Mlenge
R I P
- Oct 31, 2006
- 2,125
- 2,291
Wakati wa Nyerere Tanzania ilikuwa ikifuata, au tuseme ilitangaza rasmi kufuata, Siasa ya Ujamaa na Kujitegemea. Mafanikio au kushindwa kufanikiwa kwa siasa hiyo ni jambo la mjadala. Lakini je, kwa sasa Tanzania inafuata siasa ipi? Bayana hakuna falsafa fulani inayoliongoza taifa. Ujamaa na kujitegemea? Huo unaonekana kupitwa na wakati. Hata Redio Tanzania Dar es Salaam kwa majina iliyonayo sasa imeacha kuweka ngonjera na mashairi ya kusifia ujamaa na kuwananga mabepari. Ubepari ni Unyama! ndio iliyokuwa kibwagizo cha miaka ile. Sasa hivi lakini hakuna pia vibwagizo vya kuusifia ubepari. Lipo ombwe la falsafa ya kitaifa.
Ilhali zipo falsafa nyingi ambazo taifa linaweza kuzichagua kuzifuata, siasa za uhurukweli, liberty, ndizo ambazo zinaweza kufanya nchi hii ipige hatua kubwa za maendeleo.
Kimsingi, uhurukweli unataka yafuatayo:
Kama Mheshimiwa Rais Magufuli akiichukua falsafa hii, atakuwa amejenga msingi muhimu ambao utalifanya taifa hili liwe na nguvu kubwa, lenye wananchi wanaoneemeka na taifa lao, na yeye kukumbukwa kama Founder of Modern Tanzania hata miaka hamsini ijayo. Isije kuandikwa kwenye vitabu vya historia namna hii:
1964-1985 JK Nyerere
1995-2005 BM Mkapa
2005-2015 JK Kikwete
2015-2025 JP Magufuli
2025-2035 Rais Fulani
2035-2045 Rais Mwingine
2045-2055 Rais Mwinginewe
2055-2065 Rais Mwinginewe Tena
Falsafa hii pia itamsaidia kupunguza changamoto nyingi ambazo zinatokea sasa hivi shauri ya ombwe la siasa inayofuatwa.
Ilhali zipo falsafa nyingi ambazo taifa linaweza kuzichagua kuzifuata, siasa za uhurukweli, liberty, ndizo ambazo zinaweza kufanya nchi hii ipige hatua kubwa za maendeleo.
Kimsingi, uhurukweli unataka yafuatayo:
- Haki ya mtu binafsi kujiamulia mambo yake mwenyewe.
- Serikali iliyoachia nguvu ya soko kutoa ufumbuzi kwa mambo anuai.
- Kuwepo kwa mfumo imara wa sarafu isiyoweza kubadilishwa thamani na kitu chochote.
Kama Mheshimiwa Rais Magufuli akiichukua falsafa hii, atakuwa amejenga msingi muhimu ambao utalifanya taifa hili liwe na nguvu kubwa, lenye wananchi wanaoneemeka na taifa lao, na yeye kukumbukwa kama Founder of Modern Tanzania hata miaka hamsini ijayo. Isije kuandikwa kwenye vitabu vya historia namna hii:
1964-1985 JK Nyerere
1995-2005 BM Mkapa
2005-2015 JK Kikwete
2015-2025 JP Magufuli
2025-2035 Rais Fulani
2035-2045 Rais Mwingine
2045-2055 Rais Mwinginewe
2055-2065 Rais Mwinginewe Tena
Falsafa hii pia itamsaidia kupunguza changamoto nyingi ambazo zinatokea sasa hivi shauri ya ombwe la siasa inayofuatwa.