Tanzania inaweza kufanya nini kukabiliana na pigo la wafadhili?

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Watanzania lazima tukubali kuwa hatua ya wafadhili ni pigo kwa nchi yetu. ni lazima tuchague njia sahihi ya kutufikisha tunakokwenda.

kwa mtizamo wangu yapo mambo serikali yetu inaweza kufanya.

1. kutunishiana misuli na wafadhili hakutatusaidia bali kushuka chini na kutambua kuwa yapo mambo wanazungumza yanakuwa na mantiki. serikali ya awamu ya tano imeonyesha nia ya dhati katika kusimamia haki na yapo mambo yamefanyika huko nyuma hawawezi kubadilisha lakini wanachoweza kufanya ni kuwaonyesha wafadhili hawa kuwa tunasikitika kwa kukosa ufadhili wao na mabadiliko ambayo serikali hii imeyalenga hayawezi kuja kwa mara moja bali jamii itabadilika taratibu. hapa suluhisho ni serikali kuanzisha mchakato wa katiba mpya unaojumuisha wataalamu ni kuweka misingi ya taifa iliyo imara lakini ambayo haitaonyesha kupendezesha kundi fulani la siasa.

2. upo uwezekano kuwa mbali na matatizo yetu ya ndani lakini diplomasia yetu kimataifa inaweza kuwa inalega na ndio chimbuko la mtikisiko mkubwa. raisi anatakiwa kuangalia timu yake ya washauri pamoja na timu inayojihusisha na diplomasia ya kimataifa ili kuona kama kunahitajika overhauling.

3. kusitishwa kwa ufadhili ni pigo kubwa sana katika bajeti yetu. hapa hakuna mjadala ni lazima bajeti ya serikali ifumuliwe na kuweka vipaumbele vipya ili kulinda uchumi wetu. lazima tutambue kuwa misaada hii ilikuwa ni source kubwa ya foreign currency. tukijidai kukusanya kodi na kutekeleza bajeti tuliyokuwa nayo ni wazi tutakumbana na mporomoko mkubwa sana kwa shilingi yetu kushuka thamani.

je wewe kama mtanzania unadhani ni kitu gani kifanyike?
 
watu wengi wanadai tanzania inaweza kujitegemea kwa kuangalia kodi za ndani! hapa tunaomba wachumi mtujuze maana kwa uelewa wangu foreign currency zinatupa uwezo wa kununua bidhaa na huduma nje. hivyo kama tunataka kujitegemea tunapoongelea wahisani kuondoa misaada yao lazima tuongelee tunajenga vipi uwezo wa kupata foreign currency kuziba pengo linalowekwa na wahisani kujiondoa.

lakini tukitaka kuondoa pengo hilo kwa kodi za ndani maana yake ni lazima tuhakikishe mzani wa uwezo wetu wa foreign currency na mahitaji yetu ya foreign currency yanabaki kwenye uwiano sawa au uwezo uko juu ya mahitaji.

la sivyo tutajikuta tuna matumizi makubwa huku huku tukiwa na uwezo kidogo na matokeo yake ni shilingi yetu kuporomoka.

kuangalia kodi tu bila mbinu za kuwekea mzani sawa utatupeleka kwenye hali kama ya zimbabwe ya shilingi kuporomoka.
 
Wengi wanaangalia maamuzi ya wafadhili kuondoa misaada kama kitendo kibaya lakini ukikiangalia kwa upande mwingine yawezekana huu ukawa msaada kwa watanzania.

tunazungumza sana kujitegemea, tunazungumza sana kwa nini hatuzalishi, tunazungumza sana kutengeneza ajira lakini yawezekana haya tunazungumza bila mikakati halisi ya kutekeleza tunachokizungumza.

hawa jamaa kimsingi yawezekana wanatamani tujitegemee hivyo kutuondolea misaada ni njia moja wapo wa kutulazimisha kutekeleza yale tuliyokuwa tukiyazungumza.

hapa tuna njia mbili na ni lazima kuchagua njia ya kufuata.

kimsingi uwezo wetu wa kununua bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi yetu utapungua kutokana na msimamo huu wa wafadhili.

