Tangia uongozi wa awamu ya tano uingine madarakani; mengi yameanza kuonekana kuhusu uhalisia wa upinzani wa taifa hili. Upinzani katika inch hii umekosa muelekeo ya nini wanakitaka na kukisimamia. Hoja za msingi wananchi walizozitarajia kutoka kwao zimeyeyuka.
Hususani hoja ya kupiga vita rushwa na ufisadi, kutowajibika na uzembe kwa serikali na mengineyo. Wananchi wanataka kuona upinzani uliosimama kwa kupigania haki zao na kujenga hoja za maendeleo ya taifa hili.
Wananchi wanataka rasilimali za taifa hili zisaidie kunufaisha taifa hili sio kuibiwa na wageni. Wapinzani wamekuwa na utamaduni wa kukosoa kauli za rais na watendaji wake bila kuja na hoja mbadala. Kiufupi upinzani katika taifa hili umekuwa hauna dira wala muelekeo wa nini hasa wanaona mbadala katika kuleta maendeleo ya taifa hili.
Kuna hoja wanasimamia kusema ccm imeongoza miaka 50 lakini hakuna maendeleo. Hivi hawa jamaaa wanaelewa tumetoka wapi. Mi niwakumbushe kidogo tu; miaka ya 1970's usafiri ulikuwaje Tanzania. Ulikuwa unasafiri siku ngapi kutoka Dar hadi Songea ama Arusha.
Pili; idadi ya wasomi walikuwa wangapi na sasa wako wangapi; vipi kuhusu maendeleo ya miji na mikoa ilikuwaje kulinganisha na sasa (najua kuna watu humu wanapicha ya Dar es Salaam miaka ya 1970's, maybe wakiwawekea mtaweza kuelewa tuliko toka). Vipi kuhusu upatikanaji wa nishati ya maji na umeme ilikuwaje ukilinganisha na sasa.
Kama hoja ni hii, swali ni kwamba upinzani unaleta hoja ipi mbadala ya kupaisha taifa hili katika maendeleo ya haraka kiasi wanachoota wao? Ili upinzani wa Tanzania usionekane kanjaja naomba wadau mtuambie tu; ni vitu gani mtakavyoleta kwa muda mfupi tufikie hayo maendeleo mnayosema ccm imeyashindwa kwa muda wa miaka hamsini?
Naomba kuwasilisha.