ni bahati tu kwamba CCM inaendelea kutupatia matukio lakini CCM na serikali yake wakitunyima matukio, CHADEMA chini ya Mkt Mbowe, Katibu mkuu Slaa na Naibu Zitto utakuwa ndo mwisho wake.”
Kauli ya kinabii kwa kina mwigamba na kitila inaanza kujidhihirisha hapa kwani leo hii chadema uhai wake unategemea Hotuba za Magufuli. Magufuli asipohutubia taifa kwa mwezi mzima na Ukawa nao watakosa cha kuzungumza mwezi mzima.
Kama mtakumbuka Kipindi cha kampeni chadema ilisema CCM wamekosea kumteua Magufuli kwa kuwa si mwanasiasa na hajawahi kuwa hata mwenyekiti wa ccm wa Tawi.
Kwangu hii ilikuwa ni projection nzuri kabisa walifanya ila hawakuandaa miundombinu ya ku deal naye kama akishinda. Wao wanataka mtu ambaye si mwanasiasa afanye siasa hii mbinu wakiendelea kuitumia kwa style Hii ya Mh Magufuli Ukawa watapotea kabisa.
Huwezi kufukuza kina slaa, zitto, kitila na Mwigamba halafu utegemee akili za kina Sugu na Lema wa Arusha. Chadema inapaswa ijifanyie tathmini yenyewe wajaribu kuweka opinion poll waangalie wamepoteza wapenzi wangapi. Na hili ni gap kwa watu wa research kutuambia kama uchaguzi ungefanyika leo nani angeshinda.
[HASHTAG]#KINACHOTOKEA[/HASHTAG] KWA SASA AMBACHO HAKIONEKANI.
1. Vyombo vya habari ikiwa ni magazeti, television na radio zimepunguza kwa asilimia 70 kuripoti habari zinazohudu Chadema ikilinganishwa na kipindi cha January 2014 -October 2015.
2. Mitandao ya kijamii ikiwa ni pamoja na social media zote na vijiweni vijana wa Chadema kwa aslimia 90 wamekosa hoja na wanatukana matusi makubwa sana. Kama Malisa au Yericko hataandika kitu kupinga yanayofanywa na CCM basi watabaki kutukana hata kwa mambo ya msingi. Unapokosa vijana ambao wanaweza kujenga hoja kwenye hizi social media ni umeruhusu watu kupenyeza propaganda.
3. Uungwaji mkono toka makundi mengine nao umepungua. Makundi haya ni yale ya taasisi za kidini kama wachungaji, Mashekhe, na taasisi za elimu ya juu.
Makundi haya kila moja yameonekana kuunga mkono juhudi za serikali ya CCM kuliko maigizo ya Chadema.
4. Wanaoondoka Chadema ni wale wenye akili tu wanawaacha hawa vijana wanaotukana, vijana ambao hawana uwezo wa kutoa hata mkakati mmoja wa kukisaidia chama hii ni hatari kubwa sana kwa uhai wa Chama.
5. Kitendo cha Chadema kuanza kujiondoa kwenye chaguzi ni kiashiria tosha kuwa kinaanza kupoteza Uhai.
Kwa akili hizi za Kina Lema za kuota ndoto na kufanya mazishi ya mbwa kitaifa kazi mnayo sana.
Ole Mushi