njia ya kwanza ni ama kuendelea kutumbua maisha kwa staili tuliyonayo ambayo itasabisha shilingi kuporomoka na kuturudisha nyuma kwa nguvu au

njia ya pili ni kupunguza huduma na bidhaa kutoka nje kwa vitendo sasa ukiwa ndio msingi wa kujenga nidhamu katika matumizi ya fedha zetu za kigeni na kulinda uchumi wetu.

iwapo tutaitumia nafasi hii kwa uangalifu kwa kuchagua njia sahihi yawezekana kipindi kifupi kijacho tutakuwa tumeingia katika desturi ya kudhibiti uchumi wetu.
 
watu wengi wanadai tanzania inaweza kujitegemea kwa kuangalia kodi za ndani! hapa tunaomba wachumi mtujuze maana kwa uelewa wangu foreign currency zinatupa uwezo wa kununua bidhaa na huduma nje. hivyo kama tunataka kujitegemea tunapoongelea wahisani kuondoa misaada yao lazima tuongelee tunajenga vipi uwezo wa kupata foreign currency kuziba pengo linalowekwa na wahisani kujiondoa.

lakini tukitaka kuondoa pengo hilo kwa kodi za ndani maana yake ni lazima tuhakikishe mzani wa uwezo wetu wa foreign currency na mahitaji yetu ya foreign currency yanabaki kwenye uwiano sawa au uwezo uko juu ya mahitaji.

la sivyo tutajikuta tuna matumizi makubwa huku huku tukiwa na uwezo kidogo na matokeo yake ni shilingi yetu kuporomoka.

kuangalia kodi tu bila mbinu za kuwekea mzani sawa utatupeleka kwenye hali kama ya zimbabwe ya shilingi kuporomoka.
Lete mpango kazi wa kujipatia hizo foreign currency.
Na si kutegmea za kupewa na wafadhili.
Tuna raslimali nyingi, hebu ainisha, tuzitumie vipi kupata hizo foreign currency 's.
Na si za kutegmea kupewa.
 
Pigo wewe ndio unaliona ss wengine hilo hatulijui , tunakula na kushiba mengine ni nyongeza tu. Majipu ndiyo yanaumia maana yanakosa tenda kwenye pesa za MCC.
Lowassa na Mbowe ndio wamepeleka fitina
 
Wengi wanaangalia maamuzi ya wafadhili kuondoa misaada kama kitendo kibaya lakini ukikiangalia kwa upande mwingine yawezekana huu ukawa msaada kwa watanzania.

tunazungumza sana kujitegemea, tunazungumza sana kwa nini hatuzalishi, tunazungumza sana kutengeneza ajira lakini yawezekana haya tunazungumza bila mikakati halisi ya kutekeleza tunachokizungumza.

hawa jamaa kimsingi yawezekana wanatamani tujitegemee hivyo kutuondolea misaada ni njia moja wapo wa kutulazimisha kutekeleza yale tuliyokuwa tukiyazungumza.

hapa tuna njia mbili na ni lazima kuchagua njia ya kufuata.

kimsingi uwezo wetu wa kununua bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi yetu utapungua kutokana na msimamo huu wa wafadhili.

njia ya kwanza ni ama kuendelea kutumbua maisha kwa staili tuliyonayo ambayo itasabisha shilingi kuporomoka na kuturudisha nyuma kwa nguvu au

njia ya pili ni kupunguza huduma na bidhaa kutoka nje kwa vitendo sasa ukiwa ndio msingi wa kujenga nidhamu katika matumizi ya fedha zetu za kigeni na kulinda uchumi wetu.

iwapo tutaitumia nafasi hii kwa uangalifu kwa kuchagua njia sahihi yawezekana kipindi kifupi kijacho tutakuwa tumeingia katika desturi ya kudhibiti uchumi wetu.
Unaweza kujijenga kiuchumi huku hauna viwanda vya kuzalisha bidhaa ambazo unaweza kuuza nchi za nje? Hapa tunachofanya ni kujifariji tu lakini kiuhalisia CCM hawapo kwa ajili ya kuhakikisha nchi inaendelea zaidi wanaangalia matumbo yao na lichama lao.
 
Ushauri wangu kwa Magufuli ni ule ule, atekeleze wazo lake la kuwapeleka JKT 'special' vijana wote wasio na ajira wakazalishe na kufuga. Baada ya miezi sita tutalisha Afrika na Asia yote. Fedha za kigeni tutapata tu.
 
Mbona mnatuchanganya! Habari kutoka Lumumba kwa Lizaboni, YEHODAYA zinasema Marekani na EU walituma maombi ya mkopo Serikalini. Baada ya kukataliwa ndio wakaanza vituko vyao alimradi waifitinishe nchi na mataifa mengine ya dunia. Wazungu sio watu wazuri sana.
 
Nakubaliana na wote wanaosema tumeumia kwa wafadhili waliopunguza misaada. Kama tunaamini uwezo wa akili zetu ni maumivu ya muda tu.Tuishi kiuhalisia,tupange mipango yetu wenyewe, tuamue kujitegemea kwa kumaanisha.
 
Watanzania lazima tukubali kuwa hatua ya wafadhili ni pigo kwa nchi yetu. ni lazima tuchague njia sahihi ya kutufikisha tunakokwenda.

kwa mtizamo wangu yapo mambo serikali yetu inaweza kufanya.

1. kutunishiana misuli na wafadhili hakutatusaidia bali kushuka chini na kutambua kuwa yapo mambo wanazungumza yanakuwa na mantiki. serikali ya awamu ya tano imeonyesha nia ya dhati katika kusimamia haki na yapo mambo yamefanyika huko nyuma hawawezi kubadilisha lakini wanachoweza kufanya ni kuwaonyesha wafadhili hawa kuwa tunasikitika kwa kukosa ufadhili wao na mabadiliko ambayo serikali hii imeyalenga hayawezi kuja kwa mara moja bali jamii itabadilika taratibu. hapa suluhisho ni serikali kuanzisha mchakato wa katiba mpya unaojumuisha wataalamu ni kuweka misingi ya taifa iliyo imara lakini ambayo haitaonyesha kupendezesha kundi fulani la siasa.

2. upo uwezekano kuwa mbali na matatizo yetu ya ndani lakini diplomasia yetu kimataifa inaweza kuwa inalega na ndio chimbuko la mtikisiko mkubwa. raisi anatakiwa kuangalia timu yake ya washauri pamoja na timu inayojihusisha na diplomasia ya kimataifa ili kuona kama kunahitajika overhauling.

3. kusitishwa kwa ufadhili ni pigo kubwa sana katika bajeti yetu. hapa hakuna mjadala ni lazima bajeti ya serikali ifumuliwe na kuweka vipaumbele vipya ili kulinda uchumi wetu. lazima tutambue kuwa misaada hii ilikuwa ni source kubwa ya foreign currency. tukijidai kukusanya kodi na kutekeleza bajeti tuliyokuwa nayo ni wazi tutakumbana na mporomoko mkubwa sana kwa shilingi yetu kushuka thamani.

je wewe kama mtanzania unadhani ni kitu gani kifanyike?


Wakati umefika kurudisha kipembele cha kila mwekezaji, hasa wanaochimba madini yetu, kuhakikisha wanabakiza asilimia 60 ya mapato yote hapa Tanzania, na wao wanapeleka 40% huko nje. Yaani pesa za kigeni asilimia 60 zibaki nchini kwenye akaunti ya hazina ili Tanzania iweze ku accumulate pesa za kigeni. Hili likifanyika tutakusanya pesa ya kigeni nyingi sana. Pia kubuniwe njia nyingine ya kupata pesa za kigeni.
 
si kwamba Mahiga hawezi kazi yake. suala ni freedom ya kufanya kazi yake. kuna haja sasa uongozi wa nchi ukatambua kuwa kuna kitu kinaitwa profession na kinahitaji kuenziwa...pia tangu kuumbwa kwa ulimwengu no one has been the master of all....changamoto aliyo nayo kiongozi yoyote ni uwezo kw kujieasy na kupata ushauri kutoka kwa wasaidizi..na kuzikubali kritik za watu wenye fani yao..kiongozi ukiwa mkali sana pia wasaidizi huwa wanaogopa - - - wanarudisha majeshi nyuma kwana hakuna anayependa kumkera kiongozi.

so, nilishaandika hapa jukwaani kuwa mkuu

1. awape room wasaidizi wake kudisplay professions zao mbalimbali akiwemo mahiga.......(but sina uhakika sana kama mahiga anaweza zaidi economic diplomacy...au ni ile diplomacy ya vita na migogoro as muda mrefu amukuwa huko)

2. wataalamu wake wafanyie kazi maelekezo yake na kuyaintegrate - kuyatumia kureview economic diplomacy iliyokuwepo wakati wa Jakaya na kutengeneza sera mpya ya mambo ya nje.... ambayo itakuwa bado ni economic diplomacy lakiniinayoadress a more win win international relationship.

NB ni ukweli mkavu kuwa Dr Kikwete alitumia nguvu zake nyingi na resources nyingi za taifa kutafuta marafiki... kushindwa kucapitalise katika urafiki huo kwa kuuingiza katika awamu nyingine ya kuboresha maslahi yetu kama taifa italirudisha taifa letu miaka 50 nyuma.....mbayaaaaaaa.....

nyerere alitamani watoto wa tanzania wassome ili waweze kuendesha nchi yao wenyewe kwa faida. sasa wamesoma. ni vema tukawapa vijana wetu nafasi wakadisplay professionalism zao kwa maendeleo ya nchi

hatutaweza kuendesha nchi kwa mihemko ya kisiasa na matamko...we need to sit down and decide which way we want to go...kisha tudraft mwelekeo wetu...kisha baada ya hapo wote tunyanyuke na kutekeleza majukumu yetu....

popote pale ulipo na utakapokuwa kuna wakubwa na kuna wadogo

unaweza kuwa na hela nyingi na kila kitu...lakini ukajikuta unaenda kuomba mafuta ya taa kwa jirani..dukani wamefunga......unaweza kuwa na mabinti wengi na vijana wengi..lakini hawa hawataoana...

nimekuta watu wanapayuka kijiweni kuwa waende na hela zao...lakini nikiwauliza mikakati ya kuziba gap...hakuna hata mmoja aliyesema chochote...kimyaaaaaa

wanasema tutakata kodi ya nyumba...lakini kama ile ingekuwepo...changanya na hiyo kodi ya nyumba si tungeenda mbele zaidi??? ni kujumlisha na kutoa tu....

marekani mwenyewe na nguvu zake..anaomba sapoti akitaka kufanya vita....ni lazima tujipange.....tuache ushabiki kwenye haya mambo....tujenge taifa letu wajameni....

pamoja we can

naomba kuwasilisha.
 
kuwa na rasilimali ni sawa na mtaji na kujitegemea ni sawa na utajiri, hivyo si kila mwenye mtaji anakuwa tajiri ingawa ni vigumu kwa asiye na mtaji kuwa tajiri labda kwa kukiuka sheria.

uchumi hauna general formula kwa maana inategemea mazingira aliyonayo mhusika.

kitu cha msingi ni kutumia rasilimali hizo unazozisema kwa tija. baada ya kuwa na mtaji hiyo ni hatua ya kwanza kuelekea katika kujitegemea na tunayoyafanya kwa kutumia rasilimali zetu na kile tunachokipata kutoka huko tunakitumiaje ndiyo inayodetermine kama tutajitegemea au.

Lete mpango kazi wa kujipatia hizo foreign currency.
Na si kutegmea za kupewa na wafadhili.
Tuna raslimali nyingi, hebu ainisha, tuzitumie vipi kupata hizo foreign currency 's.
Na si za kutegmea kupewa.
 
Wakati umefika kurudisha kipembele cha kila mwekezaji, hasa wanaochimba madini yetu, kuhakikisha wanabakiza asilimia 60 ya mapato yote hapa Tanzania, na wao wanapeleka 40% huko nje. Yaani pesa za kigeni asilimia 60 zibaki nchini kwenye akaunti ya hazina ili Tanzania iweze ku accumulate pesa za kigeni. Hili likifanyika tutakusanya pesa ya kigeni nyingi sana. Pia kubuniwe njia nyingine ya kupata pesa za kigeni.

Tumbua- - - - good diplomacy will do that....not vululu vululu na makelele ya vijiweni
 
binadamu wote hawako sawa na kila mmoja alivyo inaleta mchango kwenye jamii.

kama wote tungekuwa sawa maisha haya yangekuwa magumu maana ni sawa na mwili wako kuwa na kiungo kimoja tu yaani functions zinazotoka kwa viungo vingine unazikosa.

ndugu yangu usisubiri mpaka umekosa chakula ndio uanze kuona hatari bali ukiona dalili tu za hali ya hatari chukua hatua mapema kujiepusha na hilo linaloweza kukumba. wahenga walisema kinga ni bora kuliko tiba. madhara haya ya fedha za wafadhili inawezekana yasikufikie leo lakini yasipodhibitiwa yatakufikia tu.

Pigo wewe ndio unaliona ss wengine hilo hatulijui , tunakula na kushiba mengine ni nyongeza tu. Majipu ndiyo yanaumia maana yanakosa tenda kwenye pesa za MCC.
Lowassa na Mbowe ndio wamepeleka fitina
 
Mbona mnatuchanganya! Habari kutoka Lumumba kwa Lizaboni, YEHODAYA zinasema Marekani na EU walituma maombi ya mkopo Serikalini. Baada ya kukataliwa ndio wakaanza vituko vyao alimradi waifitinishe nchi na mataifa mengine ya dunia. Wazungu sio watu wazuri sana.
Sio watu wa kucheza nao kabisa na mgufuli ndo dawa yao we tulia tu kama namuona vile magu anavyowapa kisogo siku za mbeleni
 
hizo habari zaweza kuwa sawa na mtu anayekabiliwa na matatizo alafu akaamua kwenda baa kunywa pombe ili azisahau shida zake kumbe anapojifanya hazioni ndio shida hizo huongezeka.

mwanaume hakimbii matatizo bali anakabiliana nayo.

hatuhitaji kujifanya hakuna tatizo bali ni kuangalia tatizo likoje na tulitatue vipi.

Mbona mnatuchanganya! Habari kutoka Lumumba kwa Lizaboni, YEHODAYA zinasema Marekani na EU walituma maombi ya mkopo Serikalini. Baada ya kukataliwa ndio wakaanza vituko vyao alimradi waifitinishe nchi na mataifa mengine ya dunia. Wazungu sio watu wazuri sana.
 
Pigo wewe ndio unaliona ss wengine hilo hatulijui , tunakula na kushiba mengine ni nyongeza tu. Majipu ndiyo yanaumia maana yanakosa tenda kwenye pesa za MCC.
Lowassa na Mbowe ndio wamepeleka fitina
asee wee ni bonge la ndina
 
wewe ni mwoga kwa upande mmoja lakini kwa upande mwingine unaongea ukweli.

kujitegemea ni pamoja na kuzalisha bidhaa zako na huduma zako ndani kadiri unavyoweza. sasa ukikaa kusubiri ujenge viwanda vya kuzalisha upeleke nje ndio ujitegemee ujue utaishi masikini milele na hilo hutakaa kulifikia.

japani, china, marekani au nchi za viwanda hazikuwa nchi za viwanda "over night" bali hiyo ni process inayoanzia hatua ya chini inakuzwa taratibu.

ukikaa kuangalia kuzalisha kuzalisha kuuza nje wakati hujawahi hata kuzalisha kujitosheleza mwenyewe upo uwezekano wa kuwa unaota ndoto za mchana kwa maana hauna uzoefu na pili yawezekana unatafuta wenye uzoefu waje kukodisha kwako wazalishie kwako.

kuna faida zaidi kulima shamba lako ukavuna kuliko kukodisha. ila mazingira husika ndio yanayoamua cha kufanya.

Unaweza kujijenga kiuchumi huku hauna viwanda vya kuzalisha bidhaa ambazo unaweza kuuza nchi za nje? Hapa tunachofanya ni kujifariji tu lakini kiuhalisia CCM hawapo kwa ajili ya kuhakikisha nchi inaendelea zaidi wanaangalia matumbo yao na lichama lao.
 
Screenshot_2016-04-01-16-26-48.png
huyu ndie maitarahamwe ndio yanasema uchaguzi wa haki.pumbavu zao na ma ccm


swissme
 
si kwamba Mahiga hawezi kazi yake. suala ni freedom ya kufanya kazi yake. kuna haja sasa uongozi wa nchi ukatambua kuwa kuna kitu kinaitwa profession na kinahitaji kuenziwa...pia tangu kuumbwa kwa ulimwengu no one has been the master of all....changamoto aliyo nayo kiongozi yoyote ni uwezo kw kujieasy na kupata ushauri kutoka kwa wasaidizi..na kuzikubali kritik za watu wenye fani yao..kiongozi ukiwa mkali sana pia wasaidizi huwa wanaogopa - - - wanarudisha majeshi nyuma kwana hakuna anayependa kumkera kiongozi.

so, nilishaandika hapa jukwaani kuwa mkuu

1. awape room wasaidizi wake kudisplay professions zao mbalimbali akiwemo mahiga.......(but sina uhakika sana kama mahiga anaweza zaidi economic diplomacy...au ni ile diplomacy ya vita na migogoro as muda mrefu amukuwa huko)

2. wataalamu wake wafanyie kazi maelekezo yake na kuyaintegrate - kuyatumia kureview economic diplomacy iliyokuwepo wakati wa Jakaya na kutengeneza sera mpya ya mambo ya nje.... ambayo itakuwa bado ni economic diplomacy lakiniinayoadress a more win win international relationship.

NB ni ukweli mkavu kuwa Dr Kikwete alitumia nguvu zake nyingi na resources nyingi za taifa kutafuta marafiki... kushindwa kucapitalise katika urafiki huo kwa kuuingiza katika awamu nyingine ya kuboresha maslahi yetu kama taifa italirudisha taifa letu miaka 50 nyuma.....mbayaaaaaaa.....

nyerere alitamani watoto wa tanzania wassome ili waweze kuendesha nchi yao wenyewe kwa faida. sasa wamesoma. ni vema tukawapa vijana wetu nafasi wakadisplay professionalism zao kwa maendeleo ya nchi

hatutaweza kuendesha nchi kwa mihemko ya kisiasa na matamko...we need to sit down and decide which way we want to go...kisha tudraft mwelekeo wetu...kisha baada ya hapo wote tunyanyuke na kutekeleza majukumu yetu....

popote pale ulipo na utakapokuwa kuna wakubwa na kuna wadogo

unaweza kuwa na hela nyingi na kila kitu...lakini ukajikuta unaenda kuomba mafuta ya taa kwa jirani..dukani wamefunga......unaweza kuwa na mabinti wengi na vijana wengi..lakini hawa hawataoana...

nimekuta watu wanapayuka kijiweni kuwa waende na hela zao...lakini nikiwauliza mikakati ya kuziba gap...hakuna hata mmoja aliyesema chochote...kimyaaaaaa

wanasema tutakata kodi ya nyumba...lakini kama ile ingekuwepo...changanya na hiyo kodi ya nyumba si tungeenda mbele zaidi??? ni kujumlisha na kutoa tu....

marekani mwenyewe na nguvu zake..anaomba sapoti akitaka kufanya vita....ni lazima tujipange.....tuache ushabiki kwenye haya mambo....tujenge taifa letu wajameni....

pamoja we can

naomba kuwasilisha.

..sababu zilizotolewa za kutunyima mcc ziko ndani ya uwezo wetu.

..sababu ya kwanza, ni ZANZIBAR. Kama tuliamua kufuta uchaguzi basi uchaguzi mpya ulipaswa kusimamiwa na tume huru. Mimi ningekuwa Magufuli ningewalazimisha ccm-Zanzibar na cuf wakubali kurejea ktk uchaguzi utakaosimamiwa na TUME YA KIMATAIFA itakayojumuisha UN, AU, EAC,SADC, na EU.

..Sababu ya pili ni sheria kandamizi ya Mitandao na vyombo vya habari. What is so difficult kufuta sheria hiyo na kutunga nyingine isiyobana uhuru wa wananchi kujieleza?

..ni aibu kwa Tz kukatiwa misaada kwa vigezo kwamba serikali inakandamiza haki za raia.
 
Back
Top Bottom