...kodi hii itahamishiwa kwenye bidhaa za nje au kwa wafanyakazi?nahisi kodi ya kichwa inarudi tena.
.....Nadhani hii ni kwa wageni tu ambao watakuwa wamenunua bidhaa mbali mbali nchini. Pale Airport kawa wataweza kutimiza masharti yote ya kuweza kurudishiwa VAT waliyolipa wakati wakinunua bidhaa hizo, basi watarudishiwa.
.....Nadhani hii ni kwa wageni tu ambao watakuwa wamenunua bidhaa mbali mbali nchini. Pale Airport kama wataweza kutimiza masharti yote ya kuweza kurudishiwa VAT waliyolipa wakati wakinunua bidhaa hizo, basi watarudishiwa.
vat exemption kwa bidhaa za kitanzania tu.wasiwasi wangu haya mapato yatatoka wapi?je kodi hii itahamishiwa kwenye bidhaa za nje au kwa wafanyakazi?nahisi kodi ya kichwa inarudi tena.
Kiongozi inaonekana umefanya haraka kupost hii kitu.
VAT exemption kwa bidhaa zote au zile zinazalishwa Tanzania tu?
Kwa akili ya haraka wasipotoza VAT kwenye bidhaa zote serikali itapata wapi fedha?
Tia nyama kwenye post yako
Kwa kanuni za uchumi hii wanayofanya kufuta VAT kwa bidhaa za ndani ni moja ya njia za kuwapunguzia wananchi gharama za maisha. lakini wasi wasi wangu ni kuwa kutokana na udhaifu wa ukusanyaji wa mapato na kutokuwa waangalifu katika matumizi, kitakachofanyika hapa ni kusamehe upande mmoja na kuwaongezea mzigo wengine i.e wafanyakazi through PAYE. Hapo sidhani kama serikali itakuwa imetatua tatizo hili kwa sababu hao hao unaowapunguzia VAT kwenye bidhaa, ndio hao hao unawaongezea mzigo wa kodi. yaani ni sawa na kutoa kwa mkono wa kulia na kuchukua kwa mkono wa kushoto.vat exemption kwa bidhaa za kitanzania tu.wasiwasi wangu haya mapato yatatoka wapi?je kodi hii itahamishiwa kwenye bidhaa za nje au kwa wafanyakazi?nahisi kodi ya kichwa inarudi tena.
.....Nadhani hii ni kwa wageni tu ambao watakuwa wamenunua bidhaa mbali mbali nchini. Pale Airport kama wataweza kutimiza masharti yote ya kuweza kurudishiwa VAT waliyolipa wakati wakinunua bidhaa hizo, basi watarudishiwa. Mie uamuzi huu umenishangaza sana hasa ukitilia maanani hali mbaya ya kifedha ndani ya hii Serikali.
Kuanzia Januari mwakani, kodi ya ongezeko la thamani almaarufu VAT itaacha kutozwa kabisa na Mamlaka ya Mapato Tanzania, TRA.
Sosi: Magazetini, RFA.
TRA kuwarejeshea Vat kwa wageni
James Magai
MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imekamilisha mchakato wa urejeshaji wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kwa wageni wanaonunua bidhaa mbalimbali nchini kwa ajili ya matumizi, nje ya nchi.Mkurugenzi wa Fedha katika mamlaka hiyo, Saleh Mshoro, aliwaambia waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam kuwa utaratibu huo utaanza Januari mosi makani.
Alisema hatua hiyo ni utekelezaji wa Sheria ya VAT 1997 sura ya 148, kama ilivyorekebishwa mwaka 2011.
Mkurugenzi huyo alisema huko nyuma, raia wa kigeni walikuwa wanakatwa Vat kwa bidhaa walizozinunua nchini na kwenda kuzitumia katika nchi zao.
Alisema hata hivyo kwa mujibu wa marekebisho hayo, wageni hao sasa watakuwa wakirejeshewa fedha walizokatwa kulipia Vat wakati wakinunua bidhaa hizo.
Mshoro alisema ingawa utaratibu huo hautakuwa na faida ya moja kwa moja kwa Serikali lakini pia haikuwa halali kutoza tozo hilo hasa ikizingatiwa kuwa Vat inatokana na matumizi ya bidhaa husika.Utaratibu huu umekuwa ukitumika katika sehemu mbalimbali duniani kutokana na ukweli kuwa Vat ni kodi inayotokana na matumizi ya bidhaa. Hata hivyo bidhaa zilizotozwa Vat kwa watu hao hazitumika humu nchini na badala yake zilikwenda nje ya nchi na kwa hiyo si vema kutoza Vat, alisisitiza.
Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo wa fedha, wanaostahili kudai marejesho haya ni wasafiri ambao si raia wa Tanzania wanaosafiri kwenda nje ya nchi akiwa na bidhaa walizonunua Tanzania Bara kwa rejareja na kuilipia Vat.
Hata hivyo Mshoro alisema bidhaa ambazo zitastahili kurejeshewa Vat ni zile zenye thamani isiyokuwa chini ya Sh400,000 na kwamba utaratibu huo utaambatana na masharti.
Alitaja masharti hayo kuwa ni pamoja na marejesho hayo kufanyika katika Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Julius Kambarage Nyerere (JKNI) wa jijini Dar es Salaam na Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Kilimanjaro (KIA).
Alisema marejesho hayo yatafanywa kupitia kwa wakala aliyeteuliwa kwa ushirikiano wa TRA na Benki ya Twiga Bancorp, ambayo itakuwa na ofisi katika viwanja hivyo.
Aliyataja masharti mengine kuwa ni muombaji kuwa risiti ambayo imetolewa na mashine ya kielektroniki (EFDs), ili kuthibitisha madai yake na kwamba risiti hiyo lazika ionyeshe maelezo ya bidhaa. Madai kwa ajili ya marerjesho yanatakiwa yatolewe kabla ya miezi sita tangu risiti ilipotolewa na bidhaa husika zilizoponunuliwa, ziwe hazijatumika na kama zimewekwa kwenye makasha, lakiri iwe haijavunjwa, alisema Mshoro.
Lakini pia msafiri lazima awe na hati ya kusafiria, tiketi, na hati ya kuruhusiwa kupanda ndege (Board Pass). Nyaraka hizo pamoja na bidhaa husika zitahakikiwa na maofisa wa Mamlaka ya Mapato na mawakala, alifafanua Mshoro.
Kwa upande wake Naibu Kamishna wa Kodi za Ndani, Christine Shekidele alisema manufaa ya kutumia risiti za EFDs kuhakikisha kuwa kodi inayostahili kukusanywa inakusanywa na hivyo kuongeza mapato ya Serikali.
Hata hivyo alitoa wito kwa wafanyabiashara waliojiandikisha katika mfumo wa risiti hizo kuwa waaminifu katika kutoa risiti hizo